Tabia ya Mtoto Kunyonya Kidole!

Tafadhali usimpake kiongozi wetu wa badaaye(Mtoto) kitu chochote ili kumfanya kuacha kunyonya kidole. Ni utoto tu ataacha tu akifikia umri fulani. Ni kama mtoto kukojoa kitandani akifika umri fulani mwenyewe anaacha tu.
 

BAK sidhani kama pilipili inasaidia. mimi nimenyonya sana kidole nikaja kuacha mwenyewe nilipoenda sekondari (bording). nilipakwa sana pilipili, sikuacha. nakumbuka siku kaka yangu alinivizia nikiwa nimelala akanipaka pilipili, badala ya kuvyonya kidole nikakiweka jichoni, ilikuwa balaa. na sikuacha.
ataacha akikuwa, miaka 8 bado mdogo. akikua ataona aibu.
 
Mi nimenyonya mpaka form one ila usiku tu
na akili ilikuwepo tu lakini baada ya hapo niliacha
si ugonjwa na sidhani kama ni tatizo

FL1 kumbe wewe kama mimi?
nakumbuka nilikuwa nikilala na kidole changu mdomoni basi kama mtoto ananyonya chuchu. wenzangu walikuwa wanakusanyika kitandani kwangu nikiwa nimelala wananishangaa ninavyonyonya kidole. siku walinicheka mpaka nikaamka (niliona aibu sana) eti nikawa namwomba Mungu naomba unisaidie niache kunyonya kidole. nikaja kuacha
 

Pole saana,naona wadau wengi waliotangulia wameshatoa ushauri wao lakini kwa nitatofautiana na kukubaliana na baadhi ya wadau.uSHAURI WANGU NI KAMA UFUATAVYO

1.Muweke chini na mueleze athari ambazo anazoweza kupata kutokana na kunyonya kidole mfano minyoo n.k

2.Waweza mfunga kitambaa katika kidole anachopenda kukinyonya ili kiwe kinamualert pindi atakapo taka kukinyonya.

3.Mpe ahadi ya zawadi pindi atakapoacha kunyonya kidole N:B utakapotumia njia hii basi jaribu kunote rate yake ya kunyonya kwa saa au siku ili ujue kama imepungua au laa,pia hakikisha unampa zawadi yake kama atakuwa amesuccess.

4.Usimpe vitisho kwasababu anaweza akawa anaacha pindi akuonapo lakini akiwa peke yake atakuwa ananyonya pia vitisho vinaweza kumuathili kisaikolojia.
 
Sioni haja ya kuanzisha thread nyengine, hata hivyo naomba ruhusa kwa mwenye thread hii nitoe mchango wangu kwa kuweka nami nililonalo..

Kijana wangu 4yrs old nae alikua na tabia hiyo (ya kunyonya kidole), tulifanikiwa kumsaidia kuacha kwa kumkataza kwa maneno na wakati mwengine tulimfunga plasta.
Ila amekuja na tabia nyengine ya ajabu pia,,anachofanya sasa ni kwamba, anapokula chakula akiweka tonge moja linabaki kinywani kwa muda mrefu sana (anamung'unya) kwahiyo wakati wa kula lazima kuwe na mtu wa kumsisitiza atafune chakula na kumeza,,vyenginevyo itamchukuaa hata 2 hours kula chakula,,na mara kadhaa anapokua amelala usiku utakuta ana chakula kinywani.
Bado tunaendelea kumuelekeza lakini kama kuna njia nyengine ya kumsaidia naomba michango yenu
 
Asante mama...ila kula kucha nimeshindwa kuacha...watoto wangu nao wameiga

.........Kumbe tupo wengi tunaokula kucha, mie udogo wangu nilikuwa nanyonya kidole baadaye nilivyokuwa nikaacha kunyonya kidole nikahamia kwenye kucha. Huwezi amini hadi leo bado nakula kucha za vidole vya mkononi, natamani kuwa na kucha ndefu lakini siwezi kuvumilia kula kucha.

Sasa hivi nimeamua kukomesha hii tabia ya kula kucha, nimeamua kuweka kucha bandia na kupaka rangi ili nitakapotaka kula kucha nakutana na rangi.......lakini ninamiss kweli kweli kula kucha zangu......hivyo nimeacha kama vidole vitatu special kwa kula kucha.
 
Mimi ningekushauri umwache afaidi mpaka pale atakapoona inafaa kuacha, atakuja kuacha mwenyewe. Binafsi nimetumia sana hiyo kitu, wazazi walipiga kelel mpaka wakachoka. Pilipili walitumia sana tu, nakumbuka walishawahi kunipeleka hospital na kunipaka dawa na kufunga kama nina kidonda vile, lakini wakastaajabu kuniona asubuhi kidole kipo safi bila plaster na kipo mdomoni kama kawaida.
Lakini muda ulipofika niliacha mwenyewe.
 

Sikulijua hili. Ahsante Carmel.
 

siyo kweli hata kidogo. usitiwe hofu na maneno ya kufikirika, hakuna kitu kama hicho mama!


huyu mheshimiwa kamaliza kila kitu. huu ndio ukweli. baba uliyeleta kisa hiki, jitahidi kumsoma mwanao na utagundua mengi sana. watoto huwa wana tabia nyingi na tofauti sana, ukiwa mvivu kuwa soma na kuwaelewa utaishia kuwachukulia kirahisirahisi na utakuwa unakoseaa sana.

kuna mtoto mmoja wa kiume alikuwa na mazoea ya kushikilia sweta mknoni kwa mkono wa kushoto na kushikilia tumbo kwa mkono wa kulia kila anapotaka kulala, bila hivyo halali. wazazi hawakugundua mara moja ila walikuwa wanalalamika kuwa ni mtundu kupita kiasi na walikuwa wanchukulia kuwa kung'ang'ania sweta kila siku ni utundu wake.

nilipozungumza nao kuhusu utundu huyo mtoto wao, nilipata shauku ya kumsoma.... ndipo nilipogundua kuwa mtoto yule anajijengea na aina fulani ya hofu akilini mwake na anashika sweta na tumbo kudhibiti hofu inayompata. niliwashauri mbinu za kujitahidi kumuondolea hofu kulingana na mazingira waliyokuwa nayo, mfano wasizime taa kabla hajalala, wakitaka kuwasha redio ana televisheni wamuita awawashie na hata watafute michezo wawe wancheza naye, na wajitahidi wamnunulie kitu cha kuchezea ambacho watoto wengine pale mtaani kwao hawana. kwa kuusoma mtaa wao nilipendekeza wamnunulie mpira mkubwa kabisa kama wa kucheza watu wazima au baiskeli ya watoto au vyote kwa pamoja na wamwache huru kuchezea na kuhifadhi atakavyo.

walijitahidi wakanunua vyote, na baada ya mwezi mmoja na nusu ile tabia ilipotea hadi leo kijana ana miaka 12.
 

Nawafahamu watoto watatu ambao wazazi wao baada ya kujaribu njia mbali mbali waliamua kutumia hii ya kupaka pilipili. Hata wiki haikumalizika watoto wakaacha kabisa kunyonya vidole. Basi inategemea mtoto na mtoto, lakini namkumbuka kijana mmoja mpaka form 2 bado alikuwa ananyonya kidole. Pia kidole kama kinanyonywa kwa muda mrefu kinaweza kuharibika.
 

Mhhhh! Pretty! warembo hawali kucha bwana!!!!...umekosa vya kula? πŸ˜‰ Ziache kucha zipendeze πŸ™‚
 
Mhhhh! Pretty! warembo hawali kucha bwana!!!!...umekosa vya kula? πŸ˜‰ Ziache kucha zipendeze πŸ™‚
........Ndio maana nataka kuacha kaka yangu, maana kucha ni sehemu ya urembo ya mwanamke. Halafu hizi kucha bandia wala sijisikii kabisa kuwa comfortable nikiziweka.........hata hivyo nimeshapiga hatua katika kuacha, siku hizi nanunua candies ili nikijisikia kula kucha basi nachukua candy nakula.
 
Usimtese mwanao kwa kumkaripia wala pilipili na vitu vya namna hiyo. Jaribu kum-keep busy na shughuli zinazolingana na umri wake kama michezo nk. Akikua ataacha. Mwanangu pia alikuwa na tabia hiyo, na hasa akiwa na njaa au usingizi, nilipojaribu kumkeep busy na toys za magari na michezo ya kitoto aliacha kabisa.
 
Asante mama...ila kula kucha nimeshindwa kuacha...watoto wangu nao wameiga

Exactly! Matokeo ya kunyonya dole muda mrefu ndo hayo. Mimi ninashem wangu (female) mtu mzima ameshindwa kutunza kucha zake, anazitafuna kila zikichomoza!
Mwanangu alijaribu kufanya hivyo wakati fulani, mamake akamkanya akaacha, sielewi ndio jawabu au kijamaa kilikuwa hakijakolea, ua.
 

Hayo matatizo ya kula mimi nimeyapata sana kwa wanangu. Mkubwa alitusumbua, anakaa na msosi 2 -3 hrs, anakula chini ya robo yake. Mwanzo tulikuwa tunamshurutisha, kuna mtu katuambia tusifanye hivyo ila tujaribu good timing ya kumpa msosi, na hakikisha haumwi ila msosi uwe saa zote upo, akitaka unampa. Jamaa sasa liko 7.5 yrs, linafukia mpaka tunaogopa, mdogo wake akiringia msosi anamwambia lete hapa nikuonyeshe njia ya kuupeleka...finito! Sasa tunakimbembe cha mdogo wake, ananusa tu anakwambia nimeshiba, mda kidogo nina njaa, kidogo tu...nimeshiba. Ila tunahakikisha kila wakati kipo cha kumpa akisikia njaa...mwisho wa siku anagalau tumbo litakuwa na kitu.
Watoto wengi wanasumbua kula...nadhani mikaangizo pia haiwapi appetite, bora mara nyingi kuwapa michemsho zaidi.
 
Mimi nashauri kwamba, um-promise zawadi, kama pipi na chocolate, asiponyonya vidole kwa muda mrefu. Na, unapomfuma ananyonya tena; unamwambia kuwa, hutompa zawadi. Baada ya muda ataacha tu!!!
 
Kwema wadau,naomba mnisaidie tatizo la mtoto wangu kunyonya vidole viwili mkono wa kulia nimejaribu kumkemea imeshindikana nikajaribu kumpaka pilipili wapi naona kama tabia inamlemaza nini dawa yake?mtoto wa kike ana umri wa miaka3 anasoma

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…