Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Tabia ya Watanzania ya kuzaa hovyo ndiyo chanzo cha umaskini. Bodaboda ana watoto sita! Hata Serikali inashindwa kupanga mipango

Sexless

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2017
Posts
23,683
Reaction score
55,898
Kwa mwendo huu hakuna Rais atakayeweza kuumaliza umaskini wa nchi hii.

Ili twende sawa nitoe tafsiri ya umaskini kwa mujibu wa IMF:- umaskini ni hali ya kukosa huduma za afya/maji, chakula, elimu na mahala pazuri pa malazi (nyumba bora).

Kwa tafsiri hii, na kwa uzazi holela wa hapa nchini, ni lini kila mtanzania atakuwa na uwezo wa kuwa na nyumba bora, uwezo wa kupata huduma za afya aitakayo kwa bima ama fedha yake, uwezo wa kupata milo 3 bila shida yoyote?

Unakuta bodaboda ana watoto 6? Mama ntilie, machinga na barmaid eti nao wana familia kubwa? Nchi hii tunaenda wapi? Watu waelimishwe kuwa, siyo kila mtu lazima azae. Watoto siyo asset kwamba utakopea mkopo.

Serikali ikijenga shule ama zahanati, miaka 2 tu zimezidiwa na idadi ya watu. Hata madawati yanakuwa tatizo kila mwaka kwasababu watanzania wanafyatua watoto mno. Hakuna kitu kinawezekana bila family planning.

Dkt. Slaa alipokuwa balozi Sweden alisema "Tanzania na Sweden zilikuwa na idadi sawa ya watu mwaka 1961 (milioni 9 kila moja). Hivi sasa Sweden ina watu 15M, wakati Tanzania ina watu 60+M". Hii ni hatari.

Kwa ujinga huu wa kuzaa hovyo umaskini hautatuachia. Watu milioni 60, walipa Kodi 2M !!!

Itungwe sheria, mtu akitaka kuzaa aweke milioni 10M benki kama dhamana ya malezi bora ya mtoto.

Vinginevyo, shika, peleka akafungwe.
 
UMESHAFIKA ULAYA UKAONA WENZAKO WANAVO ZAA
12-years-12-children-family-littlehouseinthehighdesert-cover_800.png
 
Kwa mwendo huu hakuna rais atakayeweza kuumaliza umaskini wa nchi hii.

Ili twende sawa nitoe tafsiri ya umaskini kwa mujibu wa IMF:- umaskini ni hali ya kukosa huduma za afya/maji, chakula, elimu na mahala pazuri pa malazi (nyumba bora)...
Ukisoma kitabu cha "Building a Peaceful Nation: Julius Nyerere and the Establishment of Sovereignty in Tanzania 1960-1964" Dr. Paul Bjerk ameandika jinsi serikali ya kwanza kabisa ya Nyerere ilipojitahidi kufanya mipango mizuri sana ya maendeleo, lakini tatizo likawa kuwa serikali haikuangalia ongezeko la watu.

Mipango ya miaka mitano ikikamilika, inakuwa haijamaliza tatizo, kwa sababu by the time miaka mitano inaisha, idadi ya watu ineshaongezeka na kuipita sana mipango.
 
Ukisoma kitabu cha "Building a Peaceful Nation: Julius Nyerere and the Establishment of Sovereignty in Tanzania 1960-1964" Dr. Paul Bjerk ameandika jinsi serikali ya kwanza kabisa ya Nyerere ilipojitahidi kufanya mipango mizuri sana ya maendeleo, lakini tatizo likawa kuwa serikali haikuangalia onhezeko la watu.

Mipango ya miaka mitano ikikamilika, inakuwa haijamaliza tatizo, kwa sababu by the time miaka mitano inaisha, idadi ya watu ineshaongezeka na kuipita sana mipango.
Sawa kabisa mkuu. Watanzania wanazaana kama bakteria. Kapanga chumba kimoja lkn ana watoto 4. Kaah!
 
Back
Top Bottom