Tabora: Askofu KKKT, Isaac Laizer: Ataka maombi yakitaifa kukemea utekaji, mauaji

Tabora: Askofu KKKT, Isaac Laizer: Ataka maombi yakitaifa kukemea utekaji, mauaji

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Jimbo la Magharibi Tabora, Isaac Laizer, ameonya juu ya ongezeko la matukio ya utekaji na mauaji, akiwataka wakristo kote nchini kufunga na kuomba kwa dhati ili kutokomeza matukio hayo.

Akizungumza jana, Desemba 8, 2024, katika maombi ya kitaifa ya vijana yanayoendelea mkoani Tabora, Askofu Laizer amesema Taifa linakabiliwa na changamoto kubwa na maombi ya pamoja ni njia muhimu ya kufanikisha mabadiliko.

"Endapo maombi hayatafanyika kwa dhati, nchi yetu itaendelea kupitia kipindi kigumu. Tunapaswa kuungana kwa maombi ili kutokomeza utekaji na mauaji yanayoshika kasi," amesema Laizer.

Pia, amewataka wakazi wa Tabora kuachana na fikra za kutegemea miujiza badala yake wafanye kazi za kuwaingizia kipato. "Mkoa wetu unaongoza kwa watu kutosimama kidete kujitafutia maendeleo, hali inayorudisha nyuma juhudi za maendeleo ya kiuchumi."


Pia, Soma:

Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) yakemea vitendo vya utekaji, ukatili na mauaji yanayoendelea nchini

Askofu Shoo akemea vitendo vya kikatili vinavyohusisha mauaji, utekaji na matumizi mabaya ya nguvu na mamlaka

Askofu Dkt. Malasusa: Mambo ya Utekaji yafike mwisho nchi inalaanika Damu zinavyomwagika, Dkt. Biteko Wanasiasa kaeni chini msikilizane!
 
Wakuu,

Wakati taifa la Tanzania likiwa bado lina taharuki kuhusu masuala ya utekaji nchini, viongozi wa dini wameendelea kupaza sauti.

Siku ya jana, Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Jimbo la Magharibi Tabora, Isaac Laizer, ameonyesha wasiwasi kuhusu kuongezeka kwa matukio ya utekaji na mauaji akiwataka wakristo kote nchini kufunga na kuomba kwa dhati ili kutokomeza matukio hayo.


Akizungumza jana, Desemba 8, 2024, katika maombi ya kitaifa ya vijana yanayoendelea mkoani Tabora, Askofu Laizer amesema Taifa linakabiliwa na changamoto kubwa na maombi ya pamoja ni njia muhimu ya kufanikisha mabadiliko. andika hii kwa kutumia maneno mengine.


 
Kwanini tutumie nguvu yote hiyo wakati wanaofanya hayo wanafanya makusudi kabisa...tena makusudi kabisa...

Hapana,kama ni mwisho wa dunia bas iwe tu... inachosha sasa
 
Kwanini tutumie nguvu yote hiyo wakati wanaofanya hayo wanafanya makusudi kabisa...tena makusudi kabisa...

Hapana,kama ni mwisho wa dunia bas iwe tu... inachosha sasa

Kazi na sala tu mkuu

Kusali tu sali lakini pia tuwe makini na hawa watu
 
Kwanini tutumie nguvu yote hiyo wakati wanaofanya hayo wanafanya makusudi kabisa...tena makusudi kabisa...

Hapana,kama ni mwisho wa dunia bas iwe tu... inachosha sasa
Inaumiza sana hii To yeye.

Unajiuliza, hivi hii nchi au huko CCM hakuna kabisa wazee wenye busara au wazalendo?

Hivi JK kwa mfano, hawezi kabisa kuongea na Samia na kumshauri?
Mbona yeye JK alijitahidi vizuri kuongoza?

Kwani hakuna namna nyingine ya kuongoza zaidi ya utekaji?
Hawaoni kwamba utekaji ukiendelea raia hawataheshimu vyombo vya dola?

Ni mambo ya kushangaza sana.
 
Inaumiza sana hii To yeye.

Unajiuliza, hivi hii nchi au huko CCM hakuna kabisa wazee wenye busara au wazalendo?

Hivi JK kwa mfano, hawezi kabisa kuongea na Samia na kumshauri?
Mbona yeye JK alijitahidi vizuri kuongoza?

Kwani hakuna namna nyingine ya kuongoza zaidi ya utekaji?
Hawaoni kwamba utekaji ukiendelea raia hawataheshimu vyombo vya dola?

Ni mambo ya kushangaza sana.
Sad,ila kunamuda nahisi wenzake wanamzunguka ili wananchi tumchukie tumwondoshe....

Lakin kwanini watumie Mbinu hii ya kuangamiza watu😔
 

Maombi hayatosaidia chochote mpaka jeshi la polisi na vyombo vingine vya ulinzi na usalama vitengenanishwe na CCM.

Kinyume na hapo hakuna maombi yatakayofua dafu hata muitishe maombi kila mtaa .
 
Tabora: Askofu KKKT, Isaac Laizer: Ataka maombi yakitaifa kukemea utekaji, mauaji
Wakati mwingine hata hawa wapiga zomari hawaeleweki.
Ni nini mantiki ya kufanya maombi wakati watekaji wanajulikana?
Kwanini watekaji wasiambiwe wazi wazi kuwa waache mara moja kuteka na kuua raia?
 
Sad,ila kunamuda nahisi wenzake wanamzunguka ili wananchi tumchukie tumwondoshe....

Lakin kwanini watumie Mbinu hii ya kuangamiza watu😔
Wanamzunguka kivipi?

Akitekwa mtu na kuuawa kikatili wanamzunguka na kumwambia aseme kifo ni kifo tu?!
 
Sadaka tu hapo inatafutwa katika tukio hilo.
Hawa viongozi wa dini ni sehemu ya wanaotumika kubariki hayo matukio ya kikatili ukimuondoa Mwamakula.
 
Usalama wa Watanzania ni muhimu kuliko Ujenzi wa barabara na madarasa.
 
Back
Top Bottom