Tabora: Jiko la mkaa laua watoto wawili kwa kukosa hewa ya kutosha

Tabora: Jiko la mkaa laua watoto wawili kwa kukosa hewa ya kutosha

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Watoto wawili wa familia moja katika kijiji cha Usuhilo Manispaa ya Tabora, wamefariki dunia kwa kukosa hewa ya kutosha baada ya wazazi wao kuwasha jiko la mkaa na kuliweka ndani ili waote moto na kujikinga na baridi. Watoto waliofariki ni Amani Athumani, (1) na Zainabu Athumani (1). Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora ACP Richard Abwao amesema tukio hilo limetokea February 5, 2022 majira ya saa 6 usiku

Baba wa Watoto hao Athumani Shabani (45), Mkewe Magreth Joseph (34) pamoja na Neema Athumani (17) wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tabora Kitete kutokana na kuathirika kwa kukosa hewa pia kulikosababishwa na jiko hilo la mkaa na hali zao sio nzuri.

Sababu zinazoweza kusababisha kifo kutokana na jiko la mkaa. soma Kwanini jiko la mkaa ukiwa ndani linaweza kupelekea vifo

Visa mbalimbali vya vifo vitokanavyo na jiko la mkaa

pic-gesi-data.jpg
 
Watu hawajifunzi tuu kwamba ukilala na jiko ndani unapoteza uhai
 
Wizara ya Afya izunguke vijijini sehemu zenye baridi kutoa elimu,nashangaa bado watu wanatumia majiko ya mkaa ndani huku kukiwa hakuna circulation nzuri ya hewa.
 
hii kitu naona fire na uokoaji wameitelekeza wakati ni jukumu lao kabisa kutoa elimu kuhusu hili jambo.

wenzao police kupitia traffic wameanza kuingia mashuleni kutoa elimu za usalama barabarani.
nao wanatakiwa waandaliwe vipindi wawe wanapita mashuleni.
 
Back
Top Bottom