Tabu kwa waliokuwa karibu na Mzee Kitwana Selemani Kondo kuacha kumkumbuka

Tabu kwa waliokuwa karibu na Mzee Kitwana Selemani Kondo kuacha kumkumbuka

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Rafiki yangu Salum Matimbwa ametukumbusha baba yetu Mzee Kitwana Selemani Kondo. Kanirudisha nyuma mbali sana.

Namkumbuka Kitwana Kondo na Peugeot yake 404 rangi ya kijani ameiegesha pembeni anazungumza Pan Africa, club iliyojitenga na Yanga.

Mzee Kondo hii rangi ya kijani ni kwa kuwa alikuwa mpenzi ya Yanga. Wakati huo sikuwa namfahamu kwa karibu ila kwa kumuona tu.

Alipokuja kunijua alinambia kuwa akimfahamu sana baba yangu na akaniambia kuwa katika ujana wake alipata kupanga nyumba ya mmoja wa bibi zangu Bi. Asha bint Farjallah maarufu akijulikana kama Mama Salehe.

Nyumba hii ilikuwa Mtaa wa Likoma mwisho.

Mama Salehe alikuwa make wa Sheikh Yassin ambae sisi tumezaliwa hakutumkuta alikuwa keshafariki.

Tulichokikuta pale ni madrasa yake ambayo bibi yangu aliiendesha hadi kifo chake na kumbukumbu yangu ya utoto ya madrasa hii ni ile Maulidi ya Mfungo Sita kila mwaka na kipunga chake.

Sisi wajukuu tulikuwa lazima tuhudhurie maulidi ile.

Huyu Salehe ni baba yangu mdogo kwa kuwa mama yake Bi. Asha na mama yake baba yangu Bi. Zena walikuwa ndugu wote mabint Farjallah na alikuwa mtoto pekee wa huyu bibi yangu.

Bwana Salehe akifanya kazi Dar es Salaam Club toka enzi ya ukoloni.

Ninachomkumbuka baba yangu huyu mdogo ni utanashati wake.

Huyu ndiye baba yake Yassin Saleh aliyekuja kuwa golikipa maarufu kufika gadi kucheza Taifa Stars.

Mzee Saleh alikuwa rafiki sana na Mzee Kondo na Dar es Salaam Club ilipofungwa na baba yangu kujikuta hana kazi Mzee Kondo alimpa kazi State Motor Corporation ambako yeye alikuwa Mkurugenzi Mkuu.

Ninapomkumbuka Mzee Kiwana Kondo huja na kumbukumbu za hawa wazee wangu pia na nyakati zao mimi nikiwa mtoto.

Mzee Kondo kaondoka na mengi ndani ya kifua chake.

Lakini kwangu mimi kitu kikubwa alichoniachia kabla ya kufariki kwake ni kunipa jina la kachero wa serikali ya Waingereza aliyekuwa akiwachimba viongozi wa TANU bila ya wao wenyewe kufahamu, taarifa zao zote akiziwasilisha Government House kwa Gavana Edward Francis Twining kwa mdomo.

Sikumuomba Mzee Kondo taarifa hii yeye mwenyewe tu niko nyumbani kwake kwa ajili ya mahojiano ya kipindi cha televisheni aliniita akanimabia nikae pembeni yake ana jambo anataka kuniambia na akaniusia kuwa nisiandike yale atakayonieleza hadi yeye akiwa kesha ondoka duniani.

Mzee Kondo akaniuma sikio na kwa kweli aliyonieleza yalinifungulia kitendawili ambacho kilikuwa kikitaabisha akili yangu kwa miaka mingi kuwa vipi Waingereza waliwafikia Rashid Ali Meli na Iddi Faiz Mafungo kwa urahisi na wakamkamata Iddi Faizi Turiani akitokea Tanga kwa Mwalimu Kihere alipokwenda kuchukua fedha za safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955?

Picha hiyo hapo chini tulipiga siku Mzee Kondo aliponifungulia mlango wa moyo wake kwa upenyo mdogo tu nichungulie ndani.
Mzee Kondo kaingia kaburini na historia kubwa sana ya uhuru wa Tanganyika na mengi mengine.

Image may contain: 1 person, sitting
 
Mzee Mohamed Shikamoo mbona hujamtaja huyo Kachero au basi tuambie tu alikuwa muafrica mwenzetu au mzungu?
 
Mzee Mohamed Shikamoo mbona hujamtaja huyo Kachero au basi tuambie tu alikuwa muafrica mwenzetu au mzungu?
Nostra...
Mbona nilishamtaja hapa huyu kachero tena kwa jina?

Aliongozana na Abdul Sykes kwenda Nansio kwa Hamza Mwapachu mwanzoni mwa mwaka wa 1953.

Madhumuni ya safari hii ilikuwa Abdul Sykes akiwa Act. President wa TAA na Secretary alitaka kupata kauli ya mwisho ya Mwapachu kabla ya mkutano wa TAA mwaka wa 1953 kuhusu kumuingiza Julius Nyerere katika uongozi wa juu wa chama.

Ilikuwa baada ya mkutano huu wa 1953 mkutano wa 1954 waunde TANU.

Huyu bwana alishiriki katika majadiliano haya na Mwapachu alisisitiza kuwa Abdul ampishe Nyerere kwenye nafasi ya President na amsaidie kushinda uchaguzi ule ili Nyerere aongoze harakati za kudai uhuru watakapounda TANU mwaka unaokuja 1954.

Waingereza wakawa wamepewa taarifa hizi zote.

Nakupa ''homework,'' mtafute humu utamjua.
 
Rafiki yangu Salum Matimbwa ametukumbusha baba yetu Mzee Kitwana Selemani Kondo. Kanirudisha nyuma mbali sana.

Namkumbuka Kitwana Kondo na Peugeot yake 404 rangi ya kijani ameiegesha pembeni anazungumza Pan Africa, club iliyojitenga na Yanga.

Mzee Kondo hii rangi ya kijani ni kwa kuwa alikuwa mpenzi ya Yanga. Wakati huo sikuwa namfahamu kwa karibu ila kwa kumuona tu.

Alipokuja kunijua alinambia kuwa akimfahamu sana baba yangu na akaniambia kuwa katika ujana wake alipata kupanga nyumba ya mmoja wa bibi zangu Bi. Asha bint Farjallah maarufu akijulikana kama Mama Salehe.

Nyumba hii ilikuwa Mtaa wa Likoma mwisho.

Mama Salehe alikuwa make wa Sheikh Yassin ambae sisi tumezaliwa hakutumkuta alikuwa keshafariki.

Tulichokikuta pale ni madrasa yake ambayo bibi yangu aliiendesha hadi kifo chake na kumbukumbu yangu ya utoto ya madrasa hii ni ile Maulidi ya Mfungo Sita kila mwaka na kipunga chake.

Sisi wajukuu tulikuwa lazima tuhudhurie maulidi ile.

Huyu Salehe ni baba yangu mdogo kwa kuwa mama yake Bi. Asha na mama yake baba yangu Bi. Zena walikuwa ndugu wote mabint Farjallah na alikuwa mtoto pekee wa huyu bibi yangu.

Bwana Salehe akifanya kazi Dar es Salaam Club toka enzi ya ukoloni.

Ninachomkumbuka baba yangu huyu mdogo ni utanashati wake.

Huyu ndiye baba yake Yassin Saleh aliyekuja kuwa golikipa maarufu kufika gadi kucheza Taifa Stars.

Mzee Saleh alikuwa rafiki sana na Mzee Kondo na Dar es Salaam Club ilipofungwa na baba yangu kujikuta hana kazi Mzee Kondo alimpa kazi State Motor Corporation ambako yeye alikuwa Mkurugenzi Mkuu.

Ninapomkumbuka Mzee Kiwana Kondo huja na kumbukumbu za hawa wazee wangu pia na nyakati zao mimi nikiwa mtoto.

Mzee Kondo kaondoka na mengi ndani ya kifua chake.

Lakini kwangu mimi kitu kikubwa alichoniachia kabla ya kufariki kwake ni kunipa jina la kachero wa serikali ya Waingereza aliyekuwa akiwachimba viongozi wa TANU bila ya wao wenyewe kufahamu, taarifa zao zote akiziwasilisha Government House kwa Gavana Edward Francis Twining kwa mdomo.

Sikumuomba Mzee Kondo taarifa hii yeye mwenyewe tu niko nyumbani kwake kwa ajili ya mahojiano ya kipindi cha televisheni aliniita akanimabia nikae pembeni yake ana jambo anataka kuniambia na akaniusia kuwa nisiandike yale atakayonieleza hadi yeye akiwa kesha ondoka duniani.

Mzee Kondo akaniuma sikio na kwa kweli aliyonieleza yalinifungulia kitendawili ambacho kilikuwa kikitaabisha akili yangu kwa miaka mingi kuwa vipi Waingereza waliwafikia Rashid Ali Meli na Iddi Faiz Mafungo kwa urahisi na wakamkamata Iddi Faizi Turiani akitokea Tanga kwa Mwalimu Kihere alipokwenda kuchukua fedha za safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955?

Picha hiyo hapo chini tulipiga siku Mzee Kondo aliponifungulia mlango wa moyo wake kwa upenyo mdogo tu nichungulie ndani.
Mzee Kondo kaingia kaburini na historia kubwa sana ya uhuru wa Tanganyika na mengi mengine.

Image may contain: 1 person, sitting
Sheikh Mohamed: una tabia nimeiona tangu zamani, unachoandika huwa unaongea kana kwamba ni hicho hicho hakuna kingine. Mhe KK mie alinipa Kadi yangu uasisi CCM mwaka 1977 nikiwa Mhadhiri pale IFM, yeye Mwenyekiti Ilala (W) aliandamana na kada toka Zanzibar jina lake Seif Bakari. Titbits ziko nyingi tu, mathalani tulikuwa na Walimu wawili Audit na Mwanafunzi mmoja kabila lao tukijua ni Wahangaza: kufika1994 tukasikia wako msituni RPF baadaye wakawa maafisa waandamizi Banki Nkuru y'Rwanda na bungeni kwao kumbe Watutsi. Mengi tu, walimu tulikuwa wengine toka UK wengine US wengine USSR wengine Bangladesh - minyukano na hadaa na mbwembwe kama kazi. Hapa sijataja (kama ingekuwa wewe) Waislamu kudogoshwa wala Wamanyema kuongoza, lakini post si imenoga?
 
Sheikh Mohamed: una tabia nimeiona tangu zamani, unachoandika huwa unaongea kana kwamba ni hicho hicho hakuna kingine. Mhe KK mie alinipa Kadi yangu uasisi CCM mwaka 1977 nikiwa Mhadhiri pale IFM, yeye Mwenyekiti Ilala (W) aliandamana na kada toka Zanzibar jina lake Seif Bakari. Titbits ziko nyingi tu, mathalani tulikuwa na Walimu wawili Audit na Mwanafunzi mmoja kabila lao tukijua ni Wahangaza: kufika1994 tukasikia wako msituni RPF baadaye wakawa maafisa waandamizi Banki Nkuru y'Rwanda na bungeni kwao kumbe Watutsi. Mengi tu, walimu tulikuwa wengine toka UK wengine US wengine USSR wengine Bangladesh - minyukano na hadaa na mbwembwe kama kazi. Hapa sijataja (kama ingekuwa wewe) Waislamu kudogoshwa wala Wamanyema kuongoza, lakini post si imenoga?
LGF,
Sijui kwa nini umefikiria hivyo kuwa mimi najichukulia kuwa ndiyo mwisho.

Yapo mengine nami natambua hilo na ndiyo maana nami nikaandika kuongozea kama wewe ulivyofanya hapa.

Umeongeza baada ya kuona lipo la kusemwa.
Kama nisingeandika kuhusu Waislam na Wamanyema historia hii isingefahamika.

Historia iliyokuwa inatakiwa iwepo ni ile ya Chuo Cha CCM Kivukoni iliyoandikwa mwaka wa 1981 iliyowafuta wazee wangu.

Mimi nitakaa kimya vipi ilhali wazee wangu ndiyo waliounda TANU na hawaonekani popote?

Nikiwashangaza walimu wangu pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam walipokuwa wakisomesha historia siyo na nikiwaambia msiniulize rejea hicho chama babu yangu alikuwapo toka siku ya kwanza na wengi katika waasisi wa TANU wakija hadi nyumbani kwetu.

Namtaja Dome Okochi Budohi (TANU Card no. 5).
Kishindo kilikuwa kizito.

Ulikuwa unayajua haya?

Hilo la kudogoshwa Waislam wala si lako kulisemea.

Wanaohusika wamekaa kimya kwa muda mrefu sana hata pale Mzee Kitwana Kondo alipouliza Bungeni mwaka wa 1999 kuwa mbona takwimu za uchaguzi wa vijana kuingia sekondari zinaelemea upande mmoja tu?

Wizara ya Elimu ilibakia kimya.

Nakusihi hili tusiliguse tubakie na historia ya Iddi Faizi Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU na mkusanyanyi wa fedha za safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955 lakini historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika imemsahau.

1611632438484.png

Kushoto: Iddi Faiz Mafungo (TANU Card no. 24), Sheikh Mohamed Ramiyya, Julius Nyerere (TANU Card no. 1), Saadan Abdul Kandoro na Haruna Taratibu Dodoma Railway Station 1955/56

1611632752639.png
 
Dah maneno mujarabu haya

Dagii,
Hakika maneno yake mazuri hata mie yamenifurahisha na nampa zawadi hii ya picha yangu na Dome Okochi Budohi Nairobi 1972 kiongozi TAA 1953 na kadi yake ya TANU ni no. 5.

1611633783271.png
 
Rafiki yangu Salum Matimbwa ametukumbusha baba yetu Mzee Kitwana Selemani Kondo. Kanirudisha nyuma mbali sana.

Namkumbuka Kitwana Kondo na Peugeot yake 404 rangi ya kijani ameiegesha pembeni anazungumza Pan Africa, club iliyojitenga na Yanga.

Mzee Kondo hii rangi ya kijani ni kwa kuwa alikuwa mpenzi ya Yanga. Wakati huo sikuwa namfahamu kwa karibu ila kwa kumuona tu.

Alipokuja kunijua alinambia kuwa akimfahamu sana baba yangu na akaniambia kuwa katika ujana wake alipata kupanga nyumba ya mmoja wa bibi zangu Bi. Asha bint Farjallah maarufu akijulikana kama Mama Salehe.

Nyumba hii ilikuwa Mtaa wa Likoma mwisho.

Mama Salehe alikuwa make wa Sheikh Yassin ambae sisi tumezaliwa hakutumkuta alikuwa keshafariki.

Tulichokikuta pale ni madrasa yake ambayo bibi yangu aliiendesha hadi kifo chake na kumbukumbu yangu ya utoto ya madrasa hii ni ile Maulidi ya Mfungo Sita kila mwaka na kipunga chake.

Sisi wajukuu tulikuwa lazima tuhudhurie maulidi ile.

Huyu Salehe ni baba yangu mdogo kwa kuwa mama yake Bi. Asha na mama yake baba yangu Bi. Zena walikuwa ndugu wote mabint Farjallah na alikuwa mtoto pekee wa huyu bibi yangu.

Bwana Salehe akifanya kazi Dar es Salaam Club toka enzi ya ukoloni.

Ninachomkumbuka baba yangu huyu mdogo ni utanashati wake.

Huyu ndiye baba yake Yassin Saleh aliyekuja kuwa golikipa maarufu kufika gadi kucheza Taifa Stars.

Mzee Saleh alikuwa rafiki sana na Mzee Kondo na Dar es Salaam Club ilipofungwa na baba yangu kujikuta hana kazi Mzee Kondo alimpa kazi State Motor Corporation ambako yeye alikuwa Mkurugenzi Mkuu.

Ninapomkumbuka Mzee Kiwana Kondo huja na kumbukumbu za hawa wazee wangu pia na nyakati zao mimi nikiwa mtoto.

Mzee Kondo kaondoka na mengi ndani ya kifua chake.

Lakini kwangu mimi kitu kikubwa alichoniachia kabla ya kufariki kwake ni kunipa jina la kachero wa serikali ya Waingereza aliyekuwa akiwachimba viongozi wa TANU bila ya wao wenyewe kufahamu, taarifa zao zote akiziwasilisha Government House kwa Gavana Edward Francis Twining kwa mdomo.

Sikumuomba Mzee Kondo taarifa hii yeye mwenyewe tu niko nyumbani kwake kwa ajili ya mahojiano ya kipindi cha televisheni aliniita akanimabia nikae pembeni yake ana jambo anataka kuniambia na akaniusia kuwa nisiandike yale atakayonieleza hadi yeye akiwa kesha ondoka duniani.

Mzee Kondo akaniuma sikio na kwa kweli aliyonieleza yalinifungulia kitendawili ambacho kilikuwa kikitaabisha akili yangu kwa miaka mingi kuwa vipi Waingereza waliwafikia Rashid Ali Meli na Iddi Faiz Mafungo kwa urahisi na wakamkamata Iddi Faizi Turiani akitokea Tanga kwa Mwalimu Kihere alipokwenda kuchukua fedha za safari ya kwanza ya Julius Nyerere UNO mwaka wa 1955?

Picha hiyo hapo chini tulipiga siku Mzee Kondo aliponifungulia mlango wa moyo wake kwa upenyo mdogo tu nichungulie ndani.
Mzee Kondo kaingia kaburini na historia kubwa sana ya uhuru wa Tanganyika na mengi mengine.

Image may contain: 1 person, sitting
Yasin Salehe na Badi Salehe aliyekuwa kocha wa yanga na sigara ni ndugu au majina tu yametokea kufanana
 
LGF,
Sijui kwa nini umefikiria hivyo kuwa mimi najichukulia kuwa ndiyo mwisho.

Yapo mengine nami natambua hilo na ndiyo maana nami nikaandika kuongozea kama wewe ulivyofanya hapa.

Umeongeza baada ya kuona lipo la kusemwa.
Kama nisingeandika kuhusu Waislam na Wamanyema historia hii isingefahamika.

Historia iliyokuwa inatakiwa iwepo ni ile ya Chuo Cha CCM Kivukoni iliyoandikwa mwaka wa 1981 iliyowafuta wazee wangu.

Mimi nitakaa kimya vipi ilhali wazee wangu ndiyo waliounda TANU na hawaonekani popote?

Nikiwashangaza walimu wangu pale Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam walipokuwa wakisomesha historia siyo na nikiwaambia msiniulize rejea hicho chama babu yangu alikuwapo toka siku ya kwanza na wengi katika waasisi wa TANU wakija hadi nyumbani kwetu.

Namtaja Dome Okochi Budohi (TANU Card no. 5).
Kishindo kilikuwa kizito.

Ulikuwa unayajua haya?

Hilo la kudogoshwa Waislam wala si lako kulisemea.

Wanaohusika wamekaa kimya kwa muda mrefu sana hata pale Mzee Kitwana Kondo alipouliza Bungeni mwaka wa 1999 kuwa mbona takwimu za uchaguzi wa vijana kuingia sekondari zinaelemea upande mmoja tu?

Wizara ya Elimu ilibakia kimya.

Nakusihi hili tusiliguse tubakie na historia ya Iddi Faizi Mafungo Mweka Hazina wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na TANU na mkusanyanyi wa fedha za safari ya Mwalimu Nyerere UNO 1955 lakini historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika imemsahau.

View attachment 1686316
Kushoto: Iddi Faiz Mafungo (TANU Card no. 24), Sheikh Mohamed Ramiyya, Julius Nyerere (TANU Card no. 1), Saadan Abdul Kandoro na Haruna Taratibu Dodoma Railway Station 1955/56

View attachment 1686318
Mzee MS kuna picha hapo ya hao wabibi na nyerere Yericko Nyerere anadai ni masista wa maryknol
 
Unamaanisha Dome Okochi Budohi alikuwa kachero au ni titbits tu kama za LGF?
FPS,
Dome Okochi Budohi hakuwa kachero.

Huyu alikuwa Mluya kutoka Kenya aliyekuja kutafuta maisha Tanganyika na akashiriki katika siasa za TAA na TANU.

Alikamatwa kwa mwaka wa 1955 kwa kushukiwa ni Mau Mau akafungwa kisiwani Lamu, Kenya hadi mwaka wa 1963.

Nimemwandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kachero ndani ya TAA alikuwa Alexander Thobias.

Huyu alimchimba sana Abdul Sykes hadi 1954 alipogundulika.
 
FPS,
Dome Okochi Budohi hakuwa kachero.

Huyu alikuwa Mluya kutoka Kenya aliyekuja kutafuta maisha Tanganyika na akashiriki katika siasa za TAA na TANU.

Alikamatwa kwa mwaka wa 1955 kwa kushukiwa ni Mau Mau akafungwa kisiwani Lamu, Kenya hadi mwaka wa 1963.

Nimemwandika kwa kirefu katika kitabu cha Abdul Sykes.

Kachero ndani ya TAA alikuwa Alexander Thobias.

Huyu alimchimba sana Abdul Sykes hadi 1954 alipogundulika.
Mkuu huyu Snitch alikua anatokea wapi n mbn historia imeishia kwake tu, mke wake ni yupi na watoto wake je
 
Mkuu huyu Snitch alikua anatokea wapi n mbn historia imeishia kwake tu, mke wake ni yupi na watoto wake je
Shark,
Unamkusudia Mole yupi huyu ambae sijamtaja jina au Alexander Thobias?
 
Kwan c umesema ni Alexander au walikua na mwenzake
Shark,
Kisa hiki kimetoka nyuma kidogo.

Nilieleza kuhusu jina la kachero nililopewa na Mzee Kondo kwa sharti nisilitaje hadi yeye akiwa kesha fariki.

Kuna msomaji akataka niliseme.

Nikamwambia nimelitaja hapa barzani siku za nyuma alitafute.
 
Shark,
Kisa hiki kimetoka nyuma kidogo.

Nilieleza kuhusu jina la kachero nililopewa na Mzee Kondo kwa sharti nisilitaje hadi yeye akiwa kesha fariki.

Kuna msomaji akataka niliseme.

Nikamwambia nimelitaja hapa barzani siku za nyuma alitafute.
Umemtaja kwenye Uzi upi sheikh tumtafute
 
Ndiyo 'raha' ya Nchi kuwa na makachero. Mzee Kitwana 'smart' , akaitia Nchi mbele ili iendelee kuwa na mtangamano. Akiwa kule mtetezi 'wetu', akiwa kazini 'Mzalendo! Basi wote mnaoonekana watetezi wa kundi fulani na mnasikilizwa lazima muwekwe karibu na kujiona mna Mtu muhimu sana anayewapa 'mazito'.

Hii kazi ilishawahi kumpa tabu sana Mwanazuoni mmoja mahiri Nchini, akiwa na uwezo mkubwa wa akili kuchambua mambo mazito. Siku 'walipomwambia' afanye about turn kidogo asijisahau sana ilimpa tabu sana, lakini alikumbuka kiapo akarudi mstarini.

Nimemkumbuka sana Shehe na Mzee wetu Marehemu mtabiri maarufu (huyu Bwana Mwijage aliyekuwa mpinzani wa Mwalimu na akiishi uhamishoni hawezi kumsahau). Nakumbuka nilivyokuwa Sekondari ndiyo kilikuwa kipindi chake cha 'kuihenyesha' Serikali. Alikuwa machachari kweli, ila baadaye naona akapiga breki. Labda alichoka!!

Sijui kwa nini picha ya Balozi wetu Malaysia na Profesa ngangari imenijia ghafla!
Hii Nchi Nyerere aliifunda, ingawa natofautiana naye kwenye sera za Uchumi.
 
Back
Top Bottom