Mama Anne Makinda,
Nimeona leo mahali unasema vyombo vya habari vimuache Pius Msekwa kwani kalitumikia taifa kwa muda mrefu na sasa ni mstaafu.
Mama Makinda, Pius Msekwa hajastaafu kutumia haki yake ya kutoa maoni kama Katiba inavyomruhusu.
Tatizo siyo Msekwa, tatizo ni wewe hutaki Msekwa aseme kwamba akina Halima Mdee si wabunge tena tangu walipovuliwa uanachama.
Msekwa kanukuu ibara ya 71(1)(e) sasa wewe ulitaka awe kipofu kwa ibara hiyo.
Sasa mama Makinda ngoja nikufundishe mambo matatu inayoelekea huyajui.
Jambo la kwanza ni kwamba Pius Msekwa ndiye mtu pekee aliyebaki hai aliyeshiriki kamati ya kuiunda Katiba hii mwaka 1977.
Kumbuka Mwenyekiti wa kamati hiyo ni alikuwa hayati Thabit Kombo na katibu akawa ni huyu Msekwa.
Wewe ulikuwa wapi wakati huo maana historia haikutaji.
Hivyo Pius Msekwa ni mtunzi wa Katiba yetu bila kujali ni mbovu au nzuri.
Waandishi wanamfuata kwa sababu ni mtungaji wa hiyi Katiba hawakufuati wewe uliyepata uspika kwa kigezo cha Samwel Sitta kukosa jinsia ya Kike mwaka 2010.
Jambo la pili ni kwamba Pius Msekwa ndiye kiongozi pekee ndani ya CCM kuandika vitabu vingi na vinasomwa duniani kote.
Ndiye msomi pekee aliyeandika mengi kuhusu Bunge. Wewe huna article hata ya page moja kwenye gazeti lolote.
Jambo la tatu ni kwamba wiki juzi wakati Bunge hili linazinduliwa Pius Msekwa alialikwa kwenye semina ya wabunge na akatoa lecture nzuri.
Katika semina hiyo Spika Job Ndugai kawaambia kwamba wasiishie kumsikiliza Msekwa kwenye semina ile tu bali wachimbue vitabu vyake vilivyojazana kwenye library ya Bunge.
Jambo la nne ni kwamba kama unataka, japo huwezi, mwambie Pius Msekwa aache kuandika makala zake za "The Current Affairs" kila Alhamsi kwenye gazeti la Daily News.
Serekali inamtumia kila Alhamis kwenye Daily News halafu leo EATV wamemhoji unapiga kelele.
Hivyo kama wewe uliamua kuandika historia ya kukaa kimya basi acha dunia ya wasomi inayomheshimu Msekwa tumheshimu.
Msekwa ndiye mtu pekee ndani ya CCM anayeweza kuongea na wapinzani wakajibizana naye.
Cha muhimu ishauri CCM ipike vijana ma genious kama Nyerere alivyowapika hawa akina Msekwa na siyo hawa wa sasa hivi ambao wakiamka asubuhi wanatafuta tusifie lipi.
Nimeona leo mahali unasema vyombo vya habari vimuache Pius Msekwa kwani kalitumikia taifa kwa muda mrefu na sasa ni mstaafu.
Mama Makinda, Pius Msekwa hajastaafu kutumia haki yake ya kutoa maoni kama Katiba inavyomruhusu.
Tatizo siyo Msekwa, tatizo ni wewe hutaki Msekwa aseme kwamba akina Halima Mdee si wabunge tena tangu walipovuliwa uanachama.
Msekwa kanukuu ibara ya 71(1)(e) sasa wewe ulitaka awe kipofu kwa ibara hiyo.
Sasa mama Makinda ngoja nikufundishe mambo matatu inayoelekea huyajui.
Jambo la kwanza ni kwamba Pius Msekwa ndiye mtu pekee aliyebaki hai aliyeshiriki kamati ya kuiunda Katiba hii mwaka 1977.
Kumbuka Mwenyekiti wa kamati hiyo ni alikuwa hayati Thabit Kombo na katibu akawa ni huyu Msekwa.
Wewe ulikuwa wapi wakati huo maana historia haikutaji.
Hivyo Pius Msekwa ni mtunzi wa Katiba yetu bila kujali ni mbovu au nzuri.
Waandishi wanamfuata kwa sababu ni mtungaji wa hiyi Katiba hawakufuati wewe uliyepata uspika kwa kigezo cha Samwel Sitta kukosa jinsia ya Kike mwaka 2010.
Jambo la pili ni kwamba Pius Msekwa ndiye kiongozi pekee ndani ya CCM kuandika vitabu vingi na vinasomwa duniani kote.
Ndiye msomi pekee aliyeandika mengi kuhusu Bunge. Wewe huna article hata ya page moja kwenye gazeti lolote.
Jambo la tatu ni kwamba wiki juzi wakati Bunge hili linazinduliwa Pius Msekwa alialikwa kwenye semina ya wabunge na akatoa lecture nzuri.
Katika semina hiyo Spika Job Ndugai kawaambia kwamba wasiishie kumsikiliza Msekwa kwenye semina ile tu bali wachimbue vitabu vyake vilivyojazana kwenye library ya Bunge.
Jambo la nne ni kwamba kama unataka, japo huwezi, mwambie Pius Msekwa aache kuandika makala zake za "The Current Affairs" kila Alhamsi kwenye gazeti la Daily News.
Serekali inamtumia kila Alhamis kwenye Daily News halafu leo EATV wamemhoji unapiga kelele.
Hivyo kama wewe uliamua kuandika historia ya kukaa kimya basi acha dunia ya wasomi inayomheshimu Msekwa tumheshimu.
Msekwa ndiye mtu pekee ndani ya CCM anayeweza kuongea na wapinzani wakajibizana naye.
Cha muhimu ishauri CCM ipike vijana ma genious kama Nyerere alivyowapika hawa akina Msekwa na siyo hawa wa sasa hivi ambao wakiamka asubuhi wanatafuta tusifie lipi.