Tafadhali Anne Makinda jihadhari kwani Pius Msekwa si saizi yako. Msekwa katumia usomi kusema akina Halima Mdee wamefutwa Ubunge

Kunatofauti Kati ya kufurahisha na kuongea kitu sahihi.
Ni kweli kabisa ila hawa watu ninaowazungumzia hawangalii usahihi wanaangalia kama kilichozungumzwa kinaendana na msimamo wao hivyo kinaweza kuwa sahihi ama kisiwe sahihi,na hapo ndio neno "kufarahisha" linapotokea.

Hali hiyo ndio maana kunakuwa na watu wenye kusema ukweli ila kwa upande fulani tu,unakuta mfano labda chama A kikikosea huyo mtu hukosoa kwa hoja sahihi kabisa ila chama B kikikosea huyo mtu ananyamazia kimya hata kama anazo hoja sahihi kabisa za kukosoa hilo jambo.
 
Wewe wa ajabu kweli bilashaka utakuwa kilaza wewe hivi umesoma na kuelewa vizuri maoni ya Mama Makinda? Hoja yako haina mashiko umekurupuka usimlishe mama Makinda maneno yako.
Na wewe hujasema aliyo yasema mama Makinda .
 
Tatizo ni kwamba leo Msekwa ataonekana mtu wa maana kwa sababu kaongea jambo lenye kuwafurahisha watu fulani ila Msekwa huyohuyo siku nyengine akiongea jambo lisilowafurahisha hata kama ndio ukweli basi ataonekana ni hovyo.

Tuache hii tabia.
Kwani lazima aongee msekwa tu, mbona katiba ipo wazi Sana labda uamue kukaza fuvu kama Wenzio WA lumumba
 
Mzee Msekwa anatumika sana kutetea maamuzi ya kisiasa yenye utata ya watawala wetu. Mara nyingi utetezi wake haukidhi matarajio ya wengi. Lakini angalau amejijengea jina nchini na mdani ya ccm kama "theoretician". Anazumgumza na kuweka mawazo kwenye maamdishi hata kuna watu hawakubaliani naye. Tofauti sana ma viongozi wetu wengi. Kuna wakati watu walimshabikia sana mwamasiasa mmoja na kumpatia umaarufu bila sababu wala vigezo vyovyote vinavyofahamika. Mwanasiasa huyo alifanikiwa kisiasa na kushika madaraka makubwa. Hapo ndipo watu walipoanza kufuatilia matarajio yao. Hawakuridhishwa na walibaini kuwa walikuwa wakifuata mkumbo tu; walidanganyika. Mwandishi mmoja nguli akahitimisha kwamba holi ni kosa la kumshabikia mwanasiasa ambaye hajapata hata kuandika chochote kwenye karatasi kuhusu mawazo yake kisiasa watu wengine wakasoma na kujua angalau yeye ana mtazamo gani.
 
Tuwekee rejea, usituwee hisia zako. Mzee Msekwa amejibu kulingana na alivyoulizwa na mwandishi na akarejea Katiba ya nchi. Kama umemsikiliza vizuri yeye wala hakujikita kwenye ule uhuni uliofanywa na NEC pamoja na mzee Ndugai. Yeye amejibu kana kwamba wale Covid-19 walikuwa "wabunge halali" ila madam chama kimewatema, basi Ndugai asijiingize kabisa kwenye jambo hilo.
Kama unakumbuka vizuri, Ndugai wanapofukuzwa na vyama vyao wabunge wa upinzani, hasa katika mazingira ambayo CCM kina maslahi, amekuwa akiwakingia mkono akidai Bunge lina wajibu wa "kuwatetea wabunge", lakini kauli hii ya mzee Msekwa inamvua nguo Ndugai, na kumwonyesha kama Spika wa hovyo kabisa nchi hii kuwahi kumpata!
 
Uongo au makosa ya mkubwa yana maana zaidi kuliko ukweli au usahihi wa mdogo.
The Boss is always right.
Kwa mantiki hii Mama Makinda anaweza kukosolewa na mtu wa haiba yake au zaidi ikaleta maana.
Aliyeleta mada hii tunaomba CV yake tafadhali vinginevyo hakuna sababu ya kuchangia.
 

Wewe titi una akili mbovu sana. Kwani kujiita titi?
 
Kuhusu CV yangu soma ibara ya 18(1) ya katiba ya Tanzania ndiyo ujue mimi ni nani.

 

mzee hajakosolewa yeye binafsi na makinda,makinda anasema na wanahabari.
mimi nasema na mleta mada kumkosoa ane makinda.
 
Wewe sio mdogo wetu Bali mkubwa wetu.!! Hongera sana mkuu .viongozi wengi wana jibu hoja kulinda matumbo yao haijalishi wanajua ukweli. I salute you man!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…