Tafadhali Jaji Warioba,usituchagulie jina

Tafadhali Jaji Warioba,usituchagulie jina

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Kama Tume yako imeandaa Rasimu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye kujumuisha zilizokuwa nchi huru,tena Jamhuri, za Tanganyika na Zanzibar,iweje sisi tuitwe Tanzania Bara na wenzetu wabakie kuwa Zanzibar? Sisi watanganyika tutaandika Katiba yetu. Katiba itakuwa na jina la nchi yetu. Tunaweza kujiita tutakavyo. Wengi wetu twapenda tuitwe tena Tanganyika. Na tutaandika Katiba ya Tanganyika wala si ya Tanzania Bara.Subirini tuanze mchakato. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
hlo nalo nenoooooo. kwa mana tanzania ni muunganiko wa
tanganyika na zanzibar
...kwa mana hyo watanganyika tunashiriki uzanzibar bla kujua.
wakati wazanzibar wana jina lao
.........aaaaaaaaaaaa wapi hapo nimekuelewa vizuri sana.
AHSNTE KWA KUNIAMSHA ETI HATA HILO SIKULISHTUKIA DUUU MI NAE?
 
Tanganyika na Zanzibar = Tanzania

Tanzania bara ?
 
  • Thanks
Reactions: lum
Nakuunga mkono kwa asilimia zote mkuu kwanini tupoteze utanganyika wetu bila sababu?hili halikubaliki hata kidogo na hii yote nashindwa kuelewa maana yake ni nini.tanganyika ibaki tanganyika zanzibar ibaki kuwa zanzibar.
 
Kama Tume yako imeandaa Rasimu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wenye kujumuisha zilizokuwa nchi huru,tena Jamhuri, za Tanganyika na Zanzibar,iweje sisi tuitwe Tanzania Bara na wenzetu wabakie kuwa Zanzibar? Sisi watanganyika tutaandika Katiba yetu. Katiba itakuwa na jina la nchi yetu. Tunaweza kujiita tutakavyo. Wengi wetu twapenda tuitwe tena Tanganyika. Na tutaandika Katiba ya Tanganyika wala si ya Tanzania Bara.Subirini tuanze mchakato. Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


Mzee Tupatupa mbona na wewe unatuchagulia jina la Tanganyika? Yawezekana katika mchakato wa katiba za nchi mbili zenye Muungano tukapata jina la upande huu huku na upande ule wenye visiwa. Ila Tanganyika laweza kuwa jina tamu eeeeeeh? duh kumbe nami nachagua jina. loh!
 
Hivi wakuu hii rasimu mmeisoma yote au mmekimbilia huku mitandaoni na kuanza kupiga kelele za bure? Kama mmesoma msingeweza kuandika hiki mlichokiandika. Rasimu imetamka wazi wazi uwepo wa Tanganyika na Zanzibar kuanzia ukurasa wa 76. In fact, ukarasa huo ni SURA YA NANE inayohusu VYOMBO VYA DOLA VYA TANGANYIKA NA ZANZIBAR. Sehemu ya kwanza inahusu serikali ya Tanganyika na Zanzibar, sehemu ya pili mabaraza ya Wawakilishi ya Tanganyika na Zanzibar (page 77), sehemu ya tatu mahakama kuu za Tanganyika na Zanzibar (page 78). Sasa huu upotoshaji sijui nyie wenzangu mmeutoa kwenye rasimu ipi?
Wewe Mkuu ndiye unayepotosha.Ima kwa kutoelewa kilichoandikwa au kwa makusudi.Tanganyika imetajwa kwenye Utangulizi tu. Haikutajwa kwenye Ibara yoyote ya Rasimu. Nakuonjesha Ibara Ndogo ya 2 ya Ibara ya 146 ya Rasimu kuhusu Mahakama Kuu.Inasema hivi:(2)Mahakama Kuu ya Tanzania Bara na Mahakama Kuu ya
Zanzibar zitakuwa na mamlaka sawa ya kusikiliza katika ngazi ya awali,
mashauri ya madai na jinai kuhusu Mambo ya Muungano katika maeneo
ya utawala ya Washirika wa Muungano.
 
Jamani iliyotolewa ni rasimu, tujitahidi kutumia mfumo uliopo kuingiza yale tunayoona hayako tunavyotaka. Tume ingeleta rasimu ikiwa na Tanganyika, bado wasiopenda Tanganyika wangekoroma vilevile.
 
Hii ni rasimu tu wadau, bado tuna nafasi ya kufanya mabadiliko mpaka kufikia siku ya kuipigia kura mwakani panapo majaaliwa.
 
Wewe Mkuu ndiye unayepotosha.Ima kwa kutoelewa kilichoandikwa au kwa makusudi.Tanganyika imetajwa kwenye Utangulizi tu. Haikutajwa kwenye Ibara yoyote ya Rasimu. Nakuonjesha Ibara Ndogo ya 2 ya Ibara ya 146 ya Rasimu kuhusu Mahakama Kuu.Inasema hivi:(2)Mahakama Kuu ya Tanzania Bara na Mahakama Kuu ya
Zanzibar zitakuwa na mamlaka sawa ya kusikiliza katika ngazi ya awali,
mashauri ya madai na jinai kuhusu Mambo ya Muungano katika maeneo
ya utawala ya Washirika wa Muungano.
Mkuu sorry, nilikuwa na draft tofauti. Kuna draft mbili ambazo zina tofauti kubwa, wengi tunaweza ingia kwenye njia panda hii
 
Jina la upande wa pili wa Muungano na ZANZIBAR ni JAMHURI YA TANGANYIKA. Anayemeza na asiyetaka, hivyo ndivyo inavyotakiwa kuwa. Hakuna nchi inayoitwa Tanzania bara iliwahi kuungana na Jamhuri wa Watu wa Zanzibar (Serikari ya Mapinduzi ya Zanzibar). Swali jingine ni kuwa vilivyoungana ni nchi au serikali?
 

Attachments

Hivi mipaka ya bahari ya Tanganyika na Zanzibar ni ipi?
 
Back
Top Bottom