Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 876
Habarini ndugu zangu,
Jukwaa hili ni mara yangu ya kwanza kuposti uzi huu. Sijawahi kuandika zaidi ya kusoma tu yanayoandikwa. Leo nimeona nije hapa niweke wazi huu ugonjwa unaonisumbua kwa mwezi mmoja sasa.
Napata maumivu makali sana kwenye mkono wangu wa kushoto kuanzia kifundo cha katikati ya mkono hadi begani na sehemu kidogo ya bega langu.
Maumivu haya yanaleta mchanganyiko huu, mara nasikia baridi sana sehemu hiyo yote. Mara wakati mwingine nasikia ubaridi kiasi kwamba napata maumivu makali mno yakushindwa kulala na wakati mwingine kukaa.
Sijajua ni ugonjwa gani huu. Sijawahi kujigonga wala kuanguka. Wala siendeshi pikipiki. Awali nilifikiri huenda nimelala vibaya na hivyo kuulalia mkono wangu.Lakini kumbe hata mchana tu utakuta maumivu yanaanza.
Nimejaribu kuchua ua kupaka dawa aina ya diclofenac fluid lakini hakuna unafuu. Sasa naomba kama kuna mtu mwingine pia amewahi kukutana na maumivu kama haya anisaidie.Lakini pia madaktari mliopo hapa nisaidieni.
Kama nimeeleweka kwenye maelezo yangu nashukuru sana ndugu zanguni.
Jukwaa hili ni mara yangu ya kwanza kuposti uzi huu. Sijawahi kuandika zaidi ya kusoma tu yanayoandikwa. Leo nimeona nije hapa niweke wazi huu ugonjwa unaonisumbua kwa mwezi mmoja sasa.
Napata maumivu makali sana kwenye mkono wangu wa kushoto kuanzia kifundo cha katikati ya mkono hadi begani na sehemu kidogo ya bega langu.
Maumivu haya yanaleta mchanganyiko huu, mara nasikia baridi sana sehemu hiyo yote. Mara wakati mwingine nasikia ubaridi kiasi kwamba napata maumivu makali mno yakushindwa kulala na wakati mwingine kukaa.
Sijajua ni ugonjwa gani huu. Sijawahi kujigonga wala kuanguka. Wala siendeshi pikipiki. Awali nilifikiri huenda nimelala vibaya na hivyo kuulalia mkono wangu.Lakini kumbe hata mchana tu utakuta maumivu yanaanza.
Nimejaribu kuchua ua kupaka dawa aina ya diclofenac fluid lakini hakuna unafuu. Sasa naomba kama kuna mtu mwingine pia amewahi kukutana na maumivu kama haya anisaidie.Lakini pia madaktari mliopo hapa nisaidieni.
Kama nimeeleweka kwenye maelezo yangu nashukuru sana ndugu zanguni.