MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 14,588
- 32,361
Tafadhali Shilole usinunue Rolls Royce Cullinan 2021
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi. Natumaini wote mko poa mkiendelea vyema kulipia tozo za miamala. Hakika uzalendo hauepukiki. Leo nitaongelea jambo ambalo sikupenda kabisa kutia neno kwa sababu uzito wake ni mdogo sana kitaifa... ila kwasababu wengi wenu mmeniomba sana niseme kitu acha nitiririke japo kidogo.
Suala lenyewe ni kuhusu komredi Simba kununua gari la kifahari Rolls Royce Cullinan 2021 kwa gharama ya takribani Tsh 1.9b. Hizi pesa ni nyingi sana kiasi cha kuweza kujenga ofisi za CHADEMA zaidi ya 10. Baadhi ya watu wanadai zingeweza kununua wabunge kadhaa wa CHADEMA na kuhamia chama pendwa. Hawa nimewapinga kwa sababu chama pendwa hakinunui wapinzani. Huwa wanahamia wenyewe.
Alichofanya kada wa CCM, Mr Simba ni kawaida kwa wanamuziki wakubwa. Ni mbinu nzuri kibiashara. Kazi ya sanaa inahitaji mambo mengi ya kujimwambafy ili kuongeza thamani ya msanii. Kwa mfano msanii 20 percent ana kipaji cha hali ya juu na nyimbo zisizochuja lakini thamani yake ni ndogo kulinganisha na msanii mdogo kama Ali Kiba. Hii ni kwasababu 20 percent hana ujanja ujanja kama Simba au hata wasanii wengine wadogo kama Ali Kiba, Bill Nas na wengine. Mara baada ya ujio wa Rolls Royce tutegemee thamani ya Simba kupanda mno.
Baada ya kuona wasanii wanapenda kuigana nimeona nije hapa JF kumuomba msanii mkubwa kwa sasa nchini kwetu ambaye pia ni kada wa CCM asifanye kama alivyofanya Simba ingawa uwezo huo anao. Huyu si mwingine bali mwanamama Shilole a.ka SHISHI BABY. Kwa kifupi ni kwamba Shishibaby ndo msanii mkubwa kwa sasa upande wa wanawake.... katoa hits nyingi sana kwenye muziki wa bongo flava ambazo zimeacha alama zisizofutika. Show zake huwa zinauza tiketi na kuisha mapema... mauzo ya kazi zake mitandaoni ni jambo lingine linalomweka level moja na Simba.
Tunaambiwa hadi sasa hivi hakuna msanii aliyeweza vunja rekodi aliyoiweka nchini Ubelgiji kwa show kali iliyowainua wazungu vitini na kuanza kucheza. Link hiyo hapo kajionee
Hadi muda huu SHISHIBABY ndo msanii ambaye kiuchumi yuko vizuri na anaweza kununua Rolls Royce akitaka. Pamoja na kufanya vizuri upande wa muziki tukumbuke miaka ya hivi karibuni kumetokea utambulisho mwingine wa Shilole unaokua kwa kasi... SHISHIFOOD. Hii ni biashara inayoendelea kumtambulisha kwa kasi komredi Shishi.
Mimi namsihi Shilole asifikirie kununua Rolls Royce wakati huu bali hiyo 1.9b atuongezee migahawa mingi zaidi ili kutoa ajira na yeye kujiongezea kipato. Bado tunahitaji huduma ya Shishifood kwenye miji mikubwa kama Guangzhou, Yiwu, Dubai, Johannesburg, Nairobi, Lagos, London, Addis Ababa na miji mingine inayotembelewa na waafrika wengi. Shishi asijisikie vibaya kutembelea gari la 200m wakati huu anapojifunga mkanda kuipanua Shishifood.
Watanzania wote tumuombee huyu binti.
Nawasalimu kwa jina la Chama Cha Mapinduzi. Natumaini wote mko poa mkiendelea vyema kulipia tozo za miamala. Hakika uzalendo hauepukiki. Leo nitaongelea jambo ambalo sikupenda kabisa kutia neno kwa sababu uzito wake ni mdogo sana kitaifa... ila kwasababu wengi wenu mmeniomba sana niseme kitu acha nitiririke japo kidogo.
Suala lenyewe ni kuhusu komredi Simba kununua gari la kifahari Rolls Royce Cullinan 2021 kwa gharama ya takribani Tsh 1.9b. Hizi pesa ni nyingi sana kiasi cha kuweza kujenga ofisi za CHADEMA zaidi ya 10. Baadhi ya watu wanadai zingeweza kununua wabunge kadhaa wa CHADEMA na kuhamia chama pendwa. Hawa nimewapinga kwa sababu chama pendwa hakinunui wapinzani. Huwa wanahamia wenyewe.
Alichofanya kada wa CCM, Mr Simba ni kawaida kwa wanamuziki wakubwa. Ni mbinu nzuri kibiashara. Kazi ya sanaa inahitaji mambo mengi ya kujimwambafy ili kuongeza thamani ya msanii. Kwa mfano msanii 20 percent ana kipaji cha hali ya juu na nyimbo zisizochuja lakini thamani yake ni ndogo kulinganisha na msanii mdogo kama Ali Kiba. Hii ni kwasababu 20 percent hana ujanja ujanja kama Simba au hata wasanii wengine wadogo kama Ali Kiba, Bill Nas na wengine. Mara baada ya ujio wa Rolls Royce tutegemee thamani ya Simba kupanda mno.
Baada ya kuona wasanii wanapenda kuigana nimeona nije hapa JF kumuomba msanii mkubwa kwa sasa nchini kwetu ambaye pia ni kada wa CCM asifanye kama alivyofanya Simba ingawa uwezo huo anao. Huyu si mwingine bali mwanamama Shilole a.ka SHISHI BABY. Kwa kifupi ni kwamba Shishibaby ndo msanii mkubwa kwa sasa upande wa wanawake.... katoa hits nyingi sana kwenye muziki wa bongo flava ambazo zimeacha alama zisizofutika. Show zake huwa zinauza tiketi na kuisha mapema... mauzo ya kazi zake mitandaoni ni jambo lingine linalomweka level moja na Simba.
Tunaambiwa hadi sasa hivi hakuna msanii aliyeweza vunja rekodi aliyoiweka nchini Ubelgiji kwa show kali iliyowainua wazungu vitini na kuanza kucheza. Link hiyo hapo kajionee
Hadi muda huu SHISHIBABY ndo msanii ambaye kiuchumi yuko vizuri na anaweza kununua Rolls Royce akitaka. Pamoja na kufanya vizuri upande wa muziki tukumbuke miaka ya hivi karibuni kumetokea utambulisho mwingine wa Shilole unaokua kwa kasi... SHISHIFOOD. Hii ni biashara inayoendelea kumtambulisha kwa kasi komredi Shishi.
Mimi namsihi Shilole asifikirie kununua Rolls Royce wakati huu bali hiyo 1.9b atuongezee migahawa mingi zaidi ili kutoa ajira na yeye kujiongezea kipato. Bado tunahitaji huduma ya Shishifood kwenye miji mikubwa kama Guangzhou, Yiwu, Dubai, Johannesburg, Nairobi, Lagos, London, Addis Ababa na miji mingine inayotembelewa na waafrika wengi. Shishi asijisikie vibaya kutembelea gari la 200m wakati huu anapojifunga mkanda kuipanua Shishifood.
Watanzania wote tumuombee huyu binti.