Tafadhali tukutane tunywe kidogo ili tulitatue hili swala

bioto

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2017
Posts
1,261
Reaction score
2,097
Kuna watu tuna matatizo ya kunywa pombe kwanza kila unapotaka kufanya jambo fulani;

> Tukiwa na furaha tunakunywa pombe kwa ajili ya kusherekea
> Tukiwa na huzuni tunakunywa ili tufurahi

> Tukiwa na mawazo tunakunywa pombe ili tusahau

> Tukiwa na hasira tunakunywa ili hasira zipungue

> Tukiwa na aibu tunakunywa ili tuwe majasiri

Yaani ukitaka kufanya kitu lazima unywe pombe ndio ufanye. Jamani wenzangu wenye hili tatizo tukutane sehemu tunywe kidogo ili tulijadili na kutatua hili swala
 
Mwezi wa nne na nusu huu sijagusa hata white wine.

Na nyumbani kuna Heineken na Corona zimejaa katika friji, kabatini kuna mizinga ya Dwar's, Tequila, Vodka na Scotch Whiskies nyingine ambazo nimekuwa na nguvu kuzichunia tu.

Kwa sababu niliamuatu kuacha. Na mpaka sasanimesimamia uamuzi huo.

Mgeni anayehusikana mambo hayo akija atakarimiwa tu.
 
Kwa wakubwa tu watoto hawaruhusiwi hiyo pombe haitoliacha taifa salama maaana ingependeza kama tungeizimbabwe vileeee
 
Kwa hiyo ndo umetuacha kiaina
Hongera lakini
 
Kwa wakubwa tu watoto hawaruhusiwi hiyo pombe haitoliacha taifa salama maaana ingependeza kama tungeizimbabwe vileeee
mapato ya serikali yatashuka kwa hiyo haiwezekani kabisa
 
Naunga mkono hoja pia mabosi wetu TBL wanasema mauzo yameporomoka

Tunazembea kungwa au vizibo vimekaza mpaka opena zinavunjika
 
anzisha nyumba ya ibada mkuu
 
Niliacha week mbili tu yani shetani alinirudisha kwa hasira mpaka basi, ila sasa nimeacha tena, pombe ni chanzo cha maovu mengi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…