Tafakuri jadidi: Je, Urusi ametengwa na washirika wake? Ikiwa NATO ataingia Ukraine kupambana, Urusi ataweza kupambana peke yake?

kt the irreplaceable

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2017
Posts
2,375
Reaction score
4,893
Ndugu zangu ikiwa bado kuna mgogoro ukiendelea kufukuta nchini Ukraine, tumeshuhudia vikwazo na matamko mazito kutoka kwa NATO members na European union kwa Urusi. Ikiwa nato ataamua kwenda field physically kupambana na majeshi ya urusi, je Urusi ataweza kupambana mwenyewe?

Ikumbukwe Nato ni muunganiko wa nchi zaidi ya 30, je Urusi atakua na power ya kupambana nao?

Je, mataifa rafiki kama China, North Korea, Cuba, Iran nk wamemuacha solemba Russia? Je wataweza kutuma vikosi vya kijeshi kwenda kumsaidia mwenzao?

Ni nini hatma ya dounia ikiwa Urusi ataanguka kiuchumi na kua weak sana kijeshi? Je, Syria, Venezuela na belarusi serikali zao zitabaki salama?

Je, China anamchora mrusi? Ikiwa mrusi ataanguka, je China atafanikiwa kwenye ndoto zake za kua super power?

Tunapojadili hii mada, wale 'vichwa panzi' waliojaa ushabiki na mahaba, naomba muishie hapa. Tunataka 'critical thinking' juu ya maswali haya. Karibuni tujadili.
 
Kama kuna kitu USA na hata mataifa members wa NATO hasa yale yalio endelea kama UK, France, Spain nk huaga yanaogopa sana kutupiwa kitu kizito nyumbani kwao, yaani bomu kushuka Newyork, London, Madrid, Paris; sasa zile nyambizi ambazo Russia kaziongeza kule Cuba na Venezuela vinatishia kupigwa miji ya Marekani; kwa mtazamo hu naweza kusema (mtazamo wangu) USA na NATO yake watapigana vita vya maneno, kiuchumi (vikwazo being one of them ) na propaganda kama zinazoendelea kwamba Urusi anaua watu as if kule Iraq, Afghanistan, Libya Marekani hakuua watu. Ndicho watakacho kifanya and may be kuendelea kuuza silaha kwa Ukraine but wao kwenda front, nina mashaka sana. Well, baada ya vita hi, nina hakika yale mambo ya vita baridi yaliokuwepo kwa miongo kadhaa yatarudi tena, sema dunia imestaarabika zaidi kulinganisha na zamani cause zamani ukiwekewa vikwazo na USA the hutoboi, not now cause kuna mmbadala wa kufanya biashara na wengine.
 
Tsar moja inatosha London kuwa majivu
 
Enzi ya utwala wa Kennedy 1960s USSR by then walipeleka mitambo ya nyukilia pale Cuba, hali ilikua mbaya sana mpaka kupelekea makubaliano ya kimkataba yaliojulikana kama "camp David peace accords". Je kwa mgogoro huu tutegemee makubaliano mengine ya hawa wakubwa?
 
It sound it so bro, kwa wasio jua, Putin kaamua kuipiga Ukrein kwasababu ya kuvunjwa kwa makubaliano walioyafanya mwanzoni mwa miaka ya 90 kati ya Urusi na hiyo hiyo NATO, kwamba NATO asisogee kwa mataifa yaliokua Ulaya ya mashariki, hi ni pamoja na yale yaliokua yakifata siasa za Kikominist; NATIO hasa kupitia USA akavunja mkataba huo, kawasajiri Poland, Romania, Yogoslavia zote 2 ( zamani Yugoslavia ilikua nchi moja ) jamuhuri ya Chekclovakia etc, alishawishi aliyekua rais wa Ukrain kupinduliwa na akaingia huyu ambaye ana mitazamo ya Kimagharibi na alianza kumshawishi jamaa a join NATO; kwa mazingira hayo Urusi angefanyaje?? Tusubiri na tuone, lolote linaweza kutokea hasa hiyo statement yako ya mwisho, cause hiyo hasa ndio kiini cha mgogoro hu
 
Kwenye kikao cha dharula kilichofanyika jana mjini New York, mjumbe kutoka Russia alitoa sababu ya kuivamia Ukraine. Ukisikiliza sababu zile utagundua Russia wanaonewa, hivyo anaamua kutumia hasira kujilinda.
 
Vita possibility yake kutokea ni ndogo kaka.
Na hata ikitokea China hawezi kushiriki Vita ambayo haitamnufaisha badala yake ataombea iendelee ili ndoto zake za kushika hatamu kiuchumi zitimie.
Pia kumbuka hao washirika was Russia nao wana yao yanaowabana kutoka kwa USA hvyo sidhani km watataka hatari zaidi.
 
Ndiyo ataweza, ila hataacha peke yake, ana marafiki pia...
 
Hakuna Unato wowote unaoweza weka Roho zao Rehani,Maisha Matamu wee.
 
Nani aliekudanganya kuwa mchina hatoingia kwenye vita isiyo mhusu,kumbuka mchina hawezi kuwa salama kama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…