Tafakuri ya kimaisha

Tafakuri ya kimaisha

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Nazungumza na wale wenye miaka 35+

Jaribu leo utoke peke yako, na uende kwenye mazingira tulivu, kama yanaruhusu kupata kinywaji au kula matunda yoyote fanya hivyo.

Jitafakari ulipotoka, mpaka hapo ulipo sasa.

  • Jiulize haya maswali; leo hii nikifungwa gerezani ni nani atakuwa karibu na mimi au na familia yangu? Jaribu ku 'screen' kuanzia ndugu zako, mwenzi wako, watoto wako, marafiki zako n.k
  • Hivyo hivyo, jiulize tena; leo hii nikiwa kitandani najiuguza kwa muda mrefu labda miaka miwili nikiwa siwezi kuinuka wala kujisaidia, ni nani atakuwa karibu na mimi? Jaribu tena ku 'screen' kuanzia ndugu zako, mwenzi wako, watoto wako, marafiki zako n.k
  • Hivyo hivyo, jiulize tena; leo hii nikiondokewa/kufiwa na mtu muhimu sana kwangu/nguzo yangu, ni nani atakuwa karibu na mimi? Jaribu tena ku 'screen' kuanzia ndugu zako, mwenzi wako, watoto wako, marafiki zako n.k
Baada ya kupata majibu, matumizi yako ya pesa ya sasa wekeza au tumia na huyo atakayekuwa na wewe katika hayo mazingira yenye changamoto; kwa sababu unayeokota naye kuni kwa sasa ndiye mtakaye ota naye moto wakati wa baridi.

NB. Hakuna mtu atakayeuza nyumba yake ili kutatua changamoto zako.
 
We Mswati wa JF unafanya uliyoyaandika?? We si kila siku uko na vyombo vipya unahonga na akati una mke na watoto kibao kwenye sehemu ulizowekeza??
Nami nauliza swali, unapoenda kusali huwa unasikiliza neno la bwana au unaangalia tabia za muwasilishaji wa neno? Ukijibu vizuri, nakununulia sasa hivi balimi 😀 😀
 
Nami nauliza swali, unapoenda kusali huwa unasikiliza neno la bwana au unaangalia tabia za muwasilishaji wa neno? Ukijibu vizuri, nakununulia sasa hivi balimi 😀 😀
Lakini kama tabia za muwasilishaji neno ni za hovyo, hata injili atakayohubiri haitakuwa na impact yoyote ndani yangu maana neno ili liwe hai na liumbike lazima Roho Mtakatifu aliumbe ndani yangu sasa kama muwasilishaji nakutana nae kidimbwi na najua ishu zake atakuwa kama ananipigia ngoma tu..situmiagi balimi kaka mswati..🤸
 
Lakini kama tabia za muwasilishaji neno ni za hovyo, hata injili atakayohubiri haitakuwa na impact yoyote ndani yangu maana neno ili liwe hai na liumbike lazima Roho Mtakatifu aliumbe ndani yangu sasa kama muwasilishaji nakutana nae kidimbwi na najua ishu zake atakuwa kama ananipigia ngoma tu..situmiagi balimi kaka mswati..🤸
Kama ni hivyo, mambo mengi yatakuwa ni batili, ila tunavumilia tu; utasikilizaje neno kwa mtu aliyepiga madogi staili usiku 😀 😀
 
Nami nauliza swali, unapoenda kusali huwa unasikiliza neno la bwana au unaangalia tabia za muwasilishaji wa neno? Ukijibu vizuri, nakununulia sasa hivi balimi 😀 😀
Askofu gwajima akija kukuhubiria usizini utamwelewa kweli mkuu?
 
Ni wangapi katika dunia hii hawafanyi tendo?
Wengi wanafanya tendo. Lkn mchungaji mzinzi akwambie acha uzinzi kikawaida utampuuza.
Labda kama atatubu mbele ya hadhara na kuelezea madhara ya uzinzi.

Ndio maana baba akiwa mlevi atashindwa kukemea ulevi kwa watoto. Watoto watamcheka na wanaweza wakawa walevi zaidi yake
 
Wengi wanafanya tendo. Lkn mchungaji mzinzi akwambie acha uzinzi kikawaida utampuuza.
Labda kama atatubu mbele ya hadhara na kuelezea madhara ya uzinzi.

Ndio maana baba akiwa mlevi atashindwa kukemea ulevi kwa watoto. Watoto watamcheka na wanaweza wakawa walevi zaidi yake
Akikuambia uache uzinzi, ni kwa faida yake au faida yako?
 
Back
Top Bottom