Tafsiri ya Sizonje - Wimbo wa Mrisho Mpoto

SNAP J

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2013
Posts
7,106
Reaction score
8,043
SIZONJE ndio jina la wimbo wake mpya Mrisho Mpoto alieyeshirikiana na Banana Zoro. Nimeusikiliza kwa makini lakini bado sijajua maana halisi ya huu wimbo.

Huwa napenda sana nyimbo zake Mpoto, kwani zinakuwa na ujumbe mzito ndani yake ambao huufanya ubongo ufikiri, achilia mbali mtindo au staili yake anayoitumia kuwaburudisha hadhira yake..

MASHAIRI (SIZONJE)
=========

Mrisho Mpoto akiuzungumzia wimbo wake wa 'Sizonje'

Rais Magufuli akiufurahia wimbo wa Sizonje

SIZONJE wafika Ikulu
---------------

Baadhi ya maoni kutoka kwa WanaJamiiForums wakijaribu kuufafanua;


 
Km wimbo unakuwa mgumu kueleweka basi hamna kitu sanaa lazima ifikie hadhira tena kwa wepesi km kamtungia mzee sigara wa kiswahili hapo sawa ila km ni kwa wote kachemka
 
Kuna sehemu kazungumzia tatizo la ajira.nimeusikiliza leo mara moja nadhani nikiusikiliza tena nitang'amua mengi.
 
Mkuu tupia humu huo wimbo maana bado sijausikia maana ni msanii ninayemkubali sana hapa bongo.
Asante..
 
tafsida na Kiswahili fasihi zaidi kimetumika, inakupasa uwe mjuvi wa lugha.....
 
Jamaa yupo vizuri ila zaidi anaongelea udhaifu was serikali yetu...
Kushindwa kuwahudumia wananchi wake na kuanzisha taasisi za elimu pasipo kuwa na uzalishaji wa ajira.

Aidha watu wanapeana ajira pasipo kufuata taratibu zinazotakiwa...ndo maana anasema watu wanapita dirishani badala ya mlangoni.
 
Kwa kifupi Sizonje ni Mjomba wa sasa.. Sizonje ni Magufuli, amekaribishwa kwenye nyumba mpya.

Nyumba ina vyumba vinne, kaonyeshwa vyumba viwili na uwani, anamaanisha Magufuli kaingia Ikulu; chumba cha kwanza chumba cha mahakama, na uwani ni bungeni.

Watu hawafuati sheria, wanafanya pasipo kufuata utaratibu, wanapitia dirishani.

Choo kipo na shimo la taka lipo lakini watu hawatumii kabisa. Nchi ina kila kitu lakini hatufaidiki na vilivyomo yaani havina faida.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…