Tafukuri: Itakuwaje Maalim Seif akitangazwa rais wa Zanzibar?

Tafukuri: Itakuwaje Maalim Seif akitangazwa rais wa Zanzibar?

bucho

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2010
Posts
5,149
Reaction score
3,209
Nimejaribu kuwaza mimi na serikali ya kichwa changu kuwa itakuwa vipi kama Maalim Seif akitangazwa mshindi akaamua kuvunja muungano.

Je, Magufuli ataendelea kuwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania? Ama tutarudi kwenye uchaguzi upya? Nawaza tu hapa katika ulofa wangu. The game is not over yet ndio kwanza napuliza kuni zangu popcorn ziiive.
 
Kuvunja muungano ni long process serikali 2 zikae, zijadili mpk wafikie muafaka huo sidhani kama itakiwa simple simple
 
Kwenye swala la muungano najua wazanzibari wako pamoja mnoooo... Tena walivyochoka kuendeshwa na wabara kazi IPO tena sio kidogo
 
Kwani tuna katiba ya Tanganyika mku? Sijui itakuaje ila wenzetu wa Zanzibar wanakatiba yao muungano uwepo au usiwepo.
Maalim mara nyingi hua anadai Mamlaka kamili ndani ya serikali 3, swali ni Je, upande wa bara wapo tayari kwa hilo?
 
Maalim seif hawezi kuvunja muungano na hana nia ya kufanya hivo..na mara nyingi tu amekua akilisisitiza hilo ila anachotaka yeye ni kuwa na muungano wa usawa na wa kuheshimiana ktk maamlaka ,muungano ambao kila mtu atakua na uwezo wake kimaamuzi na kuendesha nchi yake sio huu wa kibabe.. CCM wanaogopa kwakua wanajua zanzibar ikitawaliwa na maalim seif basi ccm ndio imekufa visiwani na baadae bara itafuatia
 
Rais wa Zanzibar ni mjumbe wa Baraza la Mawaziri la JMT.hapo patakuwa patamu
 
Maalim seif hawezi kuvunja muungano na hana nia ya kufanya hivo..na mara nyingi tu amekua akilisisitiza hilo ila anachotaka yeye ni kuwa na muungano wa usawa na wa kuheshimiana ktk maamlaka ,muungano ambao kila mtu atakua na uwezo wake kimaamuzi na kuendesha nchi yake sio huu wa kibabe.. CCM wanaogopa kwakua wanajua zanzibar ikitawaliwa na maalim seif basi ccm ndio imekufa visiwani na baadae bara itafuatia


Trust me ....never say never...ataweza kuuvunja alafu baadae akaja kujiunga kwenye serikali tatu . chochote kinawezekana boss
 
Kuvunja muungano ni long process serikali 2 zikae, zijadili mpk wafikie muafaka huo sidhani kama itakiwa simple simple

Simple tu, wazanzibar wanaweza kupiga kura ya maoni tu,kuamua tunautaka au hatutaki. Simple
 
Simple tu, wazanzibar wanaweza kupiga kura ya maoni tu,kuamua tunautaka au hatutaki. Simple


Yes ndio nilichokuwa namaanisha haswaaaa....
 
Ibara number 41 ya katiba ya JMT inazungumzia uchaguzi wa raisi. Ninaomba wanasheria mtusaidie kupata ufafanuzi kifungu cha saba.

(6) Mgombea yeyote wa kiti cha Rais atatangazwa kuwaamechaguliwa kuwa Rais iwapo tu amepata kura nyingi zaidikuliko mgombea mwingine yeyote.

(7) Iwapo mgombea ametangazwa na Tume ya Uchaguzikwamba amechaguliwa kuwa Rais kwa mujibu wa ibara hii, basihakuna Mahakama yoyote itakayokuwa na mamlaka yakuchunguza kuchaguliwa kwake.

Ufafanuzi ninaoumba ni kama tangazo la tume juu ya raisi litakuwa na kinga ya kutokuchunguzwa na mahakama yoyote hata pale ambapo maamuzi ya tangazo hilo hayajazingatia matakwa ya Ibara hii ya 41 mfano kama kifungu cha 6 ama chochote kikiwa kimekiukwa.

Kifungu cha saba kinasema wazi "Iwapo mgombea ametangazwa na tume ya uchaguzi kwamba amechaguliwa kuwa raisi kwa mujibu wa ibara hii (ya 41)". Vipi kama kilichotangazwa hakiko kwa mujibu wa ibara hii? Bado tangazo hilo ni legally binding?

Swali lingine, ni chombo gani kinatakiwa kuhakiki compliace ya tume ( iliyopewa nguvu hiyo kwenye) ili kujiridhisha kwamba inachokitangaza kimefanyika inline with stipulations za ibara hii ya 41?

Vipi ikitokea msemaji wa tume, on insanity, corruption, Rebellion, conspiracy, au threat grounds akamtangaza mtu kuwa raisi bila taratibu na mahitaji ya ibara hii ya 41 kufuatwa, bado itakuwa ni lawful, binding and enforceable announcement?

NAOMBA TUJADILIANE NA KUELEIMISHANA KWA HOJA. Na ni vizuri tukiwa tunarejea mfano wa kifungu cha sita hapo juu..
 
Mkuu ngoja wataalam wa sheria wapite hapa labda wataweza kutusaidia kwa faida ya wote
 
Back
Top Bottom