Tahadhari kwa wanawake walioolewa

Mtambuzi

Platinum Member
Joined
Oct 29, 2008
Posts
8,809
Reaction score
15,421
Je, mlishawahi kujiuliza ni kwanini ma-house girl huwavutia waume zenu kuliko nyie wake zao?

Nyie wanawake ndio wa kujilaumu kwasababu tatizo liko kwenu na sio kwao wala kwa waume zenu…

Najua hapo pua zimewasimama kwa kutaka kubisha… Lakini leo Mtambuzi mtanitambua maana nataka niwafunde……

Ni hivi:

House girl hufanya kazi nyingi kuliko muolewaji……….. najua mtadai kuwa huo ni wajibu wao kwa sababu ya kijimshahara cha elfu thelathini mnachowalipa……lol…….. amkeni nyie acheni ujinga wajibikeni ili mlinde ndoa zenu. Mwanaume hutazama nani anawajibika ndani ya nyumba kuliko mwingine………. Yaani hata chai ya jioni ya mumeo atayarishe house girl? Mwanaume hupenda mtu anaye m-handle na kum-care kwa kila jambo, na hata kama wewe hufanyi, basi fuatilia kuhakikisha linafanyika kwa usahihi.

Hebu angalia ujinga mwingine mnaofanya…….. mnawazuia ma-house girl wenu wasiende kwa mabwana zao kumaliza ashiki zao za kimwili…….. wapeni nafasi nao wafurahishe miili na akili zao! Wasipochangamsha miili yao na mabwana zao ni rahisi kujirahisisha kwa waume zenu na waume zenu wakionja tu hawataacha maana hupata ladha ambayo nyie hamna…..lol …………….. na mkiwakatia tiketi kuwarudisha makwao waume zenu watawapa nauli ya kurudia………. Kwani hamjui kwamba, muonja asali haonji mara moja? Na wakirudi hupangishiwa mahali pa kukaa na mchezo unaendelea.

Jamani hebu amkeni, mie nimechoka kusikia hizi kesi mnazolalamika kila uchao kuwa mnazidiwa kete na ma- house girl……………

Sikukuu njema
 
eid mubarak!
Nitarudi
,ngoja nimalizie kupitia homework ya mtoto.
Lakini suffice to say tusidharau ma hausgel,ni wanawake kama mwanamke mwingine yeyotee yule.
 
Sio bure mgonjwa huyu lazima atakuwa amepona. Hahahaaaaaaaaaaaaaa!

Kaka ni kama umepiga ikulu mzee. Nna jamaa yangu kaka ya mkewe kwa sasa anajimwaga na beki tatu alofukuzwa na mkewe lakini jamaa kwa kunogewa na penzi la beki tatu, akaamua kumrudisha mjini toka kwao ujitani hadi dar. Akampangia nyumba demu, mbaya zaidi akamfanya awe house girl wa mama yake mzazi.

Kwa sasa jamaa anajimegea tena kwa raha zake, maana wife wake hajui kuwa beki tatu amerudishwa mjini na amepangiwa chumba. Mshikaji wangu ananiambia kuwa beki tatu 'kazi' anaijua maana hata yeye aliamua aonje ajue nini hasa kilichomfanya shemeji yake afikie hata kumrudisha mjini kutoka ujitani.

Aisee sisi wanaume ni nomaaaaaaaaaaaaaaaaaaa! Unapewa kila kitu lakini, waaaaaaaaaaaapi, mweeeeeeee! Ndo maana Mungu kawajalia wanawake roho ya huruma, vinginevyo dunia hii wangekuwa wao peke yao tu.
 
Safi sana mtambuzi. Endelea kupona haraka ili tuzidi kufaidi hii mambo. Sasa binam yako anaendeleaje baada ya kuibiwa mme na beki tatu?
 
Ngoja waje wakujibu wenye waume wanaotamani ma housegirl; lol.
 
Ni vigumu sana wanawake kuukubali ukweli huu,lakini ndo hivyo,mwanaume yoyote ndivyo alivyo kiasili haijalishi ana tabia ipi muda huu!Nawashauri wanawake waufanyie kazi huu ushauri!
 
Tamaa tu 99%. Vipi kwa wale wenye mabinti zao wanaofanya kazi kama kawaida?? Wengine hata ulete mdogo wako akusaidie japo kufua vinepi vya mtoto, litang'ang'aniza tu kutembea nae hata kama hafanyi kazi zote! Mianaume ndivyo mlivyo {source: Bishanga}!!!
 
Kipipi chondechonde wanaume hatuko kama unavyofikiria!
 
Safi sana mtambuzi. Endelea kupona haraka ili tuzidi kufaidi hii mambo. Sasa binam yako anaendeleaje baada ya kuibiwa mme na beki tatu?

ndio nimeanza darsa la ushauri......... tumekubaliana awe anakuja kwangu kuchota maujanja, na mama ngina naye anasaidia kuokoa jahazi
 
Kipipi chondechonde wanaume hatuko kama unavyofikiria!

Kumbe mkoje?? Housegal ni mwanamke kama alivyo mwanamke mwingine. Sasa kama kinachowapeleka kwa hao wanawake wengine ni tamaa, why mlete justification kwa housegal?? Semeni tu kwamba housegal mnakuwa mmesogezewa karibu alafu hana gharama saana kama huko kwingine (though baada ya mchezo kunoga ndo mnaamua kugaramia)!!! Narudia tena, {mianaume ndivyo mlivyo}
 
Mara nyingi wanawake tunajisahau saana na kuona kana kwamba mumeo aweza vutiwa tu na mwanamke huko nje.... IMO house gal ni binti wa kumuogopa saana na kua nae makini ni kiasi gani awe karibu na mumeo.... Nimewahi zungumzia hili kwenye thread ya First Lady, the below ni copy and paste from that thread.



Source: Thread ya First Lady - LINK
 
Mtambuzi
I had a lot to say about your type of reasoning how stup** it sounds and so forth but nikaona..................anyways let me ask you this, Je In the same token, si wamama tunapowanyima watoto wetu, wa kike kwenda kutoa ashiki zao should u as baba mwenye nyumba take care of that as well?? Acheni excuses zenu za kipumbavu!!!!Men sleeping with the help has got nothing to do with the wife but your own tamaa!!!!
 
Ni kweli kabisa nyie wanaume hamna jema jamani......ndio maana mwanzo sikutaka kusema kitu maana najionea tabu tu. Hata mkeo akufanyie nini kama haujastaaribika ndio basi tena hata mdogo wa mkeo kutembea nae huoni shida licha ya HG!!!!!

Kwakweli kilichobaki ni kila mwanamke apige goti kumuombea mumewe maana mmmhhhh.....kama ni mtihani tunao.
 
Hizi ni bla bla tu; wa kutembea na house girl atatembea nae tu; wa kujiheshimu atajiheshimu tu.

Ila kwa wenye waume wa hivyo dawa yao ni kuajiri houseboy kama yeye who ever anayempa huduma za kumpikia na kumfulia lazima achape basi amcameroon. lol.


Hizo ni justification za kipuuzi; na utakuwa kichaa kama inafikia mpaka unaogopa kuwa na msaidizi ndani; ndio ile mijanamume unakuta mdada kila akileta ndugu anachapa, housegirl anachapa; wa hivyo hata ma binti zake atakuwa anachapa maana asione sketi imekatiza, chu.pi inabana.


 

kumbe ulishawahi kutoa darasa zuri namna hii hapo nyuma...............ushanirahsishia kazi ya kumshauri binamu yangu, haa ni ku-copy na ku-pesti tu, kazi kwisha..................
 

Dah Mtambuzi Baba karibu tena. Naona umepona Baba tunamshukuru MUNGU kwa hilo.

Hii mada yako ya leo ....................Dah!

Hapo kwenye red: Unataka kunambia mwanaume anaoa kwa kuwa anataka mtu wa kuwajibika? Kumpikia, kumfulia n'k? Kama ni hivyo am sorry naombeni niprolong likizo yangu tafadhalini!!

Mtambuzi eti tuwajibike kwa kufanya kazi kwa kuwa mwanaume anaangalia nani anayefanya kazi kuliko mwingine ndani ya nyumba????!! Oh Puleeeez Mtambuzi Give me a break eh!!
Hapo kwenye Blue hebu nifafanulie Mdada wa Kazi anam-care na kum-handle vipi Mbu wangu??
 
Tena mama Tuli chunguza wanawake wenye wanaume wanaotembea na mahosegirl afu njoo utuambie; wake zao hawana kasoro na ni wachapa kazi za ndani wazuri tu; Wanaume wengine hata uwabebe na mbeleko ya chuma.

Lol. Mi wala sisumbuhi akili yangu kuwaza hubby atatembea na h/girl tena ma h/girl wangu ukiwakuta hutajua kama ni ma h/girl ni wazuri na ni wadada wa pamba. Wanawake tujiamini; mwanaume malaya ni malaya tu; msinyanyase ma housegirl wenu kisa mmeo asimtamani. Kama mumeo ni kunguru kunguru tu hafugiki.

 
Si ndo hapo; kwa hiyo nkitoka job nianze kuwajibika mpaka saa tano usiku ili nishindane na hosegirl kuchapa kazi asije nizidi kete; kwa mtaji huo atembee nae tu mradi nisiwashike.

 
Si ndo hapo; kwa hiyo nkitoka job nianze kuwajibika mpaka saa tano usiku ili nishindane na hosegirl kuchapa kazi asije nizidi kete; kwa mtaji huo atembee nae tu mradi nisiwashike.

Da Mkubwa umeiona hii ya leo??!
Mimi hii naiona tu kama ni justification kama ile ya nyumba ndogo kusema kweli.
Wanaume wetu tunawapenda sana, sana tu! But mpaka uende mvulia kufuli lako na kumwonyesha tupu yako binti yangu (Msichana wangu wa kazi) ni dharau tu kwa mkeo na utovu wa nidhamu. ......................
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…