TAHADHARI: Upepo mkali kuipiga Dar kwa siku nne mfululizo kuanzia tarehe 20 hadi 23/01/2023

TAHADHARI: Upepo mkali kuipiga Dar kwa siku nne mfululizo kuanzia tarehe 20 hadi 23/01/2023

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba vinatarajiwa kukumbwa na upepo mkali wa kasi ya kilometa 40 kwa saa kwa muda wa siku nne mfululizo. kuanzia Januari 20 hadi 23 mwaka huu.

Utabiri uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA inaonesha kuwa upepo huo unaoipiga pwani ya bahari ya Hindi utaambatana na mawimbi makubwa ya bahari yanayoifikia urefu wa mita mbili.

Akitoa taarifa za utabiri huo, Mchambuzi wa Hali ya Hewa wa TMA Rose Senyagwa amesema, upepo huo utaathiri shughuli za usafirishaji katika sekta ya bahari na kuleta athari katika makazi ya watu yatakayofikiwa na hali hiyo.!
Fm1Ul4-XgAEMV3f
 
Bado sijaanza kuusikia , ila bora upepo uje tu maana joto lilizidi
 
Wanaume wa Dar mshaanza kujawa na kitete kisa upepo tu
 
Wanaume wa dar mshaanza kujawa na kitete kisa upepo tu
Kuna nguvu za asili ambazo ni maji, upepo, na moto (jua).

Maji yakizidi huitwa mafuriko, mafuriko yanaua bila kujalisha wewe ni mwanaume wa Dar au wa mkoani.

Upepo ukizidi huitwa kimbunga, huangusha miti, huezua mapaa, huleta uharibifu mkubwa wa mali na uhai wa mwanadamu.

Jua likizidi huitwa kiangazi. Litakausha kila tone ya maji.

Kijana jifunze kuwa na heshima hata kwa watu unaowaona ni wadhaifu kwako.
 
Nipo Kunduchi Beach hapa, hakuna hata tawi linalotikisika.......labda huo upepo ni wa bluetooth.
 
Mikoa ya Lindi, Mtwara, Tanga, Pwani, Dar es Salaam, Visiwa vya Mafia, Unguja na Pemba vinatarajiwa kukumbwa na upepo mkali wa kasi ya kilometa 40 kwa saa kwa muda wa siku nne mfululizo. kuanzia Januari 20 hadi 23 mwaka huu.

Utabiri uliotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini TMA inaonesha kuwa upepo huo unaoipiga pwani ya bahari ya Hindi utaambatana na mawimbi makubwa ya bahari yanayoifikia urefu wa mita mbili.

Akitoa taarifa za utabiri huo, Mchambuzi wa Hali ya Hewa wa TMA Rose Senyagwa amesema, upepo huo utaathiri shughuli za usafirishaji katika sekta ya bahari na kuleta athari katika makazi ya watu yatakayofikiwa na hali hiyo.!
Fm1Ul4-XgAEMV3f
Nikweli jana maeneo ya Ubungo ilinyesha mvua na upepo mchana sana
 
Mbona kama Speed ya 40km/h ni ndogo? Labda wataalamu watueleze vizuri humu
 
Back
Top Bottom