JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 685
- 1,124
Kwa mujibu wa wataalamu wa afya, ‘surgical masks’ na mask aina ya N95 hazipaswi kufuliwa wala kuvaliwa zaidi ya mara moja. Baada ya matumizi, ikiloa au kila baada ya saa 4, mask ivuliwe kwa umakini na kutupwa
Mask inapofuliwa, inapoteza ubora wake na hivyo kuathiri uwezo wa awali wa kuzuia unyevu kutoka au kuingia kwa sababu malighafi yake haihimili ufuaji
Barakoa za kitambaa zifuliwe na kupigwa pasi kila zinapovuliwa ili kuua vijidudu vyovyote. Ni vyema ukawa na barakoa za kitambaa zaidi ya moja ili kurahisisha ufuaji na kuhakikisha inakauka vyema
Usitoke nje ya nyumbani kwako bila barakoa. Kumbuka kuvaa barakoa si mbadala la kunawa kwa maji tiririka na sabuni au kitakasa mikono
#JFCOVID19_Updates #Barakoa
Mask inapofuliwa, inapoteza ubora wake na hivyo kuathiri uwezo wa awali wa kuzuia unyevu kutoka au kuingia kwa sababu malighafi yake haihimili ufuaji
Barakoa za kitambaa zifuliwe na kupigwa pasi kila zinapovuliwa ili kuua vijidudu vyovyote. Ni vyema ukawa na barakoa za kitambaa zaidi ya moja ili kurahisisha ufuaji na kuhakikisha inakauka vyema
Usitoke nje ya nyumbani kwako bila barakoa. Kumbuka kuvaa barakoa si mbadala la kunawa kwa maji tiririka na sabuni au kitakasa mikono
#JFCOVID19_Updates #Barakoa