Tahadhari

Tahadhari

Shimilimana

Member
Joined
Mar 12, 2013
Posts
52
Reaction score
15
Salute wana Jf wote: Baada ya kuwa nimefuatilia kwa muda mrefu namna ya hii mitandao ya kuuza bidhaa za tiba lishe/food supplements/food dietary, nimegundua kuwa tiba lishe kama ilivyo haina tatizo bali wasambazaji wake ndiyo wenye tatizo. Mojawapo ya tatizo kubwa nililoliona ni kwa wale wasambazaji wanaomcha Mungu, nimegundua ni wengi sana kama siyo robo tatu ya wote ambao ndiyo hasa nimesukumwa kuwapa tahadhari kwa hiki wanachokifanya. Baada ya kuahidiwa utajiri kwa kushawishi watu kujiunga na mitandao hii, wanatumia nguvu nyingi ikiwemo uwongo ili kuwavuta watu kujiunga na mitadao hii badala ya kutumia nguvu hiyo na ukweli kuwafanya watu wamche Mungu ili wapate utajiri usiyo na mwisho wala majuto. Mwenye kuelewa na aelewe, tubadilike ili tuepuke hasira ya Mungu baada kuwa tumeondoka hapa dudiani na kuuacha utajiri huu wenye hila. Thanks, be blessed
 
sijui umeandika nini mkuu jiange tena iliueleweke..

:coffee:
 
Salute wana Jf wote: Baada ya kuwa nimefuatilia kwa muda mrefu namna ya hii mitandao ya kuuza bidhaa za tiba lishe/food supplements/food dietary, nimegundua kuwa tiba lishe kama ilivyo haina tatizo bali wasambazaji wake ndiyo wenye tatizo. Mojawapo ya tatizo kubwa nililoliona ni kwa wale wasambazaji wanaomcha Mungu, nimegundua ni wengi sana kama siyo robo tatu ya wote ambao ndiyo hasa nimesukumwa kuwapa tahadhari kwa hiki wanachokifanya. Baada ya kuahidiwa utajiri kwa kushawishi watu kujiunga na mitandao hii, wanatumia nguvu nyingi ikiwemo uwongo ili kuwavuta watu kujiunga na mitadao hii badala ya kutumia nguvu hiyo na ukweli kuwafanya watu wamche Mungu ili wapate utajiri usiyo na mwisho wala majuto. Mwenye kuelewa na aelewe, tubadilike ili tuepuke hasira ya Mungu baada kuwa tumeondoka hapa dudiani na kuuacha utajiri huu wenye hila. Thanks, be blessed

Kweli mkuu, naona wao mahubiri ni kutapeli watu kwa lishe na tiba ambazo hazipo
 
sijui umeandika nini mkuu jiange tena iliueleweke..

:coffee:

kama umesoma vizuri kuna mahali nimesema mwenye kuelewa na aelewe nikitambua kuwepo kwa watu kama wewe watakaoshindwa kunielewa. Asante, barikiwa
 
Mkuu ni kweli kabisa, ni utapeli wa kupitiliza ili mradi wao wapate hizo bonus zao.
 
kama umesoma vizuri kuna mahali nimesema mwenye kuelewa na aelewe nikitambua kuwepo kwa watu kama wewe watakaoshindwa kunielewa. Asante, barikiwa

Ni kwepi hujaeleweka ndugu..Fafanua vizuri hii mitandao ni ipi na wanashawishi kivipi..Je una maanisha akina Dk Ndodi?
 
Kumbe sio mie pekeyangu ambaye sijaelewa.... 😕 😕

Nilifahamu uwepo wa watu watakaoshindwa kunielewa kama wewe ndiyo maana ukisoma utaona nikisema kuwa mwenye kuelewa na aelewe hivyo isikuchanganye sana ndg. Asante, barikiwa
 
sielewi mtoa mada ana maanisha watu wanavutwa kujiunga na mitandao ya jamii au wanavutwa kwenye biashara
 
Ni kwepi hujaeleweka ndugu..Fafanua vizuri hii mitandao ni ipi na wanashawishi kivipi..Je una maanisha akina Dk Ndodi?

sina shida na watu kama kina Ndodi kwani wao wanatoa tiba na kufundisha watu kufuata kanuni bora za afya ili wawe mbali na magonjwa tofauti na mitandao kama GNLD, wao wana kauli mbiu isemayo 'KULA SEMA' ambayo inatumika kuwapatia utajiri, pia mtandao huu haufundishi watu jinsi ya kuwa na afya njema pale wanapofanya semina zao bali huwataka watu kujiunga nao ili kusambaza(kuuza) supplements, mimi ni shahidi wa hayo kwani nimewahi huhudhuria semina zao. Mitandao mingine ni forever living na mingineyo, tukumbuke Mungu pekee ndiye FOREVER LIVING, thanks
 
Shimilimana hapa nimekuelewa humu walikuwemo wengi baada ya kupata mashushu mtu anakuja na tatizo lake mtoto analia sana usiku unasikia ooh tumia FOREVER LIVING za kazi gani tumia suppliment pale unaposhauriwa na Dr. na iwe ni tatizo la haraka vinginevyo vyakula natural vya hizo suppliment si vipo.
 
Last edited by a moderator:
sina shida na watu kama kina Ndodi kwani wao wanatoa tiba na kufundisha watu kufuata kanuni bora za afya ili wawe mbali na magonjwa tofauti na mitandao kama GNLD, wao wana kauli mbiu isemayo 'KULA SEMA' ambayo inatumika kuwapatia utajiri, pia mtandao huu haufundishi watu jinsi ya kuwa na afya njema pale wanapofanya semina zao bali huwataka watu kujiunga nao ili kusambaza(kuuza) supplements, mimi ni shahidi wa hayo kwani nimewahi huhudhuria semina zao. Mitandao mingine ni forever living na mingineyo, tukumbuke Mungu pekee ndiye FOREVER LIVING, thanks
Wote hao lao moja, waweza danganyika ukafikiri wanasaidia kumbe ni pupa za kutaka mapesa tu, matapeli/wezi hao wote
 
Unategemea kwa matokeo ya O-level vikundi hivyo si ndio vitapata wafuasi wengi coz wengi wao wameshajikatia tamaa na matokeo wanaangalia shortcut ya maisha.
 
Unategemea kwa matokeo ya O-level vikundi hivyo si ndio vitapata wafuasi wengi coz wengi wao wameshajikatia tamaa na matokeo wanaangalia shortcut ya maisha.
Ni kweli MadamG unayosema, ni budi tufahamu kuwa shortcut yoyote kwa jambo lolote ktk maisha itatuletea madhara na majuto makubwa, pengine ktk maisha yetu yote.....Tuhesabu gharama kabla ya kujenga MNARA.... Thanks
 
sina shida na watu kama kina Ndodi kwani wao wanatoa tiba na kufundisha watu kufuata kanuni bora za afya ili wawe mbali na magonjwa tofauti na mitandao kama GNLD, wao wana kauli mbiu isemayo 'KULA SEMA' ambayo inatumika kuwapatia utajiri, pia mtandao huu haufundishi watu jinsi ya kuwa na afya njema pale wanapofanya semina zao bali huwataka watu kujiunga nao ili kusambaza(kuuza) supplements, mimi ni shahidi wa hayo kwani nimewahi huhudhuria semina zao. Mitandao mingine ni forever living na mingineyo, tukumbuke Mungu pekee ndiye FOREVER LIVING, thanks

Sasa umeeleweka.Ni kweli hao ni matapeli. mie siwaamini.Wanatamanisha watu kuwa na utajiri wa haraka
 
Iwapo unakula chakula bora utapata viini vyote ambavyo vinahitajika na mwili. Hutahitaji hizo supplement zinazokazaniwa na hao wanapyramid schemes mbalimbali.
 
Back
Top Bottom