mutisya mutambu
JF-Expert Member
- Nov 21, 2010
- 208
- 82
Leo nikiwa ndani ya daladala asubuhi akaja dogo dent akaketi siti ya pembeni muda kidogo katoa daftari na kuanza kupitia notice nadhani alikuwa anaelekea kwenye paper ile asubuhi...sasa na mi nikapiga chabo kidogo kilichomo ndani ya notice..ee bwana ehe...types of wines,procedures of serving dinner to customers...etc yote yakionesha dogo anasoma mambo ya hotel.. .hapo najiuliza sasa mbona hivi vyuo vimekuwa vingi sana sasa na vyote ni hotel,ba,tourism hivi huku ndiko tulikoona kutatoa jamani!!! Ule mwelekeo wa siku za nyuma ambapo mtoto akishindwa kufaulu wazo la kwanza lilikuwa vyuo vya ufundi kama cherehani,ufundi magari,umeme,useremali,ujenzi kwa nini tumeuacha huo na kukimbilia huku ambako hata ukimaliza bado shida unayo ya kutembea na bahasha kwenye migahawa ya wahindi kuomba kazi...nadhani kama taifa tubadilike sasa..tunaelekea shimoni kwa kuhamasisha hizi kozi za utumwa huko mbele na si kujituma......tukumbuke tulipochepukia turudi hapo tuendelee njia kuu...tuendako hakuna kitu tunapotea.
Karibuni wachangiaji kwa hoja
Karibuni wachangiaji kwa hoja