Taifa Stars imesukumwa nje ya mashindano ya awali ya kombe la dunia kwa aibu ya kipigo cha mabao 7-0 toka kwa Algeria. Kilimanjaro Stars (ya Tanzania Bara) imetupwa nje ya michuano ya Challenge kwa kutolewa na Ethiopia kwa penati. Hata Zanzibar Heroes nayo imetupwa nje.
Tuifanyaje Taifa Stars/Kilimanjaro Stars ili iweze kufanya vyema kwenye michuano ya kimataifa? Tuivunje na kuunda mpya? Tuiache na kuiimarisha iliyopo? Tufanyaje hasa? Inauma sana kushangilia timu za taifa za nje na kuiacha yetu ikidorora.
Tuchangie waungwana.
Nakala kwa
Jamal Malinzi