Taifa Stars waanza mazoezi chini ya Emmanuel Amunike

Taifa Stars waanza mazoezi chini ya Emmanuel Amunike

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
30 August 2018
Dar es Salaam, Tanzania

Wachezaji wote wa Taifa Stars wakiwemo wale walioitwa kuchukua nafasi ya wachezaji waliotimuliwa wa Simba SC, wameanza rasmi mazoezi chini ya Kocha Emmanuel Amunike leo jijini Dar-es-Salaam.

Kocha Amunike toka Nigeria, aliwahi kuzitumikia kama mchezaji kwa mafanikio makubwa timu ya taifa ya Nigeria na timu kadhaa za kubwa barani Ulaya ikiwemo ya Barcelona.

Emmanuel Amunike hakuwa mchoyo kuzungumzia filosofia yake ya kwanza ktk mazoezi ya jinsi ya 'timu na mchezaji' kumiliki mpira kwa manufaa ya timu kulinda na kupata ushindi.

Kocha ameonesha kuridhishwa na mapokeo ya mafunzo kwa wachezaji na ari yao ya kufanya mazoezi na hivyo kuwa na matumaini makubwa ya timu kufanya vizuri.

Source : MCL digital
Wadau wengi wa soka wamesema, ujio wa Amunike ni fursa kwa wachezaji wa ndani Tanzania kuongeza bidii, nidhamu ndani na nje ya viwanja na kufuata maelekezo ya kocha huyo mpya ili wapate kuwa wachezaji wa kimataifa kama Mbwana Samatta, Simon Msuva kwa kuwataja kwa uchache.

Fursa hiyo ni kutokana na Emmanuel Amunike kufahamika kimataifa na mtandao wake ktk ulimwengu wa soka basi wachezaji wa-Kitanzania wakisikiliza,kujifunza, kufanya mazoezi kwa bidii bila shurti wanaweza kuunganushiwa ulaji ktk timu kubwa barani Afrika, Ulaya na Marekani.
 
26 Feb 2016
Flying Eagles coach, Emmanuel Amunike spoke in a session at Social Media Week in Lagos 2016. He is the current Assistant Coach of the Super Eagles.

Source: Pulse Nigeria
 
Emmanuel Amunike on football academy

 
Mazoezi ya Aishi Manula chini ya Kocha wa Taifa Stars ni balaa

31 Aug 2018
Kocha wa timu ya Tanzania, Taifa Stars, Emmanuel Amunike, amekutana na wachezaji Simba aliowaondoa kwenye kikosi chake baada ya kuchelewa kuripoti kambini. Baada ya kukutana nao, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Clifford Ndimbo ametoa taarifa kuwa suala hilo limekwisha na kwamba hakuna kitakachozuia nyota hao kuitwa tena Stars kama tu wataonyesha kiwango kizuri kwenye klabu yao. Ndimbo ameeleza kuwa Amunike ameshamalizana na wachezaji wa Simba na atawaita tena endapo wataonesha kiwango kizuri ambacho kitamshawishi wakiwa kwenye klabu yao. Licha ya kusamehewa, wachezaji hao wataukosa mchezo wa kuelekea kufuzu AFCON dhidi ya Uganda, Septemba 8 2018 huko Kampala. Nyota hao sita watakosekana kutokana na nafasi zao kujazwa na wachezaji wengine ambao tayari wameshaanza mazoezi jana kwenye Uwanja wa Boko Veterani uliopo pembezoni kidogo mwa jiji la Dar es Salaam.
Source : ShutikaliTV
 
Nidhamu ndo chachu ya mafanikio, utovu wa nidhamu na kutlkuheshimu ratiba ndo ugonjwa haswa wa watanzania. Wamezoea taarabu na kujikokota kokota tu
 
Back
Top Bottom