Tango73
JF-Expert Member
- Dec 14, 2008
- 2,180
- 1,291
ILi kucheza world cup tunahitaji kocha mwenye kufundisha timu kucheza hadhai ya ligi kuu za ulaya magharibi. Huwezi kucheza world cup ikiwa kocha wako ndiyo wa kufundisha timu daraja la nne. Ivory cost, moroco na gambia wapo juu sana kisoka . Tanzania sasa hivi tuna wachezaji wanaohitaji kuzoea formation ya kucheza soka na sio wale wale wa kufundishwa pasi na kupangwa uwanjani wakambane adui. KIla kukicha tunajiona hatujui mpira ingawa tunawachezaji wazuri. Hii yote ni kwa sababu ya ufundi mdogo wa kocha tuliyenae. Huu ni wakati wa kumchukua kocha kama vile fillipe scorali,mario zagaro,kocha wa uruguayi wa zamani, Frank rijkard au johan cruf. Wadau tunao, wadhamini tunao, na serikali yetu ina hamasa za michezo. Ina maana hata kumlipa kocha huyo kwa miezi sita tuu tutashindwa? Huyo kocha anakuja kwa ajiri ya kutuvusha kucheza fainali tuu za brazil na sio kukaa hapa miaka miwili. Ndugu DR Nchimbi unasemaje suala hili? au wana JF mnasemaje?