Tajiri anataka niandike barua ya kuacha kazi

hoyugi

Member
Joined
Jul 3, 2013
Posts
73
Reaction score
12
Habari wana jamii?

Nilitofautiana kauri na mtoto wa bosi, baada ya hapo nikaandika barua ya kuomba msamaha. Cha ajabu boss anataka niandike barua ya kuacha kazi!

Naombeni msaada wenu jamani nipate haki yangu.
 
Usiandike barua ya kuacha kazi. Tulia.
 
Usiandike barua ya kuacha kazi, kwani umeajiriwa au kibarua? Kutokuingia na cm ni shart la kaz yako? Omba tu msamahaaaa
 
usiandike barua huyo anataka kukufukuza kazi sasa anashindwa hana sababu ya kukufukuza maana unaweza mshtaki, sasa anataka ionekane umeaacha kazi kwa hiari yako. Uwe makini naye huyo atakutafutia sababu na ukiingia kwenye 18 zake tu umeumia.
 
usiandika barua ya kuacha kazi......umeshaomba msamaha tayari kama akikufukuza yeye njoo tukuambie cha kufanya

ila kwa sasa usiandika barua ng'o!
 
pole sana na kwa yaliyokukuta.ila mwambie tu kama anataka akufukuze akupe barua ya kuacha kazi ila usiandike barua ya kuacha kazi maana utapoteza haki zako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…