Takataka za miwa Mbagala

Takataka za miwa Mbagala

FORWARD

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2014
Posts
740
Reaction score
293
Habari za sikukuu!

Biashara ya miwa imeshika kasi sana maeneo ya Mbagala hasa toka kizuiani mpaka Mbagala rangi tatu, ukipita njia ya Mbagala maeneo hayo utakuta vijana wengi sana wanajipatia ridhiki yao kwa kufanya biashara hiyo ambayo kiukweli inafanya vizuri kutokana na muonekano wa maeneo biashara hiyo inapofanyika.

Wateja wengi wa biashara hiyo ni watu walio kwenye vyombo vya usafiri haswa mida ya foleni kipindi cha jioni. Tatizo lililopo ni kwamba walaji wengi wa hiyo miwa pamoja na wauzajj hawazingatii swala la usafi wa mazingira wa maeneo biashara hiyo ilipo kwani utupaji hovyo wa makapi ya miwa baada ya kutafunwa unafanyika maeneo hayo kiasi kwamba kuanzia makapi ya miwa yaliyozagaa barabarani, pamoja na kwenye mitaro.

Nawasihi wahusika ambao wauzaji wazingatie swala la usafi wa mazingira kwa kuzikusanya taka hizo ili zikatupwe kwenye dampo lililo rasmi na wateja walio kwenye magari wasitupe hovyo makapi ya miwa waliotafuna bali watupe kwanye ndoo za taka zilizopo kwenye mabasi ya abiria.
 
Takataka za miwa zitakuja kuwa janga kubwa kama wahusika hasa serikali na wananchi tutakaa kimya maana sio Mbagala tu.
 
mtu na akili zake kabisa(Sijui kama ni TIMAMU) anatupa uchafu sehemu ya public bila hata kujali(Sijui anahisi kuna watu wa kufanya usafi)
halafu taka zikijaa mtu huyo huyo anaanza kulalamika "Haya maeneo machafu kweli"

Mi nashangaa sana

kuja kufikia civilization ya first world countries SIO LEO
 
Habari za sikukuu!

Biashara ya miwa imeshika kasi sana maeneo ya Mbagala hasa toka kizuiani mpaka Mbagala rangi tatu, ukipita njia ya Mbagala maeneo hayo utakuta vijana wengi sana wanajipatia ridhiki yao kwa kufanya biashara hiyo ambayo kiukweli inafanya vizuri kutokana na muonekano wa maeneo biashara hiyo inapofanyika.

Wateja wengi wa biashara hiyo ni watu walio kwenye vyombo vya usafiri haswa mida ya foleni kipindi cha jioni. Tatizo lililopo ni kwamba walaji wengi wa hiyo miwa pamoja na wauzajj hawazingatii swala la usafi wa mazingira wa maeneo biashara hiyo ilipo kwani utupaji hovyo wa makapi ya miwa baada ya kutafunwa unafanyika maeneo hayo kiasi kwamba kuanzia makapi ya miwa yaliyozagaa barabarani, pamoja na kwenye mitaro.

Nawasihi wahusika ambao wauzaji wazingatie swala la usafi wa mazingira kwa kuzikusanya taka hizo ili zikatupwe kwenye dampo lililo rasmi na wateja walio kwenye magari wasitupe hovyo makapi ya miwa waliotafuna bali watupe kwanye ndoo za taka zilizopo kwenye mabasi ya abiria.
Tabia hizi zipo kila Kona... Jamani tubadilike
Hulka na uchafuzi wa mazingira haikubaliki ..
Inasikitisha Kuona hali ya usafi nchini ni duni sana (zero)... Yaani maafa yake yataturudia sisi wenyewe!!
Mamlaka na wahusika na manispa chukueni hatua...
 
mtu na akili zake kabisa(Sijui kama ni TIMAMU) anatupa uchafu sehemu ya public bila hata kujali(Sijui anahisi kuna watu wa kufanya usafi)
halafu taka zikijaa mtu huyo huyo anaanza kulalamika "Haya maeneo machafu kweli"

Mi nashangaa sana

kuja kufikia civilization ya first world countries SIO LEO
Well said... onyo linatuhusu site....
Usafi ni Moja ya maendeleo na Ustaarabu
Na kings ya afya zetu..
Usafi usafi...usafi..
 
Hivi kwani ile sheria ya utupaji taka ovyo unatoa faini haipo tena?
Usafi ni tabia wala sio issue ya kushurutishwa na mtu,ni jambo la kimalezi toka utotoni,tuanze kuwafundisha watoto toka utotoni issue ya usafi na kuweka mazingira katika hali safi,mtu mzima na midevu yake ukimwambia kwanini unatupa taka hapa? mnaweza hata kupigana badala ya yeye kuelewa kua lile ni kosa na sio ustaarabu!
 
Usafi ni tabia wala sio issue ya kushurutishwa na mtu,ni jambo la kimalezi toka utotoni,tuanze kuwafundisha watoto toka utotoni issue ya usafi na kuweka mazingira katika hali safi,mtu mzima na midevu yake ukimwambia kwanini unatupa taka hapa? mnaweza hata kupigana badala ya yeye kuelewa kua lile ni kosa na sio ustaarabu!
Kuna watu pasipo shurti hawaendi
 
Hilo halitakiwi kuwa tatizo inatakiwa kuwa fursa.Maana nasikia ktmoto wanapenda sana kula miwa.
 
Mkuu kama umeniwahi aisee amna kitu nakerwa nacho kama takataka za miwa hasa kuanzia eneo la jeshi pale mpka zakiem na hii tabia ya biashara za machinga kuzuia barabara kila siku foleni ni kero kubwa mno kwangu yan huwa naichukia mbagala tukianzia kipande cha kizuiani mpaka rangi 3 watu wanapanga biashara barabarani na hadi iyo miwa mtihani sanaa.
 
Inzi wanapenda sana taga mayai kwenye hizo taka taka za miwaa... na kipindi cha mvua ndo inzi wanaongezekaaa

Siku Inzi akiwa serious kama nyuki, basi mambo yatabadilika sana
 
kwakweli, Tatizo hilo mbagala ni kubwa hawa wauza miwa wamekuwa wachafuzi wa mazingira vibaya mno mno.
 
Inzi wanapenda sana taga mayai kwenye hizo taka taka za miwaa... na kipindi cha mvua ndo inzi wanaongezekaaa

Siku Inzi akiwa serious kama nyuki, basi mambo yatabadilika sana
Hebu pandikizeni Inzi wa kipindupindu hapo, watu wata- surrender wenyewe! Maana mtu msafi kamwe hapati kipindupindu, never!
 
Back
Top Bottom