Take One: Wema Sepetu akiri kutoa Mimba

Take One: Wema Sepetu akiri kutoa Mimba

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
Nipo naangalia kipindi cha Take One cha Zamarad Mketema.

Wema kakiri kuwa alitoa mimba maana hakuwa tayari kwa wakati ule.Ilikuwa mwaka 2008 na mimba ilikuwa ya marehemu Steven Kanumba.

Kanumba alikuwa akimwambia kuwa ntakudai watoto wangu, kauli hii inamaanisha kuwa alitoa mimba zaidi ya moja.

Akizungumzia kuhusu kupata mtoto amesema anatamani sana kuwa na mtoto lakini ndio hivyo tena kahangaika sana lakini hajafanikiwa.Anadai labda wakati anatoa kuna vitu viliguswa ndio maana hafanikiwi kupata mtoto.

Anasema anajuta/hajuti kukosa mtoto.

Pia amekiri alihongwa BMW,kuhusu MURANO anasema lilikuwa na matatizo ya shockup na halikuwa katika hali nzuri.

Part IV: Wema Sepetu Interview kuhusu Mtoto na Diamond, ujauzito wa Zari, alivyotoa mimba


Part III: Wema Sepetu alipoulizwa boyfriend wake wa sasa, ile BMW, mapenzi ya kuachana, CK na mengine


Part II: Wema Sepetu Interview on TAKE ONE kuhusu Kajala na msamaha



Part I: Wema Sepetu aeleza kwanini hatomsamehe Kajala - kwenye TAKE ONE



Heshima kwenu wadau;
Sheria za Tanzania haziruhusu suala la Utoaji wa mimba katika Criminal Procdure Act ,1985 .
Katika sheria hio hio suala hili limejumuishwa katika makosa ya "Murder" ambayo makosa yake yanaweza kwenda kifungo cha maisha au kifo

Katika jedwali la Adhabu inaonesha adhabu zifuatazo kwa watu wanaotoa au kushiriki kutoa Mimba


  • 150.Attempt to procure abortion. -Imprisonment for fourteen years.
  • 151.Woman attempting to procure her own abortion. -Imprisonment for seven years.
  • 152.Supplying drugs or instruments to procure abortion. -Imprisonment for three years

Katika jamii yetu kuna watu ambao aidha kwa mazuri au mabaya yao wamekuwa wakiangaliwa na watu wengi.Vyombo vya habari pia vimekuwa vikiuza kwa kuwataja kutokana na scandals zao.

Hapa namwongelea Wema Sepetu ambaye yeye pia anaandikwa sana hasa na Magazeti ya "Udaku"

Magazeti haya yanasomwa sana na jamii kubwa ya watanzania hasa kutokana na hali zetu za elimu na "mazingira"

Huyu Binti amefikia hatua ya Kusema "Proudly" kuwa alitoa mimba kwa sababu hakuwa tayari,hili amelisema wakati akihojiwa na mtangazaji Zamaradi mketema wa Clouds TV;

Implication yake ni nini?


  1. Kwa wale wasio na uelewa mpana wataona kwamba ni sawa tu kutoa mimba kwa sababu wema ameongea proudly NA hakuna kilichofanyika
  2. Serikali inadhalilishwa wazi kuwa watu wanapigia kampeni suala la utoaji wa mimba kuwa ni halali tu
  3. Taasisi za Haki za binadamu hazifanyi kazi ipasavyo kiasi cha watu kama hawa kuachwa bila kukemewa.Huyu binti ameua na amekiri kwa mdomo wake kuua.
  4. Vyombo vya haki ya mama na Mtoto vinashindwa kuchukua hatua stahiki hata katika mazingira yaliyo wazi

Wito wangu;

Wahusika niliowataja hapo juu wachukue hatua ili kuiepusha jamii yetu na mambo kama haya
 
Last edited by a moderator:
Hapo sasa kazi kwenu. Masela watakata funua na wataigonga kigumu , kigangstar. Takukuru ya mtaa
 
Aaagh aache uongo siku hiyo hata Murano mpya hata bila hata plate numbers, ilifikaje kupewa nyumbani kwake? hakuikimbilia ya aliyopewa na ex wake alikimbilia BMW.

Yaani muongo sana huyu, manager Martin Kadinda wake alisema na kuandika watu wamechanga na kununua sasa anasema amehongwa

Kuna cha ukweli anachosemaga huyu zaidi ya kutaka kuona ex wake ameshuka kikazi kuomba wafuasi waende kiupinzani nae?

Juu ya mimba hakuna sheria ya kuua Tanzania? Mbona anaiongelea sana, kuna watafuta mimba hawapati yeye anaongelea kila mara kama ni kitu kizuri alichotenda. Inaudhi
 
Mi nasema kwa kuwa hayupo tu, huyo muongo mxiuu
Anavopenda kuongelea swala la kutoa mimba utadhani anaongea kitu kizuri huyu mheshimiwa sijui vipi, au ndo anadhani atahurumiwa
 
Heheee dah kweli ndo maana wanawake tunaugua maradhi ya ajabu ajabu...
Wee kenge sitaki uniqoute Leo nina stress za kumsubiria mume mpaka saa hizi
 
Nipo naangalia kipindi cha Take One cha Zamarad Mketema.

Wema kakiri kuwa alitoa mimba maana hakuwa tayari kwa wakati ule.Ilikuwa mwaka 2008 na mimba ilikuwa ya marehemu Steven Kanumba.

Kanumba alikuwa akimwambia kuwa ntakudai watoto wangu, kauli hii inamaanisha kuwa alitoa mimba zaidi ya moja.

Akizungumzia kuhusu kupata mtoto amesema anatamani sana kuwa na mtoto lakini ndio hivyo tena kahangaika sana lakini hajafanikiwa.Anadai labda wakati anatoa kuna vitu viliguswa ndio maana hafanikiwi kupata mtoto.

Anasema anajuta/hajuti kukosa mtoto.

Pia amekiri alihongwa BMW,kuhusu MURANO anasema lilikuwa na matatizo ya shockup na halikuwa katika hali nzuri.

Wema ana umwa kabisa...!
mgombea ubunge viti maalum kupitia ccm mkoa wa singida
 
Hivi m2 anataka mimba wkt hajaolewa,hiyo mimba ataipataje.angekuwa analalamika huku akiwa na mume ndani ningemuelewa.
 
Wangapi wanaweza kukiri hadharani kwamba walitoa mimba? Au walihongwa?


Wengi wanakufaga na siri moyoni tu
 
Huo uongo nimesikiliza lipind mwanzo mwsho hakukuwa na mahojiano hayo.msiyudanganye jaman hata kwetu tv zipo .looooooh tafuten mengine sio ya watu
 
Back
Top Bottom