TAKUKURU, Je inatimiza wajibu wake?

TAKUKURU, Je inatimiza wajibu wake?

Juaangavu

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2009
Posts
935
Reaction score
132
Jamani hii taasisi inatimiza wajibu wake kama ilivyo kusidiwa; au imegeuka kuwa ni sehemu ya polisi wa upelelezi. Ninaitafakari na kujiuliza maswali mengi ya kiuchokonozi mara zote ninajikuta nipo kizani. Nilifikiri lengo la hii taasisi ni kuangalia ‘loop holes’ zilizopo ndani ya mashirika ya umma na serikali zinazosababisha rushwa –kubwa na ndogo ndogo, kisha ku-design mifumo/taratibu zitakazoziba hiyo mianya; na pia kuhakisha kuna-ufuatiliaji wa kina ambao hautatoa mwanya wa rushwa. Lakini hali ninayoina inaelekea kuwa kinyume kabis, taasisi ipo ili isubiri taarifa za nani kadokoa wapi; na cha kusikitisha zaidi ni pale unapoina taasisi hiyo iko ‘busy’ na virushwa vidogo vidogo (dhambi ni dhambi tu haijalishi ni kubwa au ndogo) ili hali wale wanaokimbia na vijisenti vyetu wakiabudiwa badala ya kushughulikiwa ipasavyo. Je, taasisi haina wataalamu wa kutosha ili kutimiza lengo la kuwepo kwake; au sheria iliyoiweka madarakani haikuipa meno ya kuweza kutimiza kile ilichoundiwa? Je haina maono ya kuiwezesha kutimiza wajibu wake? Je, sisi watanzania tunapata thamani halisi ya kodi yetu (value for money) kwa fedha zinazotumika kuwalipa mishahara, malupulupu, na gharama za mjengo wao walioamua kujijengea? Tutafakari.
 
Kw upand mmoja inatimiza, na kwa upande mwingine haitimizi.
Nasema hivyo kwa sababu TAKUKURU imekuwa ni chombo cha kutimiza matakwa ya baadhi ya watu fulani na si kutimiza matakwa yaliyosababisha chombo hicho kiundwe kisheria.
Viongozi wa ngazi za juu serikalini wamekinyima haki yake ya kufanya kazi husika na hivyokinawakumbatia tu wakubwa.
 
Kw upand mmoja inatimiza, na kwa upande mwingine haitimizi.
Nasema hivyo kwa sababu TAKUKURU imekuwa ni chombo cha kutimiza matakwa ya baadhi ya watu fulani na si kutimiza matakwa yaliyosababisha chombo hicho kiundwe kisheria.
Viongozi wa ngazi za juu serikalini wamekinyima haki yake ya kufanya kazi husika na hivyokinawakumbatia tu wakubwa.
Jamani tufanye nini ili tukinasue ktk mtego huu wa viongozi wa ngazi za juu? Manake wasio waadirifu ndo wataendelea kula rushwa bila hata soni, wakijua jinsi walivyokiteka chombo chenyewe.
 
Imesikitisha kuona kwamba Takukuru iko chini ya uongozi wake wa sasa! Hakuna chochote kitakacho fanyika bila ya kuisafisha yenyewe kwanza! Kuna mambo ya kutisha yanayoendelea pale, na kubwa ni wao kujilimbikizia ulaji kwa ahadi ya kukulinda!Ole wako usitoee, utakoma!
 
Back
Top Bottom