TAKUKURU kuanza kushughulikia kesi za mimba za utotoni zinazomalizwa kinyemela mitaani

TAKUKURU kuanza kushughulikia kesi za mimba za utotoni zinazomalizwa kinyemela mitaani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeagizwa kushughulikia kesi za mimba za utotoni ambazo zimekuwa zikiishia mitaani badala ya kwenda kwenye vyombo vya sheria.

Vilevile, imeagizwa kufanya utafiti kuhusu rushwa ya ngono kwa vyuo vikuu vingine na vyuo vya kawaida, kama ilivyofanyika kwa vyuo vikuu vya Dodoma (UDOM) na Dar es Salaam (UDSM) ili kutokomeza rushwa hiyo.

Maagizo hayo yalitolewa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora na Menejimenti ya Utumishi wa Umma), Deogratius Ndejembi, alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa TAKUKURU wa kutathmini utendaji kazi kuanzia Julai 2019 hadi Juni 2020.

Alisema amekuwa akishuhudia kesi kama hizo nyingi katika maeneo mbalimbali zikiishia mitaani, na kutaka taasisi hiyo ilivalie njuga suala hilo ili kuwashughulikia wanaofifisha ndoto za watoto.

“Unakuta kesi nyingi za mimba mnazifuatilia ama kuzipeleka mahakamani, lakini ikifikia mahakamani mhusika hatokei au anakana tukio, ukifuatilia unakuta wahusika wamemalizana mtaani kwa kulipana faini, jambo hilo halikubaliki,” alisema Ndejembi.

Aliongeza: “Hii imekuwa ni desturi ya wazazi pale unapowakamata wahusika wao humalizana kesi na watendaji.”

“Unakuta mwalimu amempa mimba mwanafunzi, lakini ukiifuatilia hiyo mwisho wa siku unakuta mtenda kosa yupo mtaani na ukiuliza unaambiwa alimazana na wazazi wa mwanafunzi.

“Ninaomba TAKUKURU mtusaidie kufuatilia suala hili kwa sababu linakuwa sugu na wahusika wanajisikia vibaya kuona watu wanaotenda makosa kama hayo wapo mtaani ilihali wao maisha yao yameharibika,” alisema Ndejembi.

Alisema sheria ipo na hao wazazi wanaofanya vitendo hivyo wawajibishwe kwa mujibu wa sheria za nchi zinavyoelekeza ili hizo mimba za utotoni ziishe.

Alisisitiza wazazi kuhakikisha wanaacha vitendo hivyo kwa kuwa wanakatisha ndoto za watoto wao.

Ndejembi alisisitiza idara ya elimu, halmashauri zihakikishe kesi hizo zinazofanyiwa kazi na mamlaka mbalimbali ili kuhakikisha wanafunzi hao wanapata haki yao ya msingi ya kusoma.

Kuhusu rushwa ya ngono, alitaka TAKUKURU kuhakikisha inafanya utafiti wa rushwa hiyo hadi kwenye shule za msingi na sekondari.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo, alisema moja ya mikakati ambayo wamejiwekea ni kutekeleza ilani ikiwamo kusimamia mafanikio yao katika kupambana na rushwa.


Ippmedia
 
Kwa nini hizo kesi zisisimamiwe na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Polisi? Takukururu na mimba za utotoni wapi na wapi! By the way, wataweza kweli kufuatilia matukio yote ya wahusika kumalizana juu kwa ju!
 
Kwa nini hizo kesi zisisimamiwe na Ustawi wa Jamii kwa kushirikiana na Polisi? Takukururu na mimba za utotoni wapi na wapi!

Rushwa yenyewe tu imewashinda! Halafu wanajipachika/wanapachikwa majukumu mengine. Hii nchi inafurahisha sana.
Sasahivi kila kitu TAKUKURU, taasisi zinazoongoza kwa rushwa zinajulikana na rushwa ndiyo kwanza inamea
 
Nchi zingine wamewazeje kuishinda hili tatizo? Jibu ni moja tu watoto wakae boarding, bona shule za masister haya mambo hayapo na kama yapo ni machache sana?
Na wasiende likizo kabisa.

Amandla...
 
TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), imeagizwa kushughulikia kesi za mimba za utotoni ambazo zimekuwa zikiishia mitaani badala ya kwenda kwenye vyombo vya sheria.

Vilevile, imeagizwa kufanya utafiti kuhusu rushwa ya ngono kwa vyuo vikuu vingine na vyuo vya kawaida, kama ilivyofanyika kwa vyuo vikuu vya Dodoma (UDOM) na Dar es Salaam (UDSM) ili kutokomeza rushwa hiyo.

Maagizo hayo yalitolewa jana na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utawala Bora na Menejimenti ya Utumishi wa Umma), Deogratius Ndejembi, alipokuwa akifungua Mkutano Mkuu wa TAKUKURU wa kutathmini utendaji kazi kuanzia Julai 2019 hadi Juni 2020.

Alisema amekuwa akishuhudia kesi kama hizo nyingi katika maeneo mbalimbali zikiishia mitaani, na kutaka taasisi hiyo ilivalie njuga suala hilo ili kuwashughulikia wanaofifisha ndoto za watoto.

“Unakuta kesi nyingi za mimba mnazifuatilia ama kuzipeleka mahakamani, lakini ikifikia mahakamani mhusika hatokei au anakana tukio, ukifuatilia unakuta wahusika wamemalizana mtaani kwa kulipana faini, jambo hilo halikubaliki,” alisema Ndejembi.

Aliongeza: “Hii imekuwa ni desturi ya wazazi pale unapowakamata wahusika wao humalizana kesi na watendaji.”

“Unakuta mwalimu amempa mimba mwanafunzi, lakini ukiifuatilia hiyo mwisho wa siku unakuta mtenda kosa yupo mtaani na ukiuliza unaambiwa alimazana na wazazi wa mwanafunzi.

“Ninaomba TAKUKURU mtusaidie kufuatilia suala hili kwa sababu linakuwa sugu na wahusika wanajisikia vibaya kuona watu wanaotenda makosa kama hayo wapo mtaani ilihali wao maisha yao yameharibika,” alisema Ndejembi.

Alisema sheria ipo na hao wazazi wanaofanya vitendo hivyo wawajibishwe kwa mujibu wa sheria za nchi zinavyoelekeza ili hizo mimba za utotoni ziishe.

Alisisitiza wazazi kuhakikisha wanaacha vitendo hivyo kwa kuwa wanakatisha ndoto za watoto wao.

Ndejembi alisisitiza idara ya elimu, halmashauri zihakikishe kesi hizo zinazofanyiwa kazi na mamlaka mbalimbali ili kuhakikisha wanafunzi hao wanapata haki yao ya msingi ya kusoma.

Kuhusu rushwa ya ngono, alitaka TAKUKURU kuhakikisha inafanya utafiti wa rushwa hiyo hadi kwenye shule za msingi na sekondari.

Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Brigedia Jenerali John Mbungo, alisema moja ya mikakati ambayo wamejiwekea ni kutekeleza ilani ikiwamo kusimamia mafanikio yao katika kupambana na rushwa.


Ippmedia
Soma vizuri sheria ya ndoa ya 1971 na ile ya mtoto ya 2009. Utapona zinavyokimzana juu ya tafsir ya mtt
 
Polisi, Victim na Mtuhumiwa wote ni Corrupt tu Happ Police nado Balozi au mshenga wa game hii
 
Utajisikiaje ukiambiwa baba ako kafungwa miaka 30 na mama ako sababu ya wewe kuzaliwa? pia waruhusiwe kurudi shule wanapo jifungua mambo yaende, siamini kama mimba inakatisha ndoto za mtu isipokuwa siyo vizuri kuzaa katika umri mdogo maana wote mtakuwa ni watoto mama na mtoto.
Utafurahi mtoto wako akipewa mimba shuleni?halafu anaonyesha mfano gani kwa wanafunzi wenzake?
 
Back
Top Bottom