Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,108
- 10,191
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), imesema kuwa itafuatilia kwa karibu misaada yote inayotolewa kwa ajili ya kusaidia jitihada za kupamba na corona kuhakikisha hakuna vitendo vya rushwa.
Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Bregedia Jenerali John Mbungo, aliyasea hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake.
Alisema Takukuru inaomba ushirikiano wa wananchi kwa kutoa taarifa mbalimbali zenye viashiria vya rushwa katika maeneo yao katika utoaji wa misaada hiyo.
“Tungependa mtambue kwamba Takukuru iko macho katika kufuatilia matumizi ya misaada mbalimbali inayotolewa na wadau katika kipindi hiki cha janga la corona,” alisema Mbungo
NIPASHE
Mkurugenzi Mkuu wa taasisi hiyo, Bregedia Jenerali John Mbungo, aliyasea hayo jana jijini Dar es Salaam, wakati akizungumza na waandishi wa habari, ofisini kwake.
Alisema Takukuru inaomba ushirikiano wa wananchi kwa kutoa taarifa mbalimbali zenye viashiria vya rushwa katika maeneo yao katika utoaji wa misaada hiyo.
“Tungependa mtambue kwamba Takukuru iko macho katika kufuatilia matumizi ya misaada mbalimbali inayotolewa na wadau katika kipindi hiki cha janga la corona,” alisema Mbungo
NIPASHE