Takwimu: Nini kimeikwamisha Tanzania ya Viwanda?

Takwimu: Nini kimeikwamisha Tanzania ya Viwanda?

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Ni kitu kimoja kizuri kuangalia sekta ya viwanda nchini kwetu sio kwa idadi ya majengo ya viwanda bali uzalishaji ambao unafanyika katika viwanda hivyo.

Uzalishaji unapoongezeka ni wazi tutakuwa tunaweza kuuza nje zaidi, na bidhaa za viwandani zinazouzwa nje katika taarifa za BoT huwa zipo chini ya kiwango cha bidhaa zinzouzwa nje (Manufactured goods).

Katika analysis fupi ya hapa tutaangalia kiwango cha exportation huku tukiangalia pia exportation ya manufactured goods.

Hivyo manufactured goods zinaonesha jinsi uzalishaji wa ndani unavyokuwa. Kwa trends zilivyo kutokana na data zilizopo hali ilikuwa hivi kwa mwaka 2010 hadi 2015, kwamba manufactured goods zilikuwa zinaongezeka, ilishuka kidogo 2011 na tena kidogo 2014.

F588850F-F8D1-441A-997C-3051A7065810.jpeg


Tulipokuja na sera ya viwanda, maana yake kipengele cha manufactured goods kilibidi kitanuke na kukua kwa kasi ili kuweza kuonesha kwamba viwanda tunavyozungumza vimeongeza kwenye uuzaji wa bidhaa nje ya nchi. Kwa data zilizopo unaweza angalia graph hapa chini kwamba kulikuwa na poromoko kubwa la manufacturing goods kwa mwaka 2017 na hapo ikawa imebaki ikiwa hivyo.

Screenshot 2021-02-07 at 18.16.39.png


Ukiweka miaka kumi kwa pamoja yaani mwaka 2010 hadi 2020 unapata picha kama hii kwamba Uzalishaji uliongezeka na inaonekana kama viwanda vilikuwa vinafanya vizuri lakini ghafla vikateremka hadi chini kabisa.

Screenshot 2021-02-07 at 18.16.22.png


Na acknowledge kwamba total exports zimekuwa zikiongezeka kwa kiasi kikubwa, kwa data zilizopo inaonekana mapato ya madini yameongezeka kwa kiasi kikubwa kufanya total Expots kuwa ilivyo. Madini ni kitu muhimu na kwa kweli inaonekana kazi kubwa imefanyika kipande hiko lakini ni muhimu kuangalia uzalishaji ambao ndio unatafsiri viwanda.

8A7FFF3D-769A-4FDB-8FEA-6D46B2E0B8F0.jpeg
 
Viwanda vidogo vidogo vya bidhaa za kilimo. Ndio vinaweza kuwa mkombozi .
Lakini sasa umeme wa kuendesha viwanda hivyo haujawafikia wakulima
 
Back
Top Bottom