Takwimu za athari za mgao wa umeme zikoje?

Pantosha

JF-Expert Member
Joined
Sep 22, 2022
Posts
640
Reaction score
958
Taifa letu limekuwa kwenye changamoto ya kutokuwa na umeme wa uwakika toka enzi na enzi. Serikali imefanya jitihada kubwa kusambaza umeme mijini na vijijini. Tuwapongeze viongozi kwa hilo.

Kutokana na maendeleo ya teknolojia, uchumi, rasilimali tulizonazo, maendeleo haya hayaendani na ukubwa na uchumi wa nchi yetu Tanzania.

Kunapokuwa na janga lolote, kama taifa tunapima/kuangalia athari zake.

Mgao wa umeme ni janga pia. Hivi athari zake ni zipi? Je, wawajibishwe wanaosimamia swala nishati hii?
 
Nikiona posts kuhusu suala la umeme nakereka hadi nahisi kutapika

Week ya pili sasa umeme tunapata kwa masaa manne tu kwa siku tena usiku. Wanarudisha umeme saa nane usiku na kuukata saa kumi na mbili asubuhi. Hii nchi bure kabisa!
 
Apo ungewatag Tanesco
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…