Takwimu za sensa zitaboresha huduma za Afya

Takwimu za sensa zitaboresha huduma za Afya

Rashda Zunde

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2022
Posts
204
Reaction score
231
Mpishi mzuri hupenda kujua idadi ya watu waliopo, ili kupika chakula cha kutosha watu wote, kauli hii inaendana na kila ambacho Serikali inakwenda kufanya katika sensa ya watu na makazi Agosti 23, kwani ili iweze kuhudumia wananchi wake ipasavyo ni muhimu kujua takwimu zilizopo na kuzitoa kulingana na uhitaji uliopo.

Upatinaji wa takwimu hizo utaratibu uandaaji wa sera na mipango ya maendeleo kulingana na uhitaji na mazingira yaliyopo, hivyo sensa ina umuhimu mkubwa katika kuharakisha shughuli za maendeleo . Sensa itafanyika pande zote mbili za Muungano kwa maana ya Tanzania bara na Zanzibar.

Upatikanaji wa takwimu sahihi za sensa utasaidia kufanya tathmini na kufuatilia huduma za afya zitolewazo kwa jamii, hasa kwa kulinganisha idadi ya wananchi waliofikiwa na huduma za afya dhidi ya jumla ya wananchi wa eneo husika.

Wito wanguni kuwa faida nyingi kwa sekta ya afya katika kuboresha huduma z afya nchini zinatokana na takwimu za sensa. Na baadhi ya faida hizo ni katika kufanya mgawanyo sahihi wa wataalamu wa afya, mgawanyo halisia wa fedha kwa ajili ya kutekeleza shughuli mbalimbali za afya, ikiwa ni pamoja na manunuzi ya dawa, ujenzi wa vituo vya afya na upanuzi wa huduma kulingana na kuongezeka kwa idadi ya wananchi katika eneo husika.

Utekelezaji wa haya yote hutegemea sana takwimu za sensa, hivyo ni muhimu kila mwananchi ahamasike kwa kushiriki na kutoa taarifa sahihi bila kuficha kitu katika zoezi la sensa ifikapo Agosti 23, 2022.
 

Attachments

  • download (5).png
    download (5).png
    7.9 KB · Views: 4
"Mpishi mzuri hupenda kujua idadi ya watu waliopo, ili kupika chakula cha kutosha watu wote" hii nimeipenda.
 
Mbona wanajenga dispensaries na vituo vya afya hali kuna magonjwa makubwa kama cancer , Hiv na corona.
 
Sensa itasaidia kivipi kuboresha huduma za jamii.Unataka kumaanisha uchache wa hospitali,wahudumu wa afya,na huduma mbayambaya zitolewazo na serikali zinasababishwa na kutokuwepo sensa?kila sehemu kuna kiongozi na wanajua changamoto za maeneo yao ukianzia mwenyekiti wa mtaa,wakurugenzi,wakuu wa wilaya na mikoa,wote hawa wanajua uduni wa huduma za jamii ,hivyo serikali ingeboresha pasipo kusubili sensa.Faida ya sensa ni moja tu nayo ni kujua idadi ya watu basi.Hizo zingine mnazozitaja hazihitaji uwepo wa sensa kuzijua
 
Sensa itasaidia kivipi kuboresha huduma za jamii.Unataka kumaanisha uchache wa hospitali,wahudumu wa afya,na huduma mbayambaya zitolewazo na serikali zinasababishwa na kutokuwepo sensa?kila sehemu kuna kiongozi na wanajua changamoto za maeneo yao ukianzia mwenyekiti wa mtaa,wakurugenzi,wakuu wa wilaya na mikoa,wote hawa wanajua uduni wa huduma za jamii ,hivyo serikali ingeboresha pasipo kusubili sensa.Faida ya sensa ni moja tu nayo ni kujua idadi ya watu basi.Hizo zingine mnazozitaja hazihitaji uwepo wa sensa kuzijua
Upatikanaji wa takwimu sahihi za sensa utawezesha wizara kujua namna gani yakuelekeza huduma zake katika maeneo husika. Takwimu za sensa zinatoa ramani kwa serikali namna gani inapaswa kupelekea huduma kwenye jamii.
 
Mimi kwangu hakuna atakaayehesabiwa.
Ukikataa kuhesabiwa utakuja kutumia haki ya mtu mwingine kwani sensa inasaidia serikali kujua namna ya kupelekea huduma kwenye jamii kutokana na idadi waliyokuwa nayo.
 
Upatikanaji wa takwimu sahihi za sensa utawezesha wizara kujua namna gani yakuelekeza huduma zake katika maeneo husika. Takwimu za sensa zinatoa ramani kwa serikali namna gani inapaswa kupelekea huduma kwenye jamii.
Bado hujanijibu.kwa upatikanaji wa huduma nchini kwetu ulivyohafifu hauhitaji sensa ili mpeleke huduma.mfano hata muhimbili ambapo tunapategemea lakini wahudimu ni wachache.daktari mmoja anaweza kuhudumia hata watu zaidi ya 200 kwa sku.upande wa barabara,shule nk ni shida tupu tena kwenye majiji kama Dar.sasa serikali inashindwa nini kupeleka hayo mahitaji kwa kuwa yanajulikana na inafahamu na wananchi yanawasibu kilasiku.Faida ya sensa ni moja tu ambayo ni kujua idadi tu y awatu tumefika wangapi.
 
Back
Top Bottom