Talaka au kuachana kunawaathiri zaidi watoto

Talaka au kuachana kunawaathiri zaidi watoto

Mr George Francis

JF-Expert Member
Joined
Jun 27, 2022
Posts
234
Reaction score
376
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.

Sehemu Ya 1

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na changamoto nyingi sana katika ndoa na mahusiano hali inayopelekea ndoa nyingi na mahusiano mengi kuvunjika.

Mbaya zaidi kuvunjika kwa ndoa na mahusiano ambayo teyari kuna watoto ndani yake, wazazi hawaangalii kabisa madhara ambayo yanaweza kuwapata watoto mara baada ya wao kushindwa kuendelea kuishi pamoja.

Lengo kuu la kuanzisha mahusiano au ndoa ni kuishi maisha ya pamoja kama mume na mke katika siku zote za uhai lakini inapotokea imeshindikana kuendelea kuishi pamoja kama kuna watoto ni muhimu kwanza kuagalia ustawi na ukuaji bora wa watoto hao.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba watoto huathirika sana wazazi wanapoachana. Na tukiaangalia ndoa nyingi au mahusiano mengi yanavunjika kwa ugomvi hivyo kupelekea wazazi kushindwa kufikiria kuhusu usalama wa watoto baada ya wao kuachana.

Miongoni mwa athari zinazoweza kuwapata watoto baada ya wazazi kuachana ni kama hizi zifuatazo.

1. Kukosa huduma na mahitaji muhimu ya mtoto. Mfano, chakula, sehemu nzuri ya kulala, mavazi, mahitaji ya shule na afya. Mtoto anakosa huduma hizi kwasababu ya kuvunjika kwa ushirikiano mzuri kati ya baba na mama katika malezi.

2. Mtoto kuwa na mfadhaiko na kupoteza hali ya uchangamfu. Hii inatokana na upweke unaosababishwa na mazoea ya kuwaona wazazi wakiwa pamoja na kuwafurahia.

3. Mtoto kuwa na hasira za marakwamara pamoja na chuki. Hii inatokana na kuathirika kisaikolojia hasa kama ameshuhudia ugomvi wa baba na mama kabla ya kuachana.
MFANO: kama aliona baba akimpiga mama au mama akimfanyia baba ubaya fulani. Hivyo hii kitu inamuingia na kumuathiri mojakwamoja.

4. Kushuka kwa uwezo wao wa kufanya vizuri katika masomo. Hii wakati mwingine kunaweza kumfaya mtoto akaacha hata shule mojakwamoja. Hii inatokana na kukosekana kwa usimamizi mzuri kutoka kwa wazazi wote wawili baada ya kuachana.

5. Watoto kupata hofu na wasiwasi au kujiamini kupitiliza Mtoto aliyelelewa na wazazi wote wawili na yule aliyelelewa na mzazi mmoja wanatofautiana sana kwenye eneo hili.
Hapa kuna mawili; mtoto anaweza kuwa mwoga sana au kama kujiamini basi anjiamini kupitiliza. Vyote hivi vina madhara makubwa linapokuja suala la uhusiano wake na watu wengine. Akiwa na hofu basi ataogopa sana watu na kama akijiamini kupitiliza basi atakuwa na dharau sana kwa watu.

Inaendelea.....

It's me Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
 
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.

Sehemu Ya 2

Matatizo ambayo watoto hupata baada ya wazazi wao kutalikiana yanaendelea kuwaathiri hata wanapokuwa watu wazima.

Hapa tafiti nyingi zinaonesha kuwa kuna uwezekano mkubwa hata wao pia wakashindwa kudumu kwenye ndoa zao au mahusiano yao. Suala la kuacha au kuachika kwao wanaona ni kawaida tu.

Hivyo ushauri ni kwamba wazazi inapofikia point imeshindikana kuendelea kuishi pamoja basi tufikirie namna bora zaidi ya malezi kwa watoto wetu.

WAFILIPI 2:4,5
"Kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo ya wengine.

Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu"

Hivyo tusiangalie masrahi yetu peke yake bali na masrahi ya watoto wetu.

Siku zote ni lazima tukumbuke kuwa mahitaji ya mzazi na mahitaji ya mtoto yanatofautiana. Mzazi anayefukiria kuhusu kuachana na mzazi mwenzake ni kwamba anataka kuanza maisha mapya peke yake au na mtu mwingine.

Lakini kwa kawaida hasingependa maisha yake yabadilike, eti akaishi na baba bila mama au akaishi na mama bila baba. Yeye anapenda aendelee kuishi na wazazi wake wote wawili kwa amani na upendo.

Hata leo ukifanya uchunguzi na kuwauliza watoto waliopitia malezi ya upande mmoja vipi kama walipata furaha baada ya wazazi wao kuachana jibu litakuwa ni 'HAPANA.'

Binafsi nimelelewa na ndugu zangu tangu nikiwa mdogo naelewa jinsi maisha ya kuishi mbali na wazazi wazazi wako iwe wamefariki au wameachana haifurahishi hata kidogo.

Lakini kila kwenye mabaya mengi, mazuri hayakosekani. Kuna uwezekano mdogo sana wa watoto kuwa na furaha baada ya wazazi wao kutalikiana. Inawezekana pia akapata furaha japo hizi ni case chache sana.

Muhimu, kama sio salama kwa maisha yenu na kwa usalama wa watoto wenu basi hapo hakuna namna itabidi wazazi waachane kwa amani ili iwe rahisi kuendelea kushirikiana kwa ukaribu katika malezi ya watoto wao.

Inaendelea....

It's me
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
 
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.

Sehemu Ya 3

Tukiwa tunaelekea mwishoni mwa mada hii napenda tumalizie Kwa kuangalia mambo tunayopaswa kufanya baada ya kuachana au kutalikiana.

Unaweza ukajiuliza kwanini natumia maneno haya kuachana na kutalikiana. Talaka ni Kwa watu walioona na kuachana namaanisha watu walioishi pamoja bila kufunga ndoa.

I think hapo tunaelewana.

Kama ilivyo imani yangu siku zote ni kwamba kuachana sio vita. Hivyo kuachana kwa wazazi hakupaswi kuwa ndio mwisho wa ushirikiano wao katika malezi ya watoto wao.

Hata baada ya kuachana au kutalikiana wazazi wanapaswa kushirikiana katika majukumu ya kuwalea watoto wao kana kwamba bado wanaishi pamoja, japo ni kweli kwamba sio rahisi kama tunavyoweza kutamka.

Sio rahisi kwasababu wazazi walioachana au kutalikiana hawatumii muda wao pamoja. Kila mtu anakuwa na harakati zake.

Na wazazi wengine wanataka kuwashirikisha watoto ugomvi wao. Wanawaeleza watoto wao juu ya ubaya wa baba au juu ya ubaya wa mama. Kosa hili maranyingi linafanywa na wazazi wa kike, yaani kina mama.

Hii inaweza kupelekea mtoto akawa na chuki au dharau dhidi ya mzazi wake mwingine baada ya kulishwa sumu kuhusu madhaifu ya huyo mzazi.

Natoa rai yangu kwa wazazi, tusifanye ujinga huo. Tuwaache watoto wafurahie upendo wa pande zote mbili hata baada ya sisi kuachana au kutalikiana.

Kutalikiana kunaruhusiwa hata katika maandiko matakatifu lakini, tutalikiane kwa sababu za msingi na sio kwasababu ya fashion au kuchokana tu.

Maandiko yaasema...
MATHAYO 19:7,9
"Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini."

Bila shaka, huenda mengi zaidi yakahitajika kuliko kuvumilia tu katika ndoa ambayo haina furaha.

Muhimu tusiwatese watoto hata mara baada ya sisi wazazi kuachana au kutalikiana na maisha yetu yasiwe ya magomvi na uhasama usio na maana yoyote.

Tusiendeane kwa waganga ili kuharibiana maisha wala tusifanyiane visa ili kutuondoa kwenye njia sahihi za mafanikio tena ikiwezekana tusaidiane ili kila mmoja afanikiwe katika maisha yake.

Mafanikio ya wazazi ndio mafanikio ya watoto wetu.

Ahsante kwa kufuatilia mada hii na sina shaka kama utaielewa mada hii basi utaenda kuwa mzazi ambaye ni mfano wa kuigwa katika jamii zetu.

Mungu awabariki sana.

It's me Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Contacts: 0713736006
 
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.

Sehemu Ya 1

Miaka ya hivi karibuni kumekuwa na changamoto nyingi sana katika ndoa na mahusiano hali inayopelekea ndoa nyingi na mahusiano mengi kuvunjika.

Mbaya zaidi kuvunjika kwa ndoa na mahusiano ambayo teyari kuna watoto ndani yake, wazazi hawaangalii kabisa madhara ambayo yanaweza kuwapata watoto mara baada ya wao kushindwa kuendelea kuishi pamoja.

Lengo kuu la kuanzisha mahusiano au ndoa ni kuishi maisha ya pamoja kama mume na mke katika siku zote za uhai lakini inapotokea imeshindikana kuendelea kuishi pamoja kama kuna watoto ni muhimu kwanza kuagalia ustawi na ukuaji bora wa watoto hao.

Tafiti nyingi zinaonesha kwamba watoto huathirika sana wazazi wanapoachana. Na tukiaangalia ndoa nyingi au mahusiano mengi yanavunjika kwa ugomvi hivyo kupelekea wazazi kushindwa kufikiria kuhusu usalama wa watoto baada ya wao kuachana.

Miongoni mwa athari zinazoweza kuwapata watoto baada ya wazazi kuachana ni kama hizi zifuatazo.

1. Kukosa huduma na mahitaji muhimu ya mtoto. Mfano, chakula, sehemu nzuri ya kulala, mavazi, mahitaji ya shule na afya. Mtoto anakosa huduma hizi kwasababu ya kuvunjika kwa ushirikiano mzuri kati ya baba na mama katika malezi.

2. Mtoto kuwa na mfadhaiko na kupoteza hali ya uchangamfu. Hii inatokana na upweke unaosababishwa na mazoea ya kuwaona wazazi wakiwa pamoja na kuwafurahia.

3. Mtoto kuwa na hasira za marakwamara pamoja na chuki. Hii inatokana na kuathirika kisaikolojia hasa kama ameshuhudia ugomvi wa baba na mama kabla ya kuachana.
MFANO: kama aliona baba akimpiga mama au mama akimfanyia baba ubaya fulani. Hivyo hii kitu inamuingia na kumuathiri mojakwamoja.

4. Kushuka kwa uwezo wao wa kufanya vizuri katika masomo. Hii wakati mwingine kunaweza kumfaya mtoto akaacha hata shule mojakwamoja. Hii inatokana na kukosekana kwa usimamizi mzuri kutoka kwa wazazi wote wawili baada ya kuachana.

5. Watoto kupata hofu na wasiwasi au kujiamini kupitiliza Mtoto aliyelelewa na wazazi wote wawili na yule aliyelelewa na mzazi mmoja wanatofautiana sana kwenye eneo hili.
Hapa kuna mawili; mtoto anaweza kuwa mwoga sana au kama kujiamini basi anjiamini kupitiliza. Vyote hivi vina madhara makubwa linapokuja suala la uhusiano wake na watu wengine. Akiwa na hofu basi ataogopa sana watu na kama akijiamini kupitiliza basi atakuwa na dharau sana kwa watu.

Inaendelea.....

It's me Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Wakati mwingine talaka ni Bora zaidi kuliko kubaki kwenye ndoa yenye mateso na iliyokosa amani.


"The worse prison in the world is a home without peace, be very careful who you marry or fall in love with."
Johnny Depp.
 
TALAKA AU KUACHANA KUNAWAATHIRI ZAIDI WATOTO.

Sehemu Ya 3

Tukiwa tunaelekea mwishoni mwa mada hii napenda tumalizie Kwa kuangalia mambo tunayopaswa kufanya baada ya kuachana au kutalikiana.

Unaweza ukajiuliza kwanini natumia maneno haya kuachana na kutalikiana. Talaka ni Kwa watu walioona na kuachana namaanisha watu walioishi pamoja bila kufunga ndoa.

I think hapo tunaelewana.

Kama ilivyo imani yangu siku zote ni kwamba kuachana sio vita. Hivyo kuachana kwa wazazi hakupaswi kuwa ndio mwisho wa ushirikiano wao katika malezi ya watoto wao.

Hata baada ya kuachana au kutalikiana wazazi wanapaswa kushirikiana katika majukumu ya kuwalea watoto wao kana kwamba bado wanaishi pamoja, japo ni kweli kwamba sio rahisi kama tunavyoweza kutamka.

Sio rahisi kwasababu wazazi walioachana au kutalikiana hawatumii muda wao pamoja. Kila mtu anakuwa na harakati zake.

Na wazazi wengine wanataka kuwashirikisha watoto ugomvi wao. Wanawaeleza watoto wao juu ya ubaya wa baba au juu ya ubaya wa mama. Kosa hili maranyingi linafanywa na wazazi wa kike, yaani kina mama.

Hii inaweza kupelekea mtoto akawa na chuki au dharau dhidi ya mzazi wake mwingine baada ya kulishwa sumu kuhusu madhaifu ya huyo mzazi.

Natoa rai yangu kwa wazazi, tusifanye ujinga huo. Tuwaache watoto wafurahie upendo wa pande zote mbili hata baada ya sisi kuachana au kutalikiana.

Kutalikiana kunaruhusiwa hata katika maandiko matakatifu lakini, tutalikiane kwa sababu za msingi na sio kwasababu ya fashion au kuchokana tu.

Maandiko yaasema...
MATHAYO 19:7,9
"Wakamwambia, Jinsi gani basi Musa aliamuru kumpa hati ya talaka, na kumwacha?

Nami nawaambia ninyi, Kila mtu atakayemwacha mkewe, isipokuwa ni kwa sababu ya uasherati, akaoa mwingine, azini; naye amwoaye yule aliyeachwa azini."

Bila shaka, huenda mengi zaidi yakahitajika kuliko kuvumilia tu katika ndoa ambayo haina furaha.

Muhimu tusiwatese watoto hata mara baada ya sisi wazazi kuachana au kutalikiana na maisha yetu yasiwe ya magomvi na uhasama usio na maana yoyote.

Tusiendeane kwa waganga ili kuharibiana maisha wala tusifanyiane visa ili kutuondoa kwenye njia sahihi za mafanikio tena ikiwezekana tusaidiane ili kila mmoja afanikiwe katika maisha yake.

Mafanikio ya wazazi ndio mafanikio ya watoto wetu.

Ahsante kwa kufuatilia mada hii na sina shaka kama utaielewa mada hii basi utaenda kuwa mzazi ambaye ni mfano wa kuigwa katika jamii zetu.

Mungu awabariki sana.

It's me Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Contacts: 0713736006
Ubinafsi ndiyo unaleta matatizo yote haya. Pili umri wa kupata mtoto nao unachangia
 
Pia Kuna tafiti zinaonyesha, muathirika mkubwa wa talaka:
1.mwanamke
2.watoto
3.Mwanaume
 
A loveless marriage is more damaging than divorce
Mwishoni mwa sehemu ya pili na sehemu ya tatu ya chapisho hili nimeunga mkono pia kuhusu kuachana. Lakini mara baada ya kuachana watoto wasikose haki zao za msingi kama zile ambazo wangezipata wakiwa chini ya wazazi wote wawili.
 
Wakati mwingine talaka ni Bora zaidi kuliko kubaki kwenye ndoa yenye mateso na iliyokosa amani.


"The worse prison in the world is a home without peace, be very careful who you marry or fall in love with."
Johnny Depp.
Mwishoni mwa sehemu ya pili na sehemu ya tatu ya chapisho hili nimeunga mkono pia kuhusu kuachana. Lakini mara baada ya kuachana watoto wasikose haki zao za msingi kama zile ambazo wangezipata wakiwa chini ya wazazi wote wawili.
 
Wakati mwingine talaka ni Bora zaidi kuliko kubaki kwenye ndoa yenye mateso na iliyokosa amani.


"The worse prison in the world is a home without peace, be very careful who you marry or fall in love with."
Johnny Depp.
Hapo kuna kuwa kumeshatafutwa njia za kusuluisha ikashindika ndio iende kwenye talaka, sisi tulio lelewa kwenye talaka tunayajua madhara yake yasikie tu kwa mbali.
 
Mwishoni mwa sehemu ya pili na sehemu ya tatu ya chapisho hili nimeunga mkono pia kuhusu kuachana. Lakini mara baada ya kuachana watoto wasikose haki zao za msingi kama zile ambazo wangezipata wakiwa chini ya wazazi wote wawili.
Mtoto hawezi kupata haki za msingi katika talaka. Talaka ina pande mbili, uliofurahi na uliosononeka. Hakuna talaka ambayo itakuwa na upande mmoja tu. Anayeumia ni mtoto aidha moja kwa moja au mzazi mmoja kupitia kwa mtoto ili amuumize mwenza.

Kumbuka kama upande unaosononeka ni mwanamke, hakuna rangi Mwanaume utakosa kuiona.
 
Back
Top Bottom