Talaka zinazotolewa nje ya Mahakama hazitambuliki kisheria

Talaka zinazotolewa nje ya Mahakama hazitambuliki kisheria

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Joined
Aug 7, 2018
Posts
685
Reaction score
1,124
IMG_20210322_104437_180.jpg

Talaka ni Amri ya Mahakama ya kuvunja Ndoa. Chombo pekee chenye mamlaka ya kuvunja Ndoa ni Mahakama. Ni lazima talaka itolewe Mahakamani ili kila Mwanandoa haki yake itamkwe bayana.

Talaka za mtaani ama nje ya Mahakama, kwa maandishi au kwa mdomo hazitambuliki Kisheria.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 100 cha Sheria ya Ndoa, Mahakama haiwezi kusikiliza shauri la talaka kama Ndoa haijadumu kwa miaka 2.

Endapo Mwanandoa mmoja atakuwa amekumbana na matatizo yasiyovumilika na Ndoa haijafikisha miaka miwili, Mahakama haina budi kutoa idhini ya kusikiliza shauri hilo.

Kwa mujibu wa Vifungu vya 99 na 107(1) vya Sheria ya Ndoa, Mahakama hutoa talaka pale tu itakapojiridhisha kuwa Ndoa hiyo haiwezi kurekebishika kutokana na sababu zisizovumilika.
 
Upvote 0
Ndio maana waislamu walitaka mahakama ya kadhi ili iwasimamie katika mambo kama haya, kwani kwenye uislamu talaka ni jambo zito sana sio la mchezomchezo
 
Talaka ni Amri ya Mahakama ya kuvunja Ndoa. Chombo pekee chenye mamlaka ya kuvunja Ndoa ni Mahakama. Ni lazima talaka itolewe Mahakamani ili kila Mwanandoa haki yake itamkwe bayana.

Talaka za mtaani ama nje ya Mahakama, kwa maandishi au kwa mdomo hazitambuliki Kisheria.

Kwa mujibu wa Kifungu cha 100 cha Sheria ya Ndoa, Mahakama haiwezi kusikiliza shauri la talaka kama Ndoa haijadumu kwa miaka 2.

Endapo Mwanandoa mmoja atakuwa amekumbana na matatizo yasiyovumilika na Ndoa haijafikisha miaka miwili, Mahakama haina budi kutoa idhini ya kusikiliza shauri hilo.

Kwa mujibu wa Vifungu vya 99 na 107(1) vya Sheria ya Ndoa, Mahakama hutoa talaka pale tu itakapojiridhisha kuwa Ndoa hiyo haiwezi kurekebishika kutokana na sababu zisizovumilika.View attachment 1731506
Haya mambo yataleta mtafaruku sana kwa sisi waislamu, Talaka katika uislamu imetajwa kwa katika kitabu kitakatifu Qur-an na ndio muongozo kwa waislamu hatuhitaji tena kufafanuliwa na Mahakama hizi za kitwaghuuti ambazo zimeanzishwa na mwanadamu ambazo actually zinaenda nje ya muongozo ulipo katika kitabu Kitukufu Qur-an, hilo sharti la kudumu ndoa kwa miaka miwili ndio uweze kuacha ni nosense., Tunakoelekea ni kubaya.

Wenzetu hufika Beijing kudai haki zao kwa sababu dini zao na vitabu vya vimekaa kimya lakini sisi waislamu muongozo wa maisha yetu na kila kitu kipo katika kitabu kitakatifu Qur-an na Khadithi za Mtume wetu Muhammad S.A.W. hatuhitaji mashauri ya mahakamani ambayo yataenda kinyume na Qur-an.
 
Haya mambo yataleta mtafaruku sana kwa sisi waislamu, Talaka katika uislamu imetajwa kwa katika kitabu kitakatifu Qur-an na ndio muongozo kwa waislamu hatuhitaji tena kufafanuliwa na Mahakama hizi za kitwaghuuti ambazo zimeanzishwa na mwanadamu ambazo actually zinaenda nje ya muongozo ulipo katika kitabu Kitukufu Qur-an, hilo sharti la kudumu ndoa kwa miaka miwili ndio uweze kuacha ni nosense., Tunakoelekea ni kubaya.

Wenzetu hufika Beijing kudai haki zao kwa sababu dini zao na vitabu vya vimekaa kimya lakini sisi waislamu muongozo wa maisha yetu na kila kitu kipo katika kitabu kitakatifu Qur-an na Khadithi za Mtume wetu Muhammad S.A.W. hatuhitaji mashauri ya mahakamani ambayo yataenda kinyume na Qur-an.

Hii habari haihusiani na Waisilamu hata kidogo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom