TALGWU: Kikokotoo ni fumbo, uzima ni majaaliwa. Tupewe hela zetu zote tukafie mbele

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Heri ya siku ya wafanyakazi, huku kusini mwa nchi imepambwa na mabango lukuki ila moja limenivutia. Waajiriwa wanataka fao lao lote wakafanye maisha mengine na si mafungu kama Serikali wanavyoona.

Kwanini mtu pesa yake ameiifadhi maisha yake yote ya kufanya kazi halafu siku ya kuipata mnaanza kumpangia matumizi tena mtu mzima aliyekula chumvi nyingi na kuyaona yote ya hii dunia.

Serikali kama ilifanya makosa kutumia pesa zao ikakope kule ambapo huwa inakopa, hela wanazopata badala ya kununulia magari na posho zisizo na idadi wawalipe wazee waliotumikia nchi hii kwa jasho na damu.

Hivi hamna sehemu duniani hii mifuko ni hiari kuchangia?

 
Bango la UKOMBOZI
 
NENDENI MKAFE TU Kama Mwendazake itakuwa nyinyi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…