floow
JF-Expert Member
- Mar 20, 2017
- 411
- 855
Mbosso ni msanii mpya chini ya uongozi wa WCB. Kabla ya kusajiliwa WCB, Mbosso alikuwa Msanii wa Yamoto band..
Mbosso ameonyesha tamaa ya pesa baada ya kutoa nyimbo yake ya kwanza WATAKUBALI ambayo mpaka sasa imetazamwa na zaidi ya watu milioni 2..
Baada ya kuachia video ya wimbo wa "WATAKUBALI", Mbosso ameonekana akifanya media tour mbalimbali ndani na nje ya nchi, jambo ambalo lengo lake ni kukuza mziki wake zaidi.
Kosa analolifanya Mbosso ni kupost mfululizo wa matukio yake ambayo si nyimbo wala vidio ya nyimbo. Amekuwa akifanya hivyo mara nyingi kupitia mtandao wa YouTube lengo lake yeye apige ndege wawili kwa wakati mmoja; yaani alipwe kupitia nyimbo zake na pia alipwe kupitia media anazozifanya; jambo ambalo si zuri kwa mwanamuziki.
Kwa kufanya hivyo kumesababisha watu kuizoea na kuanza kuipuuzia account ya YouTube ya Mbosso, hali iliyosababisha Mbosso kushindwa kufika views 1mil kwa wakati.. Ikumbukwe views milioni 1 ni kitu rahisi kwa wasanii wa WCB!
Kijana inabidi abadilike..