Tamaduni na mila za Makabila mbalimbali Tanzania: Utamaduni gani kwenye kabila lako unaona ni wa ajabu na haufanyiki sehemu nyingine?

Tamaduni na mila za Makabila mbalimbali Tanzania: Utamaduni gani kwenye kabila lako unaona ni wa ajabu na haufanyiki sehemu nyingine?

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu Jmosi inaendaje?

Tanzania tumebarikiwa kuwa na makabila mengi yenye tamaduni mbalimbali ambazo kiasi chake zinaanza kupotea kutokana na miingiliano na wageni pamoja na sababu nyinginkede kede.

Mimi ni katika wale tumekulia mjini, tunaokoteza huku na huko na kujifunza kila siku kutokana na watu tunaochangamana nao.

Wale mmekulia vijijini na hata mjini lakini bado mnapractice utamaduni wenu njooni mfunguke, ili gen Z na sisi wa mjini tupate somo.

Utamaduni/mila gani kwenye kabila lako unaona ni wa ajabu kabisa?

- Utamaduni/mila gani unaona ni nzuri wengine tunapaswa kujifunza kutoka kwenu?

- Utamaduni/mila gani ni mbaya, inadhililisha kundi fulani inapaswa kuachwa?

- Utamaduni/mila gani inafanya kabila lenu kuwa la pekee?

Mkaribie kwenye uzi Wakuu, niko tayari kuchukua notes🌚.
 
Back
Top Bottom