Tamasha la Franco Luambo Luanzo Makiadi Grand Master( Grande Maitre) Dar es Salaam- Early 1970's

Tamasha la Franco Luambo Luanzo Makiadi Grand Master( Grande Maitre) Dar es Salaam- Early 1970's

Mgibeon

JF-Expert Member
Joined
Aug 7, 2011
Posts
11,308
Reaction score
21,507
Moja ya matukio makubwa na ya pekee yalopata kutokea uwanja wa uhuru ambao enzi hizo uliitwa uwanja wa taifa Ni s tamasha la hayati Franco, mwamba wa muziki wa rhumba, katika tamasha hilo watu walikanyagana katika harakati za kuingia uwanjani na Kuna mtu alipoteza Maisha papo hapo.

Kwenye safari hiyo Franco alikuja na ndege iliyojaa vifaa na vyombo vya muziki ambavyo vilitumia kiwango kikubwa cha umeme na ilibidi baadhi ya maeneo ya mji yazimwe umeme, ili kukidhi mahitaji ya umeme ktk tamasha hilo. Maneno hayo yalithibitishwa na mkongwe Lutumba Simaro Masiya ambaye alikuwa miongoni mwa nguzo za bendi TP OK JAZZ. Mpiga solo wa JUWATA(Msondo kwa Sasa) , Saidi Mabela alikuwepo uwanjani ili kuona uhodari wa Franco kwenye solo.

Inawezekana hii ni miongoni mwa matamasha Makubwa yaliyowahi kufanyika ktk Uwanja wa taifa(Uhuru Stadium).

R.I.P Franco..
 
Mkuu nasikia aliwahi kuwa wazir wa utamadun enz za mobutu ssesseko Ni kweli?



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Mkuu, rekodi Kama hiyo haijafika mezani kwangu bado, ila ninachojua ni kwamba Mobutu alimfunga Franco, na Akiwa gerezani alitunga wimbo unaoitwa Mokolo Tonga! Kilichofanya afungwe jela ni wimbo unaoitwa "Jackie"ambapo anamsifia Mwanamke, kingine ni tabia ya ushindani Kati yake Mhe. Rais, aliwahi kununua kitambaa kinachofanana na suti ya Rais halafu akakifanya kua mapazia nyumba nzima.

Na Mobutu alipoona kwamba kumfunga jela hakujamnyamazisha Franco akaamua kumtoa jela ili amtumie ktk kampeni za uchaguzi 1984, Franco akatunga wimbo unaoitwa "candidat na biso" maana yake "Mgombea wetu"
 
Mkuu, rekodi Kama hiyo haijafika mezani kwangu bado, ila ninachojua ni kwamba Mobutu alimfunga Franco, na Akiwa gerezani alitunga wimbo unaoitwa Mokolo Tonga! Kilichofanya afungwe jela ni wimbo unaoitwa "Jackie"ambapo anamsifia Mwanamke, kingine ni tabia ya ushindani Kati yake Mhe. Rais, aliwahi kununua kitambaa kinachofanana na suti ya Rais halafu akakifanya kua mapazia nyumba nzima.

Na Mobutu alipoona kwamba kumfunga jela hakujamnyamazisha Franco akaamua kumtoa jela ili amtumie ktk kampeni za uchaguzi 1984, Franco akatunga wimbo unaoitwa "candidat na biso" maana yake "Mgombea wetu"
Hahahahahaa!jamani

Sent from my Infinix X559C using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, rekodi Kama hiyo haijafika mezani kwangu bado, ila ninachojua ni kwamba Mobutu alimfunga Franco, na Akiwa gerezani alitunga wimbo unaoitwa Mokolo Tonga! Kilichofanya afungwe jela ni wimbo unaoitwa "Jackie"ambapo anamsifia Mwanamke, kingine ni tabia ya ushindani Kati yake Mhe. Rais, aliwahi kununua kitambaa kinachofanana na suti ya Rais halafu akakifanya kua mapazia nyumba nzima.

Na Mobutu alipoona kwamba kumfunga jela hakujamnyamazisha Franco akaamua kumtoa jela ili amtumie ktk kampeni za uchaguzi 1984, Franco akatunga wimbo unaoitwa "candidat na biso" maana yake "Mgombea wetu"
Nashukuru mkuu wimbo wa candidat aka le maleshale prezidaa wimbo mzuri Sana NABISO NABISO

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mkuu nasikia aliwahi kuwa wazir wa utamadun enz za mobutu ssesseko Ni kweli?



Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Hapana,alikuwa tu ni mpiga kampeni kama Diamond kwa Jiwe, na Mobutu alimpa state sponsorship Franco na bendi zingine kubwa, pia walikuwa ni marafiki na mara nyingi Mobutu alitembea na bahasha za khaki zimejaa fedha aligawa kwa watu ikiwemo franco
Kwa kifupi franco alikuwa tajiri
 
Ni kweli kabisa, nilimsikia marehemu simaro lutumba a.k.a Masiya akisema hii
 
Hapana,alikuwa tu ni mpiga kampeni kama Diamond kwa Jiwe, na Mobutu alimpa state sponsorship Franco na bendi zingine kubwa, pia walikuwa ni marafiki na mara nyingi Mobutu alitembea na bahasha za khaki zimejaa fedha aligawa kwa watu ikiwemo franco
Kwa kifupi franco alikuwa tajiri
Kwa hyo alikuwa CHAWA PRO MAX watoto wa sikuhiz wanaita

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Wakuu shusheni nondo za kale.
Mkuu Mgibeon wewe enzi hizo ulikuwepo?
Mkuu Mimi wakati Franco anafariki nilikua ningali mvulana tu, ila Baba yangu alimpenda sana Franco pamoja na Madilu.. So wakati nakua nimekua huku nikisikia nyimbo za hao watu wakaniingia ktk damu, ila baadae nikaja nikasoma na kufuatilia..... Mitandao inamambo mengi mazuri ya kujifunza!
 
Back
Top Bottom