Sasa wewe jifanye unampenda sana ukaanza kumsomesha,kabla hujachukua maamuzi tambua kwamba mwanamke hasomeshwi
Hawana wema hawa viumbe,unaweza kumsomesha mpaka masters halafu ukaambulia kupewa kadi ya harusi
Mpende mwanamke wako ila mwambie jukumu la kusoma ni la wazazi wake na yeye mwenyewe,mwambie ukweli tu kuwa hutahusika kwa namna yoyote ile..
Nimetoa onyo hivyo sitegemei miaka mitatu badae huko zikaja threads humu za kuomba ushauri baada ya kuachwa na waliowasomesha.Kwa wale mlianza malizieni tu kuwasomesha ili muwe case studies humu JF