TAMISEMI fuatilieni Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhusu ajira mpya za Waalimu kuna urasimu mkubwa

TAMISEMI fuatilieni Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuhusu ajira mpya za Waalimu kuna urasimu mkubwa

langaji

Member
Joined
Aug 9, 2013
Posts
45
Reaction score
39
Sote tunafahamu kwamba Katibu Mkuu wa TAMISEMI alitangaza majina ya waalimu wapya mwishoni mwa mwezi Novemba mwaka huu. Akatoa maelekezo kwa waajiriwa wapya kwenda kuripoti kwenye Halmashauri walizopangiwa kuanzia tarehe 1 hadi 14 Desemba.

Katibu Mkuu huyu alikwenda mbali zaidi na kuwaelekeza Wakurugenzi wa mamlaka ya Serikali za Mitaa kusimamia kwa karibu suala la kukamilisha taratibu za ajira mapema iwezekanavyo ili waajiriwa hao waingizwe kwenye orodha ya malipo yaani payroll ili kuondoa suala la malimbikizo ya mishahara isiyokuwa na ulazima.

Lakini hayo maagizo hayakutekelezwa ipasavyo kwenye baadhi ya Halmashauri hapa nchini.

1. Wakurugenzi hawajaandikia waajiriwa mpya barua za posting

2. Wakurugenzi hawajawapa waajiriwa fomu za kudai fedha za kujikimu

3. Wakurugenzi hawa wamewaachia Maafisa Utumishi na Utawala kazi ya kusimamia zoezi la ajira ya walimu wapya, Jambo ambalo ni sahihi. Lakini hawasimamii ipasavyo zoezi hilo. Hali hii imesababisha urasimu mkubwa sana.

Yaani wamebakia tu kupokea waajiriwa na kuwapa fomu za ajira. Zaidi ya yote wanadai kuwa hawataweza kuwapa barua za posting, fedha za kujikimu na mishahara ya mwezi disemba.

Kisingizio chao kikubwa ni kwamba wanasubiria uhakiki wa NECTA ukamilike ndo waendelee na taratibu zingine.

Inawezekana sababu zao ni sahihi ila sasa inaweza kuendelea kuleta urasimu mkubwa hata kipindi cha mwezi Januari 2021, walimu hawa wapya wakashindwa kuanza maisha vizuri hali ambayo inaweza kusababisha ufanisi mdogo wa kazi kwa hawa waajiriwa wapya.

Asanteni, naomba kuwasilisha.
 
Hizi report ndio unaleta leo !?? Kwani ume report lini mkuu ?

Pesa ya kujikimu ina sintofahamu Tanzania nzima. Ila ninavyo jua mimi ukireport chini ya tarehe 14 ambao ndio ilikuwa deadline basi unastaili kulipwa mshahara wa December, na kama umechelewa kureport basi huwezi kupata mshahara hivyo utawadai salary arrears.

Hilo la kuhakiki vyeti ndio kwanza nalisikia kutoka kwako ni geni kwangu pia.
 
Binafsi niliripoti tangu 3rd December lakini hakuna linaloendelea. Wanadai wametuma Vyeti vyetu Necta ili vihakikiwe kwanza. Yaani kila kitu Afisa utumishi anadai kuwa hadi Uhakiki ujibiwe na Necta
Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na subra.
 
Asante
Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na su
Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na subra.
Asante mkuu kwa ushauri mzuri
 
Binafsi niliripoti tangu 3rd December lakini hakuna linaloendelea. Wanadai wametuma Vyeti vyetu Necta ili vihakikiwe kwanza. Yaani kila kitu Afisa utumishi anadai kuwa hadi Uhakiki ujibiwe na Necta
Kwahiyo wewe unataka Ulipwe pesa ya Walalahoi wakati hata haijathibitika kwamba una Vyeti halali?? Endapo umelipwa na ikaja kuthibitika kwamba vyeti vyako feki unajua unajua huyo aliyeidhinisha malipo yako atakuwa kitanzini.
Heshimu Sheria na Taratibu za Kiutumishi utakuja kunishukuru ukiwa Senior.
LKN mdogo wangu, Umeweza kuishi Mtaani bila Ajira tangu 2016 au 2017 unaona shida gani kuvumilia Desemba ipite ili Januari ufurahie Maisha mpaka utakapotimiza miaka 60. Tuache kulalamika kila Wakati mnachafua Taswirra nzuri ya Kada ya Ualimu.
 
Basi una mshahara wa December na wasipokulipa maana yake utawadai haina shida.

Possibly kilichosababisha pesa za kujikimu zichelewe basi ni hilo swala la uhakiki kutoka necta, kuweni na subra.
Ila Necta sasa wanatakiwa kuboresha mfumo wa uhakiki wa vyeti. Ni vyema coordination ikafanyika ili uhakiki ufanyike electronically kama vile NIDA. Mwajiri akiingiza tu namba ya cheti, system inatakiwa kutoa majibu on the spot ili kuondoa huu usumbufu
 
Nimekuelewa vizuri ushauri wako. Ila naona umetoa ushauri general mno. Mawazo mazuri ila kwa hapa lengo langu siyo kushindwa kusubiri bali mchakato huu hauko clear kama ilivyotakiwa. Sasa kulikuwa na haja gani ya kuripoti mapema wakati uwezeshwaji unachukua muda mrefu. Necta pia hawako on time kuhakikisha zoezi linakuwa safe kwa waajiri
Kwahiyo wewe unataka Ulipwe pesa ya Walalahoi wakati hata haijathibitika kwamba una Vyeti halali?? Endapo umelipwa na ikaja kuthibitika kwamba vyeti vyako feki unajua unajua huyo aliyeidhinisha malipo yako atakuwa kitanzini.
Heshimu Sheria na Taratibu za Kiutumishi utakuja kunishukuru ukiwa Senior.
LKN mdogo wangu, Umeweza kuishi Mtaani bila Ajira tangu 2016 au 2017 unaona shida gani kuvumilia Desemba ipite ili Januari ufurahie Maisha mpaka utakapotimiza miaka 60. Tuache kulalamika kila Wakati mnachafua Taswirra nzuri ya Kada ya Ualimu.
 
Bila kukomaa hiyo hela ya kujikimu hamtaipata na mbaya zaidi mmeingia shule zimefungwa mitihani mmeshasahihisha na kupanga matokeo sasa hakuna effect kwa idara ya elimu hata mkigoma.
Mimi nakumbuka tulipata post wakati masomo yanaendelea na kukuta hali ni mbaya hakuna waalim wa sayansi. Yaaan tukakinukusha tulipewa hela fasta za kujikimu halmashauri yetu ila mshahara ulichelewa mwezi mmoja.
Ila tulisain 716,000 mshahara wa degree ila awamu hiibwa degree wamesaini 756,000.
Sijaelewa hapo inakuwaje mbona magepu hayaaa
 
Dah mazingira hayo ya kukaa guest niliwahi kuyapitia japo nashukuru mwisho wa mwezi tulilipwa mshahara bila shaka wao pia watalipwa kikubwa wawe na subra.
 
Bila kukomaa hiyo hela ya kujikimu hamtaipata na mbaya zaidi mmeingia shule zimefungwa mitihani mmeshasahihisha na kupanga matokeo sasa hakuna effect kwa idara ya elimu hata mkigoma.
Mimi nakumbuka tulipata post wakati masomo yanaendelea na kukuta hali ni mbaya hakuna waalim wa sayansi. Yaaan tukakinukusha tulipewa hela fasta za kujikimu halmashauri yetu ila mshahara ulichelewa mwezi mmoja.
Ila tulisain 716,000 mshahara wa degree ila awamu hiibwa degree wamesaini 756,000.
Sijaelewa hapo inakuwaje mbona magepu hayaaa
Kuna sintofahamu nyingi. Ila binafsi nilisaini 716,000 kama kawa. Sasa hapo sijui. Mimi nipo tayari kukinukisha, tatizo wenzangu wengi ni waoga. Siku hizi nimeanza kurudi nyuma kwa sababu ya kuhofia kuwa chambo na kujitengenezea maadui kwa faida ya wengi
 
Dah mazingira hayo ya kukaa guest niliwahi kuyapitia japo nashukuru mwisho wa mwezi tulilipwa mshahara bila shaka wao pia watalipwa kikubwa wawe na subra.
Wanazingua mno hawa wakurugenzi wetu yaani. Kuwa na subira ni hadi nikipewa allowance ili niweze kuanza maisha. Tunafahamu kuwa shule hazina nyumba za walimu, hivyo ni lazima ulipie pango kuanzia miezi mitatu na kuendelea, malazi na chakula. Wao wanakula kuku bila kufikiria hatima ya walalahoi!
 
Hao walimu wapya itabidi wawe wavumilivu, vinginevyo miongoni mwao wataikimbia ajira hiyo mapema kwa njaa ukichukulia wengine tayari walikuwa wana miradi iliyokuwa inawapa kipato mpaka wakaanzisha familia.Sasa kama kuna suala la uhakiki wa NECTA lipo mpaka hilo zoezi likamilike litachukua muda mrefu,na huu utakuwa ni usumbufu,iweje wawapangie vituo bila kujiridhisha wakati TAMISEMI na NECTA ni taasisi za serikali? TAMISEMI ilitakiwa kwanza ipate taarifa za NECTA kama taarifa za hao waajiriwa ni sahihi ndiyo wapangiwe halmashauri za kwenda kuripoti na pia mafungu ya fedha za kujikimu yapo wakati wakisubiri majina yaingizwe kwenye payroll.Barua ya ajira hufuata na hatimaye barua ya kuthibitishwa kazini kazini huja.Hao walimu wavumilie kuna taratibu za ajira zitachukua muda kukamilika
 
Hao walimu wapya itabidi wawe wavumilivu, vinginevyo miongoni mwao wataikimbia ajira hiyo mapema kwa njaa ukichukulia wengine tayari walikuwa wana miradi iliyokuwa inawapa kipato mpaka wakaanzisha familia.Sasa kama kuna suala la uhakiki wa NECTA lipo mpaka hilo zoezi likamilike litachukua muda mrefu,na huu utakuwa ni usumbufu,iweje wawapangie vituo bila kujiridhisha wakati TAMISEMI na NECTA ni taasisi za serikali? TAMISEMI ilitakiwa kwanza ipate taarifa za NECTA kama taarifa za hao waajiriwa ni sahihi ndiyo wapangiwe halmashauri za kwenda kuripoti na pia mafungu ya fedha za kujikimu yapo wakati wakisubiri majina yaingizwe kwenye payroll.Barua ya ajira hufuata na hatimaye barua ya kuthibitishwa kazini kazini huja.Hao walimu wavumilie kuna taratibu za ajira zitachukua muda kukamilika
 
Nimekumbuka mbali sanaa jinsi nilivyofanyiwa kwenye ajira yangu na serikali, barua ya kazi na kupangiwa kituo nimepewa, nimeacha kazi yangu nimeripoti kituoni nimekaa mwezi kwenye kituo cha kazi baadae naambiwa ajira zetu zimefutwa hili sitalisahau na Mungu ni Mwema kila wakati
 
Kwahiyo wewe unataka Ulipwe pesa ya Walalahoi wakati hata haijathibitika kwamba una Vyeti halali?? Endapo umelipwa na ikaja kuthibitika kwamba vyeti vyako feki unajua unajua huyo aliyeidhinisha malipo yako atakuwa kitanzini.
Heshimu Sheria na Taratibu za Kiutumishi utakuja kunishukuru ukiwa Senior.
LKN mdogo wangu, Umeweza kuishi Mtaani bila Ajira tangu 2016 au 2017 unaona shida gani kuvumilia Desemba ipite ili Januari ufurahie Maisha mpaka utakapotimiza miaka 60. Tuache kulalamika kila Wakati mnachafua Taswirra nzuri ya Kada ya Ualimu.
Narudia tena,kupata hizi ajira wafunge maombi na kumshukuru mungu kuliko kupita huku mkilalamika hovyo. Period
 
Back
Top Bottom