Chama cha Mapinduzi (CCM) na Serikali yake wamekuwa na utaratibu wa kutengeneza tatizo na kulitatua wao wenyewe ili waonekane wema kwa Wananchi na tasisi za ndani na nje ya nchi
Pia soma
Kitendo cha Katibu mkuu wa CCM Dr. Emmanuel Nchimbi leo kukutana na waandishi wa habari ofisi ndogo Lumumba jijini Darisalama na kusema kwa niaba ya mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni rais wa nchi kuomba waziri wa Tamisemi kupuuzia makosa madomdogo yaliyojitokeza kwa wagombea wa nafasi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni usanii mtupu
Cha kushangaza wizara ya Tamisemi iko chini ya rais maamuzi ya wizara hiyo kukata majina ya wagombea ni maamuzi ya ofisi yake angeweza kupiga simu tu kwa waziri au kumuita ofisini kwake kumuamuru kuacha uhuni huo mara moja
Kitendo cha Mwenyekiti wa chama kinachoongoza nchi na rais mwenye ofisi yake ya Tamisemi ndio imekata majina ya wagombea leo hii kuomba wasifanye hivyo ni jambo linalofikilisha kwa watu wazima wenye akili zao
Huko kunaitwa ni kutengeneza tatizo halafu unalitatua mwenyewe sawa sawa na baba ndani ya nyumba anaanzisha utata kwa mkewe na watoto wake kisha anautatu baadaye wanamsifu mshua ana akili nyingi sana huyu na huruma kwa familia yake
CCM Comasava
Pia soma
- CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa
- LGE2024 - Tamisemi iko ofisi ya Rais. Kikatiba Rais ndiye Waziri wa Tamisemi. Mchengerwa hastahili lawama
Kitendo cha Katibu mkuu wa CCM Dr. Emmanuel Nchimbi leo kukutana na waandishi wa habari ofisi ndogo Lumumba jijini Darisalama na kusema kwa niaba ya mwenyekiti wa chama hicho ambaye pia ni rais wa nchi kuomba waziri wa Tamisemi kupuuzia makosa madomdogo yaliyojitokeza kwa wagombea wa nafasi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ni usanii mtupu
Cha kushangaza wizara ya Tamisemi iko chini ya rais maamuzi ya wizara hiyo kukata majina ya wagombea ni maamuzi ya ofisi yake angeweza kupiga simu tu kwa waziri au kumuita ofisini kwake kumuamuru kuacha uhuni huo mara moja
Kitendo cha Mwenyekiti wa chama kinachoongoza nchi na rais mwenye ofisi yake ya Tamisemi ndio imekata majina ya wagombea leo hii kuomba wasifanye hivyo ni jambo linalofikilisha kwa watu wazima wenye akili zao
Huko kunaitwa ni kutengeneza tatizo halafu unalitatua mwenyewe sawa sawa na baba ndani ya nyumba anaanzisha utata kwa mkewe na watoto wake kisha anautatu baadaye wanamsifu mshua ana akili nyingi sana huyu na huruma kwa familia yake
CCM Comasava