DOKEZO TAMISEMI ingilieni kati sakata la walimu kutapeliwa na Afisa Elimu wao huko Katavi

DOKEZO TAMISEMI ingilieni kati sakata la walimu kutapeliwa na Afisa Elimu wao huko Katavi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

JFMemba

Senior Member
Joined
Jun 28, 2021
Posts
134
Reaction score
247
Walimu waliofanya kazi ya kusahihisha Mtihani wa Kidato cha Nne Kanda ya Nyanda za Juu mwezi Julai mwaka 2022 hawajalipwa pesa yao hadi leo na wamekuwa wakipewa ahadi hewa na bosi wao ambaye ni Afisa Elimu wa Mkoa wa Katavi.

TAMISEMI wasaidieni walimu walipwe haki yao maana inaonekana kama bosi huyo hajali yuko bize na mambo yake binafsi na pengine pesa imeshaliwa.

Pesa ilichangwa kutoka shule zote za sekondari tangu Julai hadi sasa walimu wanazungushwa tu na hakuna sababu yoyote ya kueleweka wamepewa.

Suala hili naamini Mkuu wa Mkoa anajua lakini sijajua kwanini kakaa kimya.

Mnasema mnawajali walimu sasa mbona wanadhulumiwa na mko kimya? Fuatilinieni suala hili linavunja ari ya walimu kufanya kazi.

Mikoa mingine yote wamelipwa siku nyingi siku nyingi isipokuwa Katavi tu.
 
Hii kazi ya ualimu ni ya hovyo sana.
Mzee baba wengine tunawaheshimu walimu balaa kwa sababu ndo walitufanya tuishi, tusome na tutor ujinga.
Sasa hivi naheshimu sana waokota makopp. Waliokota vyeti vyangu ambavyo wahuni wa kuvunja dirisha na kuazamia waliviiba na kuvitupa porini.
 
Walimu waliofanya kazi ya kusahihisha Mtihani wa kidato cha Nne kanda ya nyanda za juu mwezi Julai mwaka 2022 hawajalipwa pesa yao hadi leo na wamekuwa wakipewa ahadi hewa na bosi wao ambaye ni Afisa Elimu wa Mkoa wa Katavi.

TAMISEMI wasaidieni walimu walipwe haki yao maana inaonekana kama bosi huyo hajali yuko bize na mambo yake binafsi na pengine pesa imeshaliwa.

Pesa ilichangwa kutoka shule zote za sekondari tangu Julai hadi sasa walimu wanazungushwa tu na hakuna sababu yoyote ya kueleweka wamepewa.

Suala hili naamini Mkuu wa Mkoa anajua lakini sijajua kwanini kakaa kimya.

Mnasema mnawajali walimu sasa mbona wanadhulumiwa na mko kimya? Fuatilinieni suala hili linavunja ari ya walimu kufanya kazi.

Mikoa mingine yote wamelipwa siku nyingi siku nyingi isipokuwa Katavi tu.
Sasa kama mlitoa fedha wailwapa risiti?
Kama hamkupewa ndio imeshatoka hiyo
 
Back
Top Bottom