TAMISEMI, tuambieni kinachoendelea kwa sisi tuliokosa ajira za ualimu.

mwalimu wenu

JF-Expert Member
Joined
Feb 13, 2014
Posts
203
Reaction score
19
Inaelekea wiki ya 3 sasa tangu ajira zitolewe na sisi wengine kukosa,na mkadai kwamba suala letu mnalifanyia kazi.Iweje mnakaa kimya?
 
hata mimi nashangaaa labda wanasubiri watu wao wakaone mazingira wasipo yapenda ndo tupangiwe watoto wa wakulima, ambao pa1 na kutucheleweshea kutangaza ajira. wameweka pending majina yetu.
 
wako na sifa mchanganyiko kuna waliohitimu chuo cha St John Dodoma wote waliosoma bed, kuna baadhi ya waliomaliza stashahada na shahada za ualimu mwaka jana na kuna waliomaliza kipindi cha nyuma wakasup na kuzirudia hizo sup mwaka jana wakafaulu! Tamisemi walidai kuwa taarifa zao hazikufika hivo ilibidi wapeleke upya. Kiujumla hakuna watu maalumu walioachwa bali ni changanyikeni!
 
Ndugu yangu,mimi nimehitimu st.john(dom)BAED na hakuna BED sjut,tulikuwa 300+,na waliopata ajira ni watano tu.
 
Wakuu vumilieni by jumatatu post zenu zitarushwa, wory out ,alieniambia ni mmoja wao anaeprocess majina yenu TAMISEMI. By the way mko weng sana, hivo msijali
 
Serikali yetu ni sikivu, sio kiziwi hata kidogo imesha sikia kilio chenu na muda si mrefu mtapata ajira, tembeleeni website ya Tamisemi now and then.
 
Yaani hii Wizara - TAMISEMI siielewi kabisa, naona wamewapa ajira hata waalimu walihitimu masomo ili hali waliomba ruhusa. Je database ya Wizara haitumiki???
 
Yaani hii Wizara - TAMISEMI siielewi kabisa, naona wamewapa ajira hata waalimu walihitimu masomo ili hali waliomba ruhusa. Nawafahamu waalimu wengi walio katika utumishi kwa sasa, na wamepangiwa ajira mpya. Je database ya Wizara haitumiki???
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…