TAMISEMI vs Physical education students (UDSM)

stanb

Senior Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
153
Reaction score
19
Takribani wanafunzi 15 tulihitimu shahada hii (PHYSICAL EDUCATION) inayotolewa chuo kikuu dar es salaam pekee kwa hapa nchini.

Inashangaza kwa TAMISEMI kutoajiri wakufunzi wa vyuo vya ualimu kwa mwaka huu ambapo tungetumika ipasavyo, kama ivyokua kwa mwaka jana ambapo wanne kati ya 14 waliajiriwa vyuoni. Badala yake TAMISEMI imepanga wahitimu wote halmashauri. sera ya kupanga walimu vijijini iangalie na upande wa pili wa shilingi.

Asanteni.
 
Wewe naye! OWM TAMISEMI haiwezi kuajiri wakufunzi wa vyuo vya ualimu kwa sababu usimamizi wa vyuo bya ualimu uko chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, sio OWM TAMISEMI. Lakini pia kuna Waraka kwamba wakufunzi sasa hawatakuwa wanaajiriwa moja kwa moja kutoka vyuoni badala yake watakuwa wanapandishwa walimu wa sekondari au shule za msingi walioonesha umahiri katika ufundishaji wao na ambwo wana yeaching experience ya angalau miaka 3. Hata mshahara wa wakufunzi sasa uko juu kidogo ya walimu. Wanaanza na TGTS E.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…