Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kumekuwa na malalamiko ya wanafunzi na Wazazi wengi kupangiwa Tahasusi (Combinations) ambazo hawajazichagua hata kama wana vigezo vya kusoma tahasusi walizochagua.
Soma:
- KERO - Serikali mliangalie hili, inakuwaje mtu anachaguliwa kozi ambayo hajaomba?
- Serikali kuweni makini; inakuaje mtoto ana A ya math, B ya Chemistry, B ya biology na B ya Physics halafu mnampangia combination ya Art?!
Jamii Forums imewasiliana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini TAMISEMI, Nteghenjwa Hosseah kupata ufafanuzi wa malalamiko haya ambaye ameeleza:
Kuna mambo makuu 2 yanayozingatiwa wakati wa kuwapangia wanafunzi tahasusi
Alama anazotakiwa kufikisha mwanafunzi kwenye tahasusi husika (cut-off points
Mfano tahasusi ya PCB ina alama 7 lakini mwanafunzi akapata alama 6. Japokuwa wakati mwingine anaweza kuwa na alama zinazostahili lakini kila tahasusi ina ukomo wa kupokea wanafunzi kutokana na miundombinu iliyopo, idadi ikitimia waliobaki watapangiwa tahasusi nyingine
TAMISEMI waliulizwa pia inawafikishiaje ujumbe wananchi wanaotoa malalamiko yao kupitia mtandao, ambapo alisema;
Katika watu zaidi ya laki moja waliopangiwa shule malalamiko hayawezi kukosekana. Kati ya malalamiko yanayotolewa baadhi ni kutopangiwa shule wanazozitaka, wengi akilini mwao wana majina ya zile shule Kongwe 89, kila mzazi anatamani mtoto wake apangiwe kwenye hizo shule. Sasa hivi kuna shule 532, kila Wilaya na Mkoa zina shule mpya. Kila shule lazima zipelekewe Wanafunzi.
Tuna kituo cha Huduma kwa Wateja ambacho wote wenye malalamiko wanayawasilisha hapo, pale wanatoa maelezo, na kama muhusika hajaridhika na maelezo hayo atapewa mwongozo wa kufikisha malalamiko yako kwa Katibu Mkuu kwa kuandika barua na kuelezea anachokutana nacho, na ambacho hajaridhika nacho na kile anachoamini anastahili kukipata. Wakiipokea wataichambua wakiona kama ana sifa basi watambadilishia.
PIA SOMA
- TAMISEMI wafafanua utaratibu unaotakiwa kufatwa ikiwa mwanafunzi anataka kubadili tahasusi tofauti na aliyopangiwa
Soma:
- KERO - Serikali mliangalie hili, inakuwaje mtu anachaguliwa kozi ambayo hajaomba?
- Serikali kuweni makini; inakuaje mtoto ana A ya math, B ya Chemistry, B ya biology na B ya Physics halafu mnampangia combination ya Art?!
Jamii Forums imewasiliana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini TAMISEMI, Nteghenjwa Hosseah kupata ufafanuzi wa malalamiko haya ambaye ameeleza:
Kuna mambo makuu 2 yanayozingatiwa wakati wa kuwapangia wanafunzi tahasusi
Alama anazotakiwa kufikisha mwanafunzi kwenye tahasusi husika (cut-off points
Mfano tahasusi ya PCB ina alama 7 lakini mwanafunzi akapata alama 6. Japokuwa wakati mwingine anaweza kuwa na alama zinazostahili lakini kila tahasusi ina ukomo wa kupokea wanafunzi kutokana na miundombinu iliyopo, idadi ikitimia waliobaki watapangiwa tahasusi nyingine
TAMISEMI waliulizwa pia inawafikishiaje ujumbe wananchi wanaotoa malalamiko yao kupitia mtandao, ambapo alisema;
Katika watu zaidi ya laki moja waliopangiwa shule malalamiko hayawezi kukosekana. Kati ya malalamiko yanayotolewa baadhi ni kutopangiwa shule wanazozitaka, wengi akilini mwao wana majina ya zile shule Kongwe 89, kila mzazi anatamani mtoto wake apangiwe kwenye hizo shule. Sasa hivi kuna shule 532, kila Wilaya na Mkoa zina shule mpya. Kila shule lazima zipelekewe Wanafunzi.
Tuna kituo cha Huduma kwa Wateja ambacho wote wenye malalamiko wanayawasilisha hapo, pale wanatoa maelezo, na kama muhusika hajaridhika na maelezo hayo atapewa mwongozo wa kufikisha malalamiko yako kwa Katibu Mkuu kwa kuandika barua na kuelezea anachokutana nacho, na ambacho hajaridhika nacho na kile anachoamini anastahili kukipata. Wakiipokea wataichambua wakiona kama ana sifa basi watambadilishia.
PIA SOMA
- TAMISEMI wafafanua utaratibu unaotakiwa kufatwa ikiwa mwanafunzi anataka kubadili tahasusi tofauti na aliyopangiwa