Tamko la Idara, baada ya vigogo wa madawa ya kulevya duniani kutiwa nguvuni

Tamko la Idara, baada ya vigogo wa madawa ya kulevya duniani kutiwa nguvuni

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
25 July 2024

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Marekani, Bw. Merrick B. Garland Atoa Taarifa kuhusu Kukamatwa kwa Viongozi Wanaodaiwa wa Kundi la Sinaloa Bw. Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Bw. Joaquin Guzman Lopez​


viongozi wa genge la Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez watiwa nguvuni baada ya operesheni kabambe


Idara ya Sheria nchini Marekani imetoa taarifa ifuatayo kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Merrick B. Garland kuhusu kukamatwa kwa wanaodaiwa kuwa viongozi wa Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez:

"Idara ya Sheria imewaweka kizuizini viongozi wawili vigogo wanaodaiwa kuwa wa genge Sinaloa Cartel la nchini Mexico, mojawapo ya magenge yenye ukatili na yenye nguvu zaidi ya ulanguzi wa dawa za kulevya duniani.

Ismael Zambada Garcia, au "El Mayo," mwanzilishi mwenza wa Cartel, na Joaquin Guzman Lopez, mtoto wa mwanzilishi wake mwingine, walikamatwa leo huko El Paso, Texas.

Wanaume hao wawili wanakabiliwa na mashtaka mengi nchini Marekani kwa kuongoza operesheni za uhalifu za Cartel, ikiwa ni pamoja na mtandao wake hatari wa kutengeneza fentanyl na ulanguzi.

El Mayo na Guzman Lopez wanajiunga na orodha inayokua ya viongozi na washirika wa genge la Sinaloa Cartel ambao Idara ya Sheria inawajibisha nchini Marekani.

Hiyo inajumuisha mwanzilishi mwenza mwingine wa Cartel, Joaquin Guzman Loera, au “El Chapo”; mwana mwingine wa El Chapo na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Ovidio Guzman Lopez; na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Néstor Isidro Pérez Salas, au "El Nini."

Fentanyl ndio tishio baya zaidi la dawa za kulevya ambalo nchi yetu Marekani imewahi kukabili, na Idara ya Sheria haitapumzika hadi kila kiongozi wa kikundi, mwanachama, na mshirika anayehusika na kutia sumu hii katika jamii zetu watiwe mbaroni na wawajibike kwa biashara hii haramu.

Source : Attorney General Merrick B. Garland Statement on Arrests of Alleged Leaders of the Sinaloa Cartel Ismael Zambada Garcia (El Mayo) and Joaquin Guzman Lopez
 
Habari za kina mizizi ya kiongozi wa genge hilo la madawa ya kulevya duniani:

Hofu yatanda genge Sinaloa Cartel la nchini Mexico kulipiza kisasa kwa viongozi wa serikali ya Mexico

Habari zaidi zinasema kiongozi wa genge alirubuniwa kuingia katika ndege binafsi (private jet) nchini Mexico na kuelezwa wanaelekea katika jimbo moja ndani ya Mexico kuangalia uwanja mpya wa ndege utakaotumika kusafirishia madawa ya kulevya nje ya mipaka ya Mexico hususan Marekani kwenye soko kubwa la mateja.


View: https://m.youtube.com/watch?v=zLmgHStQBCA

Aliyefanya urubuni ni Joaquin Guzman Lopez mtoto wa kigogo Guzman, inasemekana ni kisasa cha mwana kwa Ismael Zambada Garcia (El Mayo) ambaye alimuuza babaye hadi akatiwa mbaroni

Joaquin Guzman Lopez mtoto alipanda private jet hiyo na kigogo Ismael Zambada Garcia (El Mayo), ambapo ndege hiyo ikaelekea El Paso Texas nchini Marekani na kusababisha kigogo huyo mkubwa kabisa aliyekuwa hakamatiki nchini Mexico kwa hogo kuingia katika mtego wa waMarekani kiurahisi.


View: https://m.youtube.com/watch?v=BFpOE2kukek

Tayari serikali ya Mexico imetoa taarifa kuwa haikuhusika na operesheni hiyo ya kukamatwa kigogo wa dawa za kulevya duniani Ismael Zambada Garcia (El Mayo), pengine ikihofia kutatokea mashambulizi kutoka genge la kigogo huyo kulipiza kisasa cha kuchuuzwa hadi kiongozi wa genge kutiwa mbaroni.
1722011259672.png

Ikumbukwe kuwa mwanzilishi mwenza mwingine wa genge / Cartel, Joaquin Guzman Loera, au “El Chapo alipotiwa mbaroni kulizuka vita mitaani kupinga serikali ya Mexico kumuuza El Chapo hadi akakamatwa na vyombo vya serikali ya Mexico kwa kushirikiana na Marekani.
 
Nani alikuwa bosi wa genge hatari la Sinaloa Cartel, ni El Chapo au El Mayo, uchambuzi wa kina unaamua :

El Mayo aliyeanza masuala akiwa na umri wa miaka 17 miaka ya 1960s ambaye aliishi kwa kutojionesha sana, mtu wa mipango mikubwa pia akili ya kuunda mikakati ili genge lifanikiwe au El Chapo mtu wa bata kwa sana kiasi akajulikana kote kutokana na kuishi kwa anasa kubwa bila kificho, kuburuza watu waziwazi mitaani kwa mkono wa chuma uliojaa damu ...


El Mayo: The Real Boss Of Sinaloa Cartel

View: https://m.youtube.com/watch?v=D35KWQu89lc&pp=ygUORWwgTWF5byBib3VudHk%3D
 
25 July 2025

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Marekani, Bw. Merrick B. Garland Atoa Taarifa kuhusu Kukamatwa kwa Viongozi Wanaodaiwa wa Kundi la Sinaloa Bw. Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Bw. Joaquin Guzman Lopez​


viongozi wa genge la Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez watiwa nguvuni baada ya operesheni kabambe


Idara ya Sheria nchini Marekani imetoa taarifa ifuatayo kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Merrick B. Garland kuhusu kukamatwa kwa wanaodaiwa kuwa viongozi wa Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez:

"Idara ya Sheria imewaweka kizuizini viongozi wawili vigogo wanaodaiwa kuwa wa genge Sinaloa Cartel la nchini Mexico, mojawapo ya magenge yenye ukatili na yenye nguvu zaidi ya ulanguzi wa dawa za kulevya duniani.

Ismael Zambada Garcia, au "El Mayo," mwanzilishi mwenza wa Cartel, na Joaquin Guzman Lopez, mtoto wa mwanzilishi wake mwingine, walikamatwa leo huko El Paso, Texas.

Wanaume hao wawili wanakabiliwa na mashtaka mengi nchini Marekani kwa kuongoza operesheni za uhalifu za Cartel, ikiwa ni pamoja na mtandao wake hatari wa kutengeneza fentanyl na ulanguzi.

El Mayo na Guzman Lopez wanajiunga na orodha inayokua ya viongozi na washirika wa genge la Sinaloa Cartel ambao Idara ya Sheria inawajibisha nchini Marekani.

Hiyo inajumuisha mwanzilishi mwenza mwingine wa Cartel, Joaquin Guzman Loera, au “El Chapo”; mwana mwingine wa El Chapo na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Ovidio Guzman Lopez; na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Néstor Isidro Pérez Salas, au "El Nini."

Fentanyl ndio tishio baya zaidi la dawa za kulevya ambalo nchi yetu Marekani imewahi kukabili, na Idara ya Sheria haitapumzika hadi kila kiongozi wa kikundi, mwanachama, na mshirika anayehusika na kutia sumu hii katika jamii zetu watiwe mbaroni na wawajibike kwa biashara hii haramu.

Source : Attorney General Merrick B. Garland Statement on Arrests of Alleged Leaders of the Sinaloa Cartel Ismael Zambada Garcia (El Mayo) and Joaquin Guzman Lopez
Wamarekani wao ni "you are either with us or you're against us". Wamarekani ni wanafik sana.

Wakiwa wanataka kuianzishia nchi mabalaa na iwe kwenye himaya yao basi wanaanza kuwajazia kila madhambi humo, madawa ya kulevya yatapatikana na kuingizwa kwa wepesi, picha za ngono na mitandao michafu itashindwa kuzuwiwa kwenye sattellites na mitandao. Pombe zitakuwa rahisi sana na zinapatikana kwa wepesi kuliko chakula.

Hao mashetani wanatumia kila ovu kama silaha yao bila wajinga ndiyo waliwao kujielewa.

Rejea Iran Contra.
 
25 July 2025

Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Marekani, Bw. Merrick B. Garland Atoa Taarifa kuhusu Kukamatwa kwa Viongozi Wanaodaiwa wa Kundi la Sinaloa Bw. Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Bw. Joaquin Guzman Lopez​


viongozi wa genge la Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez watiwa nguvuni baada ya operesheni kabambe


Idara ya Sheria nchini Marekani imetoa taarifa ifuatayo kutoka kwa Mwanasheria Mkuu Merrick B. Garland kuhusu kukamatwa kwa wanaodaiwa kuwa viongozi wa Sinaloa Cartel, Ismael Zambada Garcia (El Mayo) na Joaquin Guzman Lopez:

"Idara ya Sheria imewaweka kizuizini viongozi wawili vigogo wanaodaiwa kuwa wa genge Sinaloa Cartel la nchini Mexico, mojawapo ya magenge yenye ukatili na yenye nguvu zaidi ya ulanguzi wa dawa za kulevya duniani.

Ismael Zambada Garcia, au "El Mayo," mwanzilishi mwenza wa Cartel, na Joaquin Guzman Lopez, mtoto wa mwanzilishi wake mwingine, walikamatwa leo huko El Paso, Texas.

Wanaume hao wawili wanakabiliwa na mashtaka mengi nchini Marekani kwa kuongoza operesheni za uhalifu za Cartel, ikiwa ni pamoja na mtandao wake hatari wa kutengeneza fentanyl na ulanguzi.

El Mayo na Guzman Lopez wanajiunga na orodha inayokua ya viongozi na washirika wa genge la Sinaloa Cartel ambao Idara ya Sheria inawajibisha nchini Marekani.

Hiyo inajumuisha mwanzilishi mwenza mwingine wa Cartel, Joaquin Guzman Loera, au “El Chapo”; mwana mwingine wa El Chapo na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Ovidio Guzman Lopez; na anayedaiwa kuwa kiongozi wa Cartel, Néstor Isidro Pérez Salas, au "El Nini."

Fentanyl ndio tishio baya zaidi la dawa za kulevya ambalo nchi yetu Marekani imewahi kukabili, na Idara ya Sheria haitapumzika hadi kila kiongozi wa kikundi, mwanachama, na mshirika anayehusika na kutia sumu hii katika jamii zetu watiwe mbaroni na wawajibike kwa biashara hii haramu.

Source : Attorney General Merrick B. Garland Statement on Arrests of Alleged Leaders of the Sinaloa Cartel Ismael Zambada Garcia (El Mayo) and Joaquin Guzman Lopez
Bado El Mencho...
 
Uyo Guzman

Ni Joaquin Guzman Lopez ambaye ni mtoto wa kigogo El Chapo, ndiye ambaye amekamatwa akiwa na kigogo mkuu El Mayo walipowasili El Paso Texas US....

El Chapo ni kigogo mwenza wa Ismael Zambada Garcia (El Mayo) aliyekamatwa uwanja wa ndege El Paso Texas US.

Picha ya 'El Chapo' huyu hapa chini jina kamili Joaquín Archivaldo Guzmán Loera a.k.a El Chapo.

1722028948107.png

Watu waongeao kispanyoola na walioasili utamaduni majina ya mama zao huwa mwisho ndiyo maana huwa majina manne, la mwisho ni la upande wa mama Lopez kwa mtoto wa El Chapo na baba El Chapo utaona jina linaishi Loera la upande wa mama yake mzazi El Chapo


Soma kwa kina habari kamili: Attorney General Merrick B. Garland Statement on Arrests of Alleged Leaders of the Sinaloa Cartel Ismael Zambada Garcia (El Mayo) and Joaquin Guzman Lopez
 
Dau la Wanted kwa El Mayo, ambaye aliishi kwa usiri mkubwa bila kujulikana alipo

DAU ALOWEKEWA AKIWA ANASAKWA (WANTED) US$ 15,000,000 KWA WATAKAO TOA TAARIFA SIRI

1722032472453.png

Ismael Zambada Garcia ' El Mayo'​

Zawadi nono : HADI $15 MILIONI

Anatafutwa kwa madai yafuatayo ya ukiukaji wa sheria za shirikisho (federal)​

Madai yafuatayo ya Ukiukaji wa sheria ya Shirikisho kuhusu madawa ya kulevya : 1) 18 USC Sec 1962 (d) Njama ya RICO; 2) 21 USC 846 na 841 (a)(1) Njama ya Kumiliki Madawa Yanayodhibitiwa, zaidi ya kilo 5 za kokeini na zaidi ya kilo 1000 za bangi; 3) 21 USC 963952(a) na 960(a)(b)(1)(B) na (G); Njama ya kuingiza bidhaa inayodhibitiwa, zaidi ya kilo 5 za kokeini na zaidi ya kilo 1,000 za bangi;4)18 USC 1956 Njama ya kutakatisha pesa; 5)18 USC 2 & 924(o) Njama ya kumiliki bunduki katika kuendeleza uhalifu wa ulanguzi wa dawa za kulevya na usaidizi; 6 hadi 10) 18 USC 2 & 1959(a) (1)&(5); Uhalifu wa Kikatili katika kusaidia shughuli za ulaghai na kusaidia na kusashawishi uvunjwaji sheria; 11) 21 USC 848 (e)(1)(A) Mauaji wakati wa kushiriki au kufanya kazi katika kuendeleza biashara ya uhalifu au ulanguzi wa dawa za kulevya; 12) 21 USC 848(b)(1) na (2)(A) Kujihusisha na biashara ya uhalifu inayoendelea katika kuendeleza ulanguzi wa dawa za kulevya; 13) 18 USC 956 Njama ya kuua katika nchi ya kigeni; na (14) 18 USC 2 & 1201 Utekaji nyara na usaidizi na ushawishi wa kuvunja sheria .

Source : DEA
 
Dau la Wanted kwa El Mayo, ambaye aliishi kwa usiri mkubwa bila kujulikana alipo

DAU ALOWEKEWA AKIWA ANASAKWA (WANTED) US$ 15,000,000 KWA WATAKAO TOA TAARIFA SIRI

View attachment 3053265

Ismael Zambada Garcia ' El Mayo'​

Zawadi nono : HADI $15 MILIONI

Anatafutwa kwa madai yafuatayo ya ukiukaji wa sheria za shirikisho (federal)​

Madai yafuatayo ya Ukiukaji wa sheria ya Shirikisho kuhusu madawa ya kulevya : 1) 18 USC Sec 1962 (d) Njama ya RICO; 2) 21 USC 846 na 841 (a)(1) Njama ya Kumiliki Madawa Yanayodhibitiwa, zaidi ya kilo 5 za kokeini na zaidi ya kilo 1000 za bangi; 3) 21 USC 963952(a) na 960(a)(b)(1)(B) na (G); Njama ya kuingiza bidhaa inayodhibitiwa, zaidi ya kilo 5 za kokeini na zaidi ya kilo 1,000 za bangi;4)18 USC 1956 Njama ya kutakatisha pesa; 5)18 USC 2 & 924(o) Njama ya kumiliki bunduki katika kuendeleza uhalifu wa ulanguzi wa dawa za kulevya na usaidizi; 6 hadi 10) 18 USC 2 & 1959(a) (1)&(5); Uhalifu wa Kikatili katika kusaidia shughuli za ulaghai na kusaidia na kusashawishi uvunjwaji sheria; 11) 21 USC 848 (e)(1)(A) Mauaji wakati wa kushiriki au kufanya kazi katika kuendeleza biashara ya uhalifu au ulanguzi wa dawa za kulevya; 12) 21 USC 848(b)(1) na (2)(A) Kujihusisha na biashara ya uhalifu inayoendelea katika kuendeleza ulanguzi wa dawa za kulevya; 13) 18 USC 956 Njama ya kuua katika nchi ya kigeni; na (14) 18 USC 2 & 1201 Utekaji nyara na usaidizi na ushawishi wa kuvunja sheria .

Source : DEA
Kwanini imekuwa vigumu kwa taifa kubwa kijeshi na kiuchumi la Marekani kuyasambaratisha haya magenge ya wauza unga hapo Mexico (Cartels) ?

T14 Armata
 
Kwanini imekuwa vigumu kwa taifa kubwa kijeshi na kiuchumi la Marekani kuyasambaratisha haya magenge ya wauza unga hapo Mexico (Cartels) ?

T14 Armata

Mateja wa nchini Marekani wasipopata uraibu wao, wataandamana na kufanya fujo, bora waendelee kupata dozi nchi iwe tulivu.
 
Mateja wa nchini Marekani wasipopata uraibu wao, wataandamana na kufanya fujo, bora waendelee kupata dozi nchi iwe tulivu.
Ila hilo la madawa ya Kulevya hapo Marekani ndio limesababisha mauaji, uhalifu na kuvurugika usalama na utulivu wa kijamii hapo Mexico na nchi zote za America ya Kusini.
 
Ila hilo la madawa ya Kulevya hapo Marekani ndio limesababisha mauaji, uhalifu na kuvurugika usalama na utulivu wa kijamii hapo Mexico na nchi zote za America ya Kusini.

Huku utulivu ukipatikana katika mitaa, vitongoji na miji ya nchini Marekani.

Nchi zote za Marekani ya Kaskazini, ulaya ya magharibi wanatambua umuhimu wa kitu hiki kutuliza jamii, ama sivyo wataamka na kuanza kuona mambo wasiyostahili kuona ya tofauti kubwa baina ya walionacho na wasio kuwa nacho, tofauti ya elimu, huduma za afya n.k katika jamii zao.
 
Huku utulivu ukipatikana katika mitaa, vitongoji na miji ya nchini Marekani.

Nchi zote za Marekani ya Kaskazini, ulaya ya magharibi wanatambua umuhimu wa kitu hiki kutuliza jamii, ama sivyo wataamka na kuanza kuona mambo wasiyostahili kuona ya tofauti kubwa baina ya walionacho na wasio kuwa nacho, tofauti ya elimu, huduma za afya n.k katika jamii zao.
Yaani na wao wanaiunga mkono hiyo biashara?.....sio rahisi
 
Back
Top Bottom