"Tamko la Pinda"

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Hii imeingia sasa hivi kutoka "ndani"... Inadaiwa kuwa ni tamko ambalo Pinda anatarajiwa kutoa kesho au wakati wowote kama sakata hili la kauli yake litaendelea hasa baada ya baadhi ya Wabunge hata wa ndani ya CCM kutoridhika moja kwa moja na maelezo yake katika kipindi cha maswali na majibu leo huko Bungeni.




NB: Sijaweza kuthibitisha ukweli au usahihi wa taarifa hiyo. Muda ndio utasema.
 
Okay...sioni ubaya wowote. Angalau amekiri kuwa kachemsha na kwamba yuko tayari wabunge wenzake wampigie kura ya kuwa au kutokuwa na imani naye....
 
Kwa hiyo bado mnataka ajiuzuru?
 
ok as long as ni binadamu hawezi kuwa perfect katika matendo yake ya kila siku.
amekosea,amekiri,muacheni aendelee kuchapa kazi.
 
Kazi kubwa ipo mbeleni iwapo PM anakuwa na uwezo mdogo hivi, atawezaje kutia chachu ya maendeleo? Heri ya Lowassa!!!
 
Kwa upande mwingine mimi namsamehe kwa sababu kwa kweli inasikitisha na kutia hasira kuona ma-albino wakiuwawa hivyo. So kama alivyosema, ali react kihisia zaidi jambo ambalo ni la kibinadamu na amekuwa muungwana kukiri na kukubali makosa. Sasa what else do you people want?
 
Kazi kubwa ipo mbeleni iwapo PM anakuwa na uwezo mdogo hivi, atawezaje kutia chachu ya maendeleo? Heri ya Lowassa!!!

You kidding me! unaona heri ya fisadi kuliko aliyeteleza ulimi, tena inasemekana kakiri kakosea.

Yaani heri ya Lowassa aliyeiba na akagoma kuwa kaiba, na kuonyesha kuwa hana mshipa wa aibu, bado anapiga ndogo ndogo tena chafu arudi madarakani, huyu kwako ni wa heri......kazi ipo mbeleni.
 
Kazi kubwa ipo mbeleni iwapo PM anakuwa na uwezo mdogo hivi, atawezaje kutia chachu ya maendeleo? Heri ya Lowassa!!!

Yah heri ya lowasa alikuwa na uwezo mkubwa mpaka akatuletea richmond na ile ndege yake ya uchumi...
 
Sidhani kama PM Pinda anaweza kutoa hotuba ya kukubali makosa namna hiyo.
 
Yah heri ya lowasa alikuwa na uwezo mkubwa mpaka akatuletea richmond na ile ndege yake ya uchumi...

Msisahau shule za sekondari za kizima moto kwenye kata zenu, ambazo hazina waalimu, Lowassa for PM
 
Okay...sioni ubaya wowote. Angalau amekiri kuwa kachemsha na kwamba yuko tayari wabunge wenzake wampigie kura ya kuwa au kutokuwa na imani naye....

Kwa hiyo bado mnataka ajiuzuru?

ok as long as ni binadamu hawezi kuwa perfect katika matendo yake ya kila siku.
amekosea,amekiri,muacheni aendelee kuchapa kazi.

Iwapo hiyo stament hapo juu itakuwa ya Mh. Pinda, basi mimi kama mwananchi nimeshamsamehe. Kosa ni pale atakaporudia kosa. Wale ninaowaona wapotoshaji zaidi katika sakata hili zima ni wale ambao wanakimbilia kuzima zima kila aina ya soo litokealo au kuanzishwa na moja ya viongozi wetu serikalini kwa tactics angamizi. Tabia hii ya kufukiafukia na kufunika uozo pale tuuonapo na pale unapotokea ndiyo hiyo inayo tuangamizia Taifa letu.
 
Ala! kumbe hakuna hata uhakika kuwa hilo ni tamk lake....what ze hell is going on?
 
Watanzania bwana.......yaani watapiga porojoo weee kakiri wazi nimemsikia na katoa machozi.....sasa mnataka nini? kuna mambo mengi ya kujadili sio hili
 
Kwa hiyo bado mnataka ajiuzuru?

endapo atatoa tamko hili mimi nitamsamehe kabisa wala sitataka ajiuzuru. Mpaka sasa bado hajatoa tamko la kuomba radhi wala kufuta agizo lake au kujutia kauli yake inayokiuka katiba ya nchi.
 
Mimi nitamuona bingwa akiomba radhi. wanasiasa wengi hawajawahi kuomba radhi kwa style hiyo, sijui ni utamaduni wetu wa kisiasa au utamaduni wetu kama waafrika. Jimwage PM kama kuna nia hiyo. Changanya na kauli zote zenye utata, kwa kutoa ufafanuzi au kuomba radhi
 
Jamani nadhani tujifunze utamaduni wa kujiuzuru, kama kakili kosa basi awe tayari kuachia ngazi, kuna watanzania zaidi ya mil 40. Wapo watakaoweza ilinda katiba yetu. Asamehewe kwa sababu kakubari makosa si sababu ya kuachiwa, huyu Mh Pinda ameisha toa kauli tata nyingi mno tokea aingia madarakani....hapa sasa he should swallow the bitter pills....
 
endapo atatoa tamko hili mimi nitamsamehe kabisa wala sitataka ajiuzuru. Mpaka sasa bado hajatoa tamko la kuomba radhi wala kufuta agizo lake au kujutia kauli yake inayokiuka katiba ya nchi.
hujamsikia redioni akikiri wazi na machozi kumtoka?? au unataka akutumie Email?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…