Tamu na chungu ulizopitia wakati unaanza biashara yako

Katika ufugaji

ni bora ufuge mbwa wa kisasa watakulipa haraka na hawakupi stress na siyo kuku wa kisasa masharti kibao

wahenga wanasema ujinga ni kwenda tu na siyo kurudi

pambana.
Mkuu hao mbwa wa kisasa ni kweli wanafugwa au msemo tu?
 
Kwanza hongera kwa ujasiri wa kuamka na kuzama chimbo,tena usilolijua,na hili swala la bidhaa za kilimo aisee unaweza ukafurahi ila siku bei ikishuka unaweza changanyikiwa
 
Nakumbuka nilikuwa na dem huyo....yan yeye aliamini kwenye ajira...aliona cwezi biashara kabsaaaa...!!na ubaya zaidi mimi nd nlmpenda mno so mostly mtaji ulienda kwake kwa vizawadi na vijihela vya shule

Dem anajua hali n ngum...sina ajira...na ndo kwanza naanza biashara anauliza "lini utakuwa na kwako?"

Msekemseke mwsho wa siku nkaamua tuachane....hapo nd nkapata hasira zaidi ya kutafta

Nilipambana kwa hali na mali
Nilijinyima just kuprove kuwa nnaweza
Nilitafta ushaur wa kibiashara mitandaon na kwa wafanyabiashara wenzangu....!!

Kuna watu nakumbuka walinicheka wkt naagza bidhaa za elf 30...!!lakini now tunaheshimiana maana nnaagiza mpk za laki 3

Biashara imenona
Nmepanga na chumba kimejaa
Kiwanja mwakani natk kuanza ujenzi

Juzi juzi yule kima akataka kurudi...!!nikakumbuka kuwa yawezekana nmefanikiwa kwakuwa sipo nae....!!nikampa jibu simple "siwezi kukuamini tena"

Biashara zina chngamoto zake....lkn znazotuua ni changamoto za nje...!!
 
Duuh bei ilishukaje fastaa hivyooo...!![emoji23][emoji23][emoji23][emoji119]
 
Hakikaa mkuuu...!!
 
Kwanza hongera kwa ujasiri wa kuamka na kuzama chimbo,tena usilolijua,na hili swala la bidhaa za kilimo aisee unaweza ukafurahi ila siku bei ikishuka unaweza changanyikiwa
Nilichanganyikiwa mkuu maana sikuamini kama soko lingebadilika gafla namna ile
 
Alikuwa anakopesha sana au kutoa bidhaa bure
Ndugu mkewangu ni mrokole ana imani kali sana anasali karibia siku zote za week, hata chanzo cha kufilisi duka ni sababu alikuwa anafungu muda mchache muda mwingi yuko kanisani
 
Biashara ni ngumu kwavile imeambatana na changamoto ambazo wakati mwingine ni vigumu kuziepuka.

Mfano:

1. Uzoefu
2. Uaminifu
3. Uvumilivu
4. Usimamizi n.k

Kwanza nilianza na ufugaji wa nguruwe mmoja jike. Nikaenda nae vizuri tu. Kushika mimba, kabla hajajifungua akaanza kuumwa. Akawa anakosa nguvu za miguu, kuna jamaa mfugaji mzoefu, nilipomuelezea akasema kuna sindano inabidi achomwe. Tulipomchoma ile sindano, baada ya siku mbili mimba ikatoka. Nguruwe akaja akapona. Akashika mimba nyingine na kujifungua vitoto 5,mmoja akafa. Tukaenda nao pia fresh, ila wanakula kupita maelezo. Vilipoacha kunyonya, tukauza 3 kimoja kikabaki. Baada ya kuona uelekeo sio, mama mtu nikachinja na kuuza nyama buchani. Hela haikurudi. Nikapiga chini huo mradi.


Nikasogea kwenye kilimo. Tikiti na maharage. Hudumia sana shamba. Kwenye kuvuna, tikiti ilinipiga hasara moja matata sana. Nikapiga chini. Nikahamia kwenye kusafirisha maharage toka mkoani kuleta Dar. Nilichora mchoro vizuri tu. Nikanunua mzigo wa kutosha na kuuagiza uje mjini. Huku town alikuwepo jamaa yangu mmoja, mtu wa karibu sana (alikuwa mtu wa karibu sana, maana sio wa karibu tena). Jamaa akaupokea mzigo na kuusimamia kwa wale madalali wauzaji. Daily ananipa mrejesho wa maendeleo, nikawa nafurahishwa na bidii yake. Kumbe daily anaenda kuchukua hela alaf anaweka heshima mitaani na bar (mimi sina habari). Kuja kustuka, kashakula hela 75%, huku mimi ananiongopea madalali hawajampa bado. Biashara ikafa.


Nikageukia kwenye tangawizi. Nikalima vizuri na kila kitu kikawa chini ya usimamizi wangu mwenyewe. Kwenye mavuno mambo hayakwenda vizuri, ila walau niliona mwanga fulani hivi. Ikabidi niwekeze tena kwenye ili zao. Msimu wa pili kilichotokea ni afadhali ya msimu wa kwanza. Kama sijapalaraizi shambani, basi sidhani kama ntakuja kupalaraizi maishani mwangu. Kifupi shambani kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua, zaidi ya hapo niliwafaidisha wao tu mimi sikupata kingine. Nikasema kilimo kwangu bye bye, siingii shambani tena.

Nikaamua kufungua duka la nafaka kwa reja reja. Ushindani niliokutana nao sio wa kawaida. Mara leo mtu aje kuulizia, then anakwambia ntarudi kuchukua kiasi kadhaa siku nyingine. Kumbe nae anafanya biashara hiyo hiyo so alikuja kunichunguza. Mara wamama watake mkopo. Kipindi mchele umekuwa hadimu mtaani, bei ya chini ilikuwaga 1500 kwa kilo, ila watu wanataka mchele wa 1300,tabu tupu. Baada ya miezi 4,nikaamua kupiga chini. Maana mzunguko ulikuwa mdogo saaana, nikawa namfaidisha mwenye fremu tu.


Kutokea hapo ndio nikaamua kuwekeza kwenye kitu kingine kabisa, tena nilianza na mtaji wa 1.5 milions. Nikaamua kusimamia mwenyewe mwanzo mwisho, hapo atleast ndio mwanga kidogo ukaonekana. Now nafikiria ni jinsi gani nitaitanua .

***** ****** ****** ******

Biashara zinahitaji kujitoa. Ukiweza kuweka hela yako sehemu, basi hakikisha unaweza kuweka na muda wako. Vinginevyo utaishia kufaidisha wengine.
 
biashara gan
 
H

Hongera sana mkuu kwa kutoa point ya mbolea. Maana sio siri zile comments zako za
"Ngoja waje, kukupa muongozo.........
Cc: mahondaw "
zinakeraga basi tu, ni vile tu kila mtu ana uhuru wa kupost anachotaka
mwanangu ww kama mm yaan huwa znaniboha knyama mpaka nauliza huyu jamaa kama hana cha kucomment si apite kimya ???yaan kila post yy anaandika "ngoja waje" huwa ananikata maini kinyama mpakq huwa naclose app dadeq yaan nakerekaga asee yaan naboreka ase e kama huna cha kucomment uwe unapita kimya kimya mzee for sure watu huwa tunaboreka
 
bidhaa za chakula hazinaga specific price sjui kwa nn yaan znahtaji umakn sana
 
kuwa makn nakwambia tena kuwa makini...hz dini za sku hz kila mtu mchungaji na hujui ye mke wako anashnda anafanya ktu gan huko kansani...neno kanisani lisikupe upofu mzee
Ndugu mkewangu ni mrokole ana imani kali sana anasali karibia siku zote za week, hata chanzo cha kufilisi duka ni sababu alikuwa anafungu muda mchache muda mwingi yuko kanisani
 
kitu pekee nilichoambulia ni kuitwa bossi na wale vibarua,

asee huwa naumia sana moyo unakuta unaitwa boss,mkuu,mheshmiwa lakn moyon unaujua ukweli kwamba hata chai hujanyww
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…