TAMWA na TCRA waandaa Tuzo za Umahiri za Waandishi wa Habari 'Samia Kalamu Awards 2024'

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake (TAMWA) kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wameandaa tuzo za umahiri kwa waandishi wa habari Watanzania zinazojulikana kwa jina la “Samia Kalamu Awards 2024.”

Zoezi la kutoa tuzo hizo linatarajiwa kufanyika Novemba mwaka huu 2024 kwa kushirikisha Wanahabari wote nchini kwa kuhusisha habari zilizochapishwa kati ya Januari mosi hadi Oktoba 26, 2024 kwenye magazeti, redio, televisheni na majukwaa ya mtandaoni.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Oktoba 13, 2014, Mkurugenzi Mtendaji wa TAMWA Dkt Rose Reuben amebainisha sababu zilizopelekea wao kuja na tuzo hizo.

Soma Pia: Utoaji wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT), leo September 28, 2024

Kwa upande wake, Meneja wa Kitengo cha Huduma za Utangazaji kutoka TCRA, Mha. Andrew Kisaka amesema kuwa wameamua kushirikiana na TAMWA ili kuwa na mkazo wa uandishi wa makala ambazo zinahimiza na kuhamasisha maudhui ya ndani.

Your browser is not able to display this video.
 
Haya matangazo kila mahali ni ya nini hasa? Hivi kama unakubalika matangazo yote ya nini? Kwanini Viongozi wetu wanakuwa ving'ang'anizi kiasi hiki kwenye nafasi walizonazo? Kuna biashara gani Ikulu?
 
Uchawa imekuwa taaluma sasa, hapo hakuna zaidi ya kutafuta fursa tu.

Hivi TAMWA mmekuaje, nani kawaroga, huyo TCRA , polisi wa Vyombo vya habari, kawa malaika kwenu au kwa vile wengi hampo newsrooms😳
 
Naomba Kura yako katika kipengele Cha Habari za Kisekta Sekta ya Maji na Nishati jina Isack Dickson Lukumay tumia Link pia Samia Kalamu Awards
 

Attachments

  • kura.png
    1.3 MB · Views: 1
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…