Mwakanshahala
New Member
- Mar 31, 2022
- 1
- 0
Wana jamvi nashindwa kuelewa kama sehemu zingine za nchi hii zinapata shida ya kuunganishiwa umeme kama Nzega haswa Nzega Mjini.
Kumekua na changamoto kubwa ya kupatiwa huduma ya maunganisho ya umeme hata baada ya kufanya malipo. Mfano mteja anafanya malipo na ndani ya miezi miwili, mitatu wakati mwingine mpka mitano hapewi huduma ya umeme.
Mteja akifatilia mara nyingi majibu ni mepesi yasioridhisha kwamba vifaa hakuna, wakati mwingine watakwambia network ya kusajili inasumbua n.k.
Lakini cha kushangaza mteja akijiongeza, namaanisha akinyoosha mkono yaani akitoa fedha kwa vijana ambao wametengeneza kama ka syndicate unafungiwa umeme ndani ya masaa machache.
Wale ambao uwezo wao ni mdogo wamekua wahanga wakubwa wa hili tatizo. Mwisho wa siku binafsi naona kama ni hujuma kwa shirika maana kupatikana kwa wateja wapya naamini ndivyo mapato ya shirika yanavyoongezeka.
Kumekua na changamoto kubwa ya kupatiwa huduma ya maunganisho ya umeme hata baada ya kufanya malipo. Mfano mteja anafanya malipo na ndani ya miezi miwili, mitatu wakati mwingine mpka mitano hapewi huduma ya umeme.
Mteja akifatilia mara nyingi majibu ni mepesi yasioridhisha kwamba vifaa hakuna, wakati mwingine watakwambia network ya kusajili inasumbua n.k.
Lakini cha kushangaza mteja akijiongeza, namaanisha akinyoosha mkono yaani akitoa fedha kwa vijana ambao wametengeneza kama ka syndicate unafungiwa umeme ndani ya masaa machache.
Wale ambao uwezo wao ni mdogo wamekua wahanga wakubwa wa hili tatizo. Mwisho wa siku binafsi naona kama ni hujuma kwa shirika maana kupatikana kwa wateja wapya naamini ndivyo mapato ya shirika yanavyoongezeka.